Usimchunguze na kumfuatilia mpenzi wako kama huna uwezo wa kumuacha

Kifurukutu

JF-Expert Member
Aug 29, 2013
4,502
6,403
kheri wakuu!

Nimeona niwashirikishe wajuvi wa mambo haya na mpate kujua kwamba kama huna uwezo wa kumwacha mpenzi wako uliye naye na unahitaji mapenzi yenu yashamiri nashauri kwamba ni bora ukae kimya usimfuatilie wala kumchunguza mpenzi wako.

Hii imemtokea demu mmoja mrembo sana aliyekufa na kuoza kwa penzi la rafiki yangu mkubwa sana tangu kitambo,
baada ya penzi lao kuingia doa ndipo mwanamke huyo akaamua kufunguka na kuniomba ushauri namna ya kurudisha penzi lililokua linakaribia kuzama

Kisa cha wapenzi hao kutofautiana ni pale mwanamke alipokua anamfuatilia jamaa hadi kugundua kuwa jamaa amepata mchepuko ambaye amemkubali sana zaidi yake. Huyu mwanamke njia kuu akaamua kujifanya yeye ndio mchepuko wa jamaa kwa kutumia namba mpya ya simu ili jamaa anaswe maana alikua amepata full detail za uyo mchepuko.

akasajili namba mpya na kuamua kumtafuta Jamaa na wakawasiliana vizuri tu, uyu demu akajifanya yete ndio mchepuko wa jamaa, hivyo jamaa akaingia kingi kirahisi tu na kuweka mipango yote hadharani. mwishowe wakapanga kuonana na ilipofija siku jamaa kwenda sehem wakutane ndio hapo akamkuta demu wake wa siku zote!

Na huo ndio ukawa mwisho wa penzi lao kwani jamaa alichukia saaaaana, hapokei simu, hajibu text nk. Hivyo huyu demu ndio leo kapata ahueni kidogo baada ya kuwapa ushauri na wamekutanishwa wameyazungumza, kidogo mapenzi yanaweza rejea.

Usimchunguze wala kumjaribu mpenzi wako kama huna namna na uwezo wa kuachana naye.
 
Mungu ameshamuonyesha yote bado anataka Malaika Gabriel amtokee kumwambia huyo mwanaume hamfai?
Amependa na amerizika kabisa nafsi yake haina uwezo kukubli watengane!
[HASHTAG]#mahabaniue[/HASHTAG]
 
Kwani huyu rafiki yako anapaka asali kwana kabla ya shughuli kuwa hakuna mwanaume mwingine atakaeweza?
Ahahaha eti asali

Hii kitu anaijua yeye maana kwa alichojiinea hakupaswa hata kumfuatafuata jamaa mwenyew ndio hamuelewi ata
 
Last week niliona similar case, kuna sista alisafiri kwenda mpaka morogoro kwa kazi tu ya kumchunguza jamaa yake aliyo yakuta huko alijuta, ila tena juzi jamaa ana niambia shem alimuomba msamaha wanaendelea na amekubali kuwa yeye ni njia kuu yule wa Moro ni mchepuko tu. Na kweli nimehakikisha bado wako pamoja.
Mpaka huwa nawaza hivi masista wa kibongo ukiwa una cheat ndio wana kupenda zaid au vipi!!?
 
Last week niliona similar case, kuna sista alisafiri kwenda mpaka morogoro kwa kazi tu ya kumchunguza jamaa yake aliyo yakuta huko alijuta, ila tena juzi jamaa ana niambia shem alimuomba msamaha wanaendelea na amekubali kuwa yeye ni njia kuu yule wa Moro ni mchepuko tu. Na kweli nimehakikisha bado wako pamoja.
Mpaka huwa nawaza hivi masista wa kibongo ukiwa una cheat ndio wana kupenda zaid au vipi!!?
Ukitaka kumlainisha mwambie utamuoa asijali kule ilikuwa ni makosa tu.
 
Back
Top Bottom