Diwani
JF-Expert Member
- Oct 25, 2014
- 2,825
- 3,021
Katika karne hii ya 21 kumekuwa na manung'uniko mengi sana kuhusu changamoto zinazoikumba ndoa na malalamiko ya watu ni juu ya nini kimetokea kwenye ndoa. Mbona zama hizi ndoa zinaanguka na kuna ongezeko kubwa la madai ya talaka na kudhoofika kwa taasisi hii?
Wengi wanazungumzia sababu zao kijamii, wanasahau ndoa kwa asili yake kwenye nyanja ya uchumi.
Zamani ndoa zilikuwa ni taasisi zilizoasisiwa na mfumo wa kijima; hivyo ndoa ilikuwa na lengo la kutengeneza Familia imara ambapo familia ndiyo ilikuwa chanzo cha na msingi wa nguvukazi katika maendeleo ya kiuchumi na uwepo (survival) ya jamii husika. Ebu fikiria, unajua kama kuna wakati jamii zetu zilikuwa zikiishi chini ya mfumo wa Kijima ambapo watu walihitajika wengi kwa ajili ya uzalishaji? Hii ina maana kuwa, bila familia kusingewezekana kuwepo vijiji, miji na hata majiji, na familia ilihitajika kwa ajili ya kujenga mfumo imara wa uzalishaji mali kwenye Kilimo, Ufugaji, biashara na hata usimamizi rasilimali (siasa).
Kwa kutambua jambo hili, ndoa ndiyo ilikuwa 'base" ya familia imara; ambapo mfumo mzima wa elimu na mafunzo wa wakati huo ulikuwa umelenga katika kujenga jamii yenye kuheshimu na kuthamini ndoa kwa sababu ndio msingi wa familia na bila familia kusingekuwapo na jamii yoyote iliyopo leo hii.
Kupitia jando, unyago, na kwa baadhi ya jamii kufunda; mfumo wa elimu ulizingatia ndoa na juzi mbali mbali za uzalishaji (practical skills); lengo likiwa kujenga na kuimarisha familia. Hivyo, Watoto wa kiume walifunzwa kuwa Wame/baba wa baadae, na watoto wa kike walifunzwa kuwa Wake/mama wa badae kupitia miundo hiyo ya elimu. Ndio mana waliishi chini ya muundo maalumu (defined order) ambapo baba alikuwa kiranja wa familia na aliongoza mfumo mzima wa uzalishaji.
SIKU HIZI; mambo yamekuwa tofauti, makundi ya uzalishaji si familia tena, bali Kampuni. Na hii ni baada ya kuanza kwa mfumo wa Kibepari ambapo, familia si msingi wa uzalishaji bali Mtaji. Hata hivyo, mifumo ya elimu ya zama hizi haziandai tena mtu kuwa 'Marital individual' yaani mtu anayethamini na kulinda ndoa kama taasisi nyeti ya kuanzisha familia kwa ajili ya 'community survival' kupitia uzalishaji.
Leo tunashuhudia kuwapo kwa watu, hususan wasomi ambao wanajituma zaidi kwenye ofisi zao za kazi kuliko kwenye familia zao, kwa sababu; mfumo wa uzalishaji wa zama hizi unategemea zaidi nguvukazi ya mtu binafsi (Individualism) kuliko familia kwa ujumla.
Kijamii, mfumo wa Kibepari umetengeneza watu wanaothamini zaidi nyezo walizonazo, na nafsi zao pekee na si kundi (nje ya kampuni, shirika, taasisi au kiwanda); hivyo basi hisia za ndoa, zimeanguka kwa sababu kubwa. Anguko la ndoa ndilo sababu ya anguko la familia.
Mwisho kabisa, kuna suala zima la mabadiliko ya majukumu ya kijinsia; kutokana na mabadiliko ya ki-majukumu kati ya Mwanamke na Mwanaume, ndoa imepoteza mantiki ya kuwa taasisi, bali kwa sasa ni mtindo wa maisha tu (life style).
