Kasiano Muyenzi
JF-Expert Member
- Feb 3, 2018
- 13,972
- 22,922
Nimeshawahi kupoteza VITU ambavyo niliamini bila kuwa navyo sitaweza kuishi vizuri.
Nimeshawahi kupoteza WATU ambao niliamini bila kuwa nao sitaweza kufika ninakokwenda.
Nimeshawahi kupoteza NAFASI ambazo niliamini nikizikosa sitaweza kutimiza malengo yangu tena.
Kuna wakati unafika katika maisha UNAJIAMINISHA MOYONI...
.
...au unaaminishwa na WANAOKUZUNGUKA kuwa bila MTU FULANI au KITU fulani basi ndio utakuwa MWISHO wa safari yako.
Katika nyakati kama hizo niliwahi kupewa neno la HEKIMA ambalo limekuwa msaada mkubwa sana siku zote za maisha yangu.
Niliambiwa kuwa “Sio kila UNAYEMPOTEZA au kila UNACHOPOTEZA ni HASARA KWAKO”.
Ukiambiwa neno hili katikati ya maumivu hauwezi kuelewa.
Ila baada ya muda nimegundua lina ukweli ndani yake.
Kuna mabadiliko lazima yatokee kwanza ili uwe vile unavyotaka.
Kuna watu ambao lazima WAONDOKE kwenye maisha yako usogee hatua unayopata.
Kuna wengine inalazimika wapoteze kazi zao za sasa ili wapate kazi kubwa zaidi.
Kuna wengine inalazimika WAKATALIWE kwenye mambo fulani ili wapate hasira ya kufanya kitu wanachotakiwa kufanya.
Kuna wakati mtu unakuwa “so relaxed” na hautaki kusumbuliwa kwa namna yoyote.
Mungu anapokuangalia anajua ukiendelea hivyo HAUTAKUWA vile unatakiwa KUWA na HAUTAFIKA kule unatakiwa KUFIKA.
Lazima meli ipitie DHORUBA ili UTUPWE BAHARINI na umezwe na SAMAKI kisha akakutapike unakotakiwa kwenda.
Sio kila DHORUBA inapokuja, ukimuomba MUNGU ataiondoa.
NYINGINE AMEILETA ili: AKUTENGE na baadhi ya VITU, akutoe katikati ya WATU FULANI...
..au akutoe kwa LAZIMA eneo ambalo ukiendelea kuwepo UTADUMAA na utashindwa kufikia kilele cha MAFANIKIO YAKO.
Nakuombea AKILI yako ifunguke na USING’ANG’ANIE WATU ambao unatakiwa kuachana nao.
Somo kwa hisani ya Joel Nanauka
#timizamalengoyako.
Nimeshawahi kupoteza WATU ambao niliamini bila kuwa nao sitaweza kufika ninakokwenda.
Nimeshawahi kupoteza NAFASI ambazo niliamini nikizikosa sitaweza kutimiza malengo yangu tena.
Kuna wakati unafika katika maisha UNAJIAMINISHA MOYONI...
.
...au unaaminishwa na WANAOKUZUNGUKA kuwa bila MTU FULANI au KITU fulani basi ndio utakuwa MWISHO wa safari yako.
Katika nyakati kama hizo niliwahi kupewa neno la HEKIMA ambalo limekuwa msaada mkubwa sana siku zote za maisha yangu.
Niliambiwa kuwa “Sio kila UNAYEMPOTEZA au kila UNACHOPOTEZA ni HASARA KWAKO”.
Ukiambiwa neno hili katikati ya maumivu hauwezi kuelewa.
Ila baada ya muda nimegundua lina ukweli ndani yake.
Kuna mabadiliko lazima yatokee kwanza ili uwe vile unavyotaka.
Kuna watu ambao lazima WAONDOKE kwenye maisha yako usogee hatua unayopata.
Kuna wengine inalazimika wapoteze kazi zao za sasa ili wapate kazi kubwa zaidi.
Kuna wengine inalazimika WAKATALIWE kwenye mambo fulani ili wapate hasira ya kufanya kitu wanachotakiwa kufanya.
Kuna wakati mtu unakuwa “so relaxed” na hautaki kusumbuliwa kwa namna yoyote.
Mungu anapokuangalia anajua ukiendelea hivyo HAUTAKUWA vile unatakiwa KUWA na HAUTAFIKA kule unatakiwa KUFIKA.
Lazima meli ipitie DHORUBA ili UTUPWE BAHARINI na umezwe na SAMAKI kisha akakutapike unakotakiwa kwenda.
Sio kila DHORUBA inapokuja, ukimuomba MUNGU ataiondoa.
NYINGINE AMEILETA ili: AKUTENGE na baadhi ya VITU, akutoe katikati ya WATU FULANI...
..au akutoe kwa LAZIMA eneo ambalo ukiendelea kuwepo UTADUMAA na utashindwa kufikia kilele cha MAFANIKIO YAKO.
Nakuombea AKILI yako ifunguke na USING’ANG’ANIE WATU ambao unatakiwa kuachana nao.
Somo kwa hisani ya Joel Nanauka
#timizamalengoyako.