Prince Naahjum_
Senior Member
- Jun 13, 2016
- 139
- 125
Katika maisha, unapoanza kufanikiwa katika kila nyanja, nakuhakikishia shetani atakuja na kila aina ya uharibifu, hasa kupitia kwa watu wako wa karibu. Ataleta majaribu kutoka pande zote, kila mtu atakuzungumzia vibaya, wapo watakao kukatisha tamaa, kukudhalilisha, kukufanya ujihisi mwenye hatia, kukufedhehesha na wengine watakuonea wivu.
Ni kawaida kujisikia vibaya kwa sababu wewe ni binadamu kama mimi, na kila binadamu ana hisia. Katika kipindi hiki unaweza hata kumsahau Mungu nakuhisi Mungu hayupo kwakuwa unaona kila unacho muomba hakuna majibu.
Sikia nikwambie, hilo ni suala la muda tu na kila mtu anapitia, mambo yote yatakuwa sawa. Ni kipindi kigumu sana kwakuwa katika kipindi hichi utasalitiwa, utaonewa, utahukumiwa, na kusingiziwa. Lakini Mungu atawafichua na kuwaondoa rafiki wabaya wanaokuzuia usisonge mbele.
Wakati umekata tamaa kabisa kwa hayo unayopitia ndipo Mungu atakapokushangaza kwa Ukuu wake, atakubariki kuliko vile ulivyomuomba. Atakufungulia milango ya baraka na neema kila kona, atawaaibisha adui zako. Hapo waliokudharau watatamani wawe hata vijakazi wako. Watakuamkia hata kama una umri mdogo kuliko wao.
Kazana kupambana, usikate tamaa Mungu yupo na wewe. Wewe ni mshindi , Pambana mpaka hatua ya mwisho huku ukiamini kuwa unaweza. Na unaweza kwasababu unajuhudi na una Mungu na Mungu ndio kila kitu katika maisha yetu!
The future is brighter than ever, Keep it up.












PRINCE NAAHJUM ALSINA