Ganda Mweri
JF-Expert Member
- Mar 8, 2018
- 293
- 855
Wasalaam ndugu zangu, nikikumbuka hiki kitu huwa ninajisemea kwamba, Acheni Mungu aitwe Mungu.
Nikiwa kijana mdogo miaka kadhaa iliyopita , Nyumbani kwetu kulikua na kisima ambacho wakazi wengi wa kijijini kwetu, walikua wakija kuchota maji kwa bei ya sh 100 kwa ndoo kubwa na 50 kwa ndoo ndogo.
Siku moja nikiwa hapo kisimani alitokea Dada mmoja aliyekuwa amekuja kuchota maji, lakini hakuwa na hela. Sasa Mimi nikawa ninamzuia kuchota maji huku nimekizingira kisima.
Sasa yule Dada kiutani utani akasema tena nitakusukuma humo, kipindi anasema hivyo akawa amenisukuma moja kwa moja ndani ya kisima. Hapo hapo yule Dada akaanza kupiga yowe.
Ninachokumbuka kipindi natua mle kwenye kisima nilitua kwenye tope moja kwa moja, na nikawa najaribu kutoka, maji yakanileta mpaka juu kisha nikazama tena, Ila kipindi narudi juu kwa Mara ya 3 nakumbuka kuna kitu kilinishika baada ya hapo nikajikuta hospital.
Kumbe yule Dada kipindi anapiga yowe , Kuna mwananchi alikuja akaingia ndani ya kisima na kunitoa huku nimeshapoteza fahamu na kunipeleka hospital ilikua ipo jirani tu na nyumbani kwetu.
Sasa kipindi nimetoka hospital, Mama akaniambia, sasa mwanangu ulikua unataka kujiua kwa sababu ya Grace?? Kumbe yule Dada aliwaambia, kwamba Mimi nimejirusha kisimani kwa sababu nimemtongoza akanikataa.
Mimi nikamwambia mama ukweli, kwamba yule binti ndiye aliyenisukuma , baada ya kumdai hela ya maji.
Wazazi wakataka kwenda kumshtaki, lakini majirani wakashauri tuyaache , kwa sababu wote tulikua vijana wadogo.
Mungu ni mkubwa hicho kitu ndio huwa nasema kila siku, Kama kuna MTU aliyewahi kuponea tundu la sindano kama Mimi naomba atushirikishe .
Nikiwa kijana mdogo miaka kadhaa iliyopita , Nyumbani kwetu kulikua na kisima ambacho wakazi wengi wa kijijini kwetu, walikua wakija kuchota maji kwa bei ya sh 100 kwa ndoo kubwa na 50 kwa ndoo ndogo.
Siku moja nikiwa hapo kisimani alitokea Dada mmoja aliyekuwa amekuja kuchota maji, lakini hakuwa na hela. Sasa Mimi nikawa ninamzuia kuchota maji huku nimekizingira kisima.
Sasa yule Dada kiutani utani akasema tena nitakusukuma humo, kipindi anasema hivyo akawa amenisukuma moja kwa moja ndani ya kisima. Hapo hapo yule Dada akaanza kupiga yowe.
Ninachokumbuka kipindi natua mle kwenye kisima nilitua kwenye tope moja kwa moja, na nikawa najaribu kutoka, maji yakanileta mpaka juu kisha nikazama tena, Ila kipindi narudi juu kwa Mara ya 3 nakumbuka kuna kitu kilinishika baada ya hapo nikajikuta hospital.
Kumbe yule Dada kipindi anapiga yowe , Kuna mwananchi alikuja akaingia ndani ya kisima na kunitoa huku nimeshapoteza fahamu na kunipeleka hospital ilikua ipo jirani tu na nyumbani kwetu.
Sasa kipindi nimetoka hospital, Mama akaniambia, sasa mwanangu ulikua unataka kujiua kwa sababu ya Grace?? Kumbe yule Dada aliwaambia, kwamba Mimi nimejirusha kisimani kwa sababu nimemtongoza akanikataa.
Mimi nikamwambia mama ukweli, kwamba yule binti ndiye aliyenisukuma , baada ya kumdai hela ya maji.
Wazazi wakataka kwenda kumshtaki, lakini majirani wakashauri tuyaache , kwa sababu wote tulikua vijana wadogo.
Mungu ni mkubwa hicho kitu ndio huwa nasema kila siku, Kama kuna MTU aliyewahi kuponea tundu la sindano kama Mimi naomba atushirikishe .