Usije nyumbani bila mke

Usije nyumbani bila mke

Jamani nina mawazo, wazazi wangu wametuma ujumbe kupitia mdogo wangu kwamba nisirudi nyumbani bila mke. Sio kwamba sitaki kuoa,uwezo upo na nia ipo,tatizo tangu nimetendwa sina maandalizi wala hamu ya kuanza mahusiano mapya.Ushauri wakondugu
Wazazi wako wanakupenda sana mkuu na wameshaona udhaifu wako kwa wanawake na hali ilivyo wasije wakakusa kwa sababu ya matendo yako ya bandika bandua.heshima ya mme ana mke ni ndoa acha ubazaz kaa njia ilio sahihi.Alitendwa samson sembuse wewe au unaogopa matumizi? ni ushauri tu kama vp wapelekee shoga uone kama watamkubali
 
Sio sana ila wanafanya ivi ili nioe kwan tayari rika langu wote wameoa na hata wadogo zangu wana watoto

Asante kwakulitambua hilo bila kusurutishwa!!

Umri haumngoji mtu' hautambui kama umetenda au umetendwa! Namimi nasema oa' achana na habari za nilitendwa!

Maana matokeo yakuchelewa kuoa ni kuwa na watoto yatima' ingawa unakuwa uu hai physically.
 
Jamani nina mawazo, wazazi wangu wametuma ujumbe kupitia mdogo wangu kwamba nisirudi nyumbani bila mke. Sio kwamba sitaki kuoa,uwezo upo na nia ipo,tatizo tangu nimetendwa sina maandalizi wala hamu ya kuanza mahusiano mapya.Ushauri wakondugu

weka picha usaidiwe
 
nipo tabora, nina miezi mitano sijarudi nyumbani maana nipo kazini, sitaki kuanzisha mahusiano mapya kwa sababu nilitendwa vibaya hata wao wanajua vizuri
Tuishi usitumie kosa la mmoja aliyekutenda kuwahukumu wanawake wote, pengine tatizo ni wewe Mwenyewe kwa kutunza hasira ndani ya nafsi yako ndo maana imekuwa ngumu kwako kubadilika.
 
Last edited by a moderator:
Ondokan na ukapera kwani aliyekutenda ndugu yako? acha hizo kijana oa ubadil maisha.
 
Wewe kama wewe unatakiwa uwe na maamuzi yako binafsi sio lazima kusikiliza kila wanachosema wazazi wako kumbuka na wao ni wanaadamu kama wewe pia, sio malaika
 
Back
Top Bottom