Hivyo basi. Mfumo wa uchumi, ndio hujenga mfumo wa Kijamii. Ubepari ambao ndio mzizi wa Individualism umepunguza hitaji la ndoa kwenye uzalishaji, ila mtu binafsi tu.
Kila la heri.
Wengi wanazungumzia sababu zao kijamii, wanasahau ndoa kwa asili yake kwenye nyanja ya uchumi.
Zamani ndoa zilikuwa ni taasisi zilizoasisiwa na mfumo wa kijima; hivyo ndoa ilikuwa na lengo la kutengeneza Familia imara ambapo familia ndiyo ilikuwa chanzo cha na msingi wa nguvukazi katika maendeleo ya kiuchumi na uwepo (survival) ya jamii husika. Ebu fikiria, unajua kama kuna wakati jamii zetu zilikuwa zikiishi chini ya mfumo wa Kijima ambapo watu walihitajika wengi kwa ajili ya uzalishaji? Hii ina maana kuwa, bila familia kusingewezekana kuwepo vijiji, miji na hata majiji, na familia ilihitajika kwa ajili ya kujenga mfumo imara wa uzalishaji mali kwenye Kilimo, Ufugaji, biashara na hata usimamizi rasilimali (siasa).
Kwa kutambua jambo hili, ndoa ndiyo ilikuwa 'base" ya familia imara; ambapo mfumo mzima wa elimu na mafunzo wa wakati huo ulikuwa umelenga katika kujenga jamii yenye kuheshimu na kuthamini ndoa kwa sababu ndio msingi wa familia na bila familia kusingekuwapo na jamii yoyote iliyopo leo hii.
Kupitia jando, unyago, na kwa baadhi ya jamii kufunda; mfumo wa elimu ulizingatia ndoa na juzi mbali mbali za uzalishaji (practical skills); lengo likiwa kujenga na kuimarisha familia. Hivyo, Watoto wa kiume walifunzwa kuwa Wame/baba wa baadae, na watoto wa kike walifunzwa kuwa Wake/mama wa badae kupitia miundo hiyo ya elimu. Ndio mana waliishi chini ya muundo maalumu (defined order) ambapo baba alikuwa kiranja wa familia na aliongoza mfumo mzima wa uzalishaji.
SIKU HIZI; mambo yamekuwa tofauti, makundi ya uzalishaji si familia tena, bali Kampuni. Na hii ni baada ya kuanza kwa mfumo wa Kibepari ambapo, familia si msingi wa uzalishaji bali Mtaji. Hata hivyo, mifumo ya elimu ya zama hizi haziandai tena mtu kuwa 'Marital individual' yaani mtu anayethamini na kulinda ndoa kama taasisi nyeti ya kuanzisha familia kwa ajili ya 'community survival' kupitia uzalishaji.
Leo tunashuhudia kuwapo kwa watu, hususan wasomi ambao wanajituma zaidi kwenye ofisi zao za kazi kuliko kwenye familia zao, kwa sababu; mfumo wa uzalishaji wa zama hizi unategemea zaidi nguvukazi ya mtu binafsi (Individualism) kuliko familia kwa ujumla.
Kijamii, mfumo wa Kibepari umetengeneza watu wanaothamini zaidi nyezo walizonazo, na nafsi zao pekee na si kundi (nje ya kampuni, shirika, taasisi au kiwanda); hivyo basi hisia za ndoa, zimeanguka kwa sababu kubwa. Anguko la ndoa ndilo sababu ya anguko la familia.
Mwisho kabisa, kuna suala zima la mabadiliko ya majukumu ya kijinsia; kutokana na mabadiliko ya ki-majukumu kati ya Mwanamke na Mwanaume, ndoa imepoteza mantiki ya kuwa taasisi, bali kwa sasa ni mtindo wa maisha tu (life style).
Hivyo basi. Mfumo wa uchumi, ndio hujenga mfumo wa Kijamii. Ubepari ambao ndio mzizi wa Individualism umepunguza hitaji la ndoa kwenye uzalishaji, ila mtu binafsi tu.
Kila la heri.