Ushindi wa Kikwete wazidi kutia mashaka

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233
• Wataalamu wa Ulaya nao wafichua mianya ya wizi wa kura
• Wakiri Chadema iliungwa mkono, Dk Slaa aliepusha vurugu


Uhalali wa Rais Jakaya Kikwete kuwa madarakani unazidi kutia shaka baada ya ripoti ya mwisho ya waangalizi wa Umoja wa Ulaya (EU) kutoa maelezo yanayothibitisha kuwapo kwa mwanya mkubwa wa kura kuibiwa na matokeo kubadilishwa katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana.

Wakati rais Jakaya Kikwete na chama chake walidai kura zisingeibiwa kwa sababu kila chama huruhusiwa kuweka wakala wake, ripoti hiyo ya ujumbe wa Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka Jumuiya ya Ulaya (EU) inawaumbua, baada ya kueleza waziwazi bila kumung'unya maneno kwamba mawakala wa vyama vya siasa na waangalizi wa uchaguzi hawakuruhusiwa kushuhudia ujumlishaji wa matokeo ya uchaguzi wa urais uliokuwa ukifanywa na Tume ya Uchaguzi (NEC).

Ujumbe wa waangalizi hao wa EU ukiongozwa na Mbunge wa Bunge la Ulaya, Daid Martin, ulikuwepo nchini tangu September 29 hadi Novemba 28 mwaka jana na ulisambaza waangalizi wake 103 katika mikoa yote 26 ya Bara na Visiwani.

Katika ripoti hiyo ambayo Tanzania Daima Jumapili inayo nakala yake, wataalamu hao
wameeleza kuwa matokeo ya kura za urais mwishowe yalijumlishwa na viongozi wa Tume ya Uchaguzi, NEC wakiwa peke yao bila ya kushuhudiwa na mawakala wa vyama vya siasa, utaratibu ambao kwa mtazamo wa kawaida, ulitoa mwanya mkubwa kwa kura kuibiwa au matokeo halali kubadilishwa, huku ukiwepo uwezekano wa Kikwete kupendelewa kwa sababu ya kile kinachoifajhamika kuwa ndiye aliyewateua kuiongoza Tume hiyo kutokana na mamlaka yake ya uteuzi akiwa kama rais………………..

Habari zaidi katika Tanzania Daima Jumapili

My take:

Hili ni kosa kubwa walilofanya wapinzani kutosisitiza kuwepo kwa mawakala wao kushuhudia majumuisho hayo ya kura uliofanywa na NEC ingawa huenda sheria/kanuni hairuhusu kuwepo kwa mawakala wa vyama.

Lakini kubwa zaidi kwa nini EU katika taarifa yao wasiseme tu kwamba "ingawa uchaguzi ulikuwa huru, lakini matokeo hayakuwa ya haki?"
 
Mkuu Zak nashukuru umeniwahi.

Asubuhi nilikuwa natazama TBC1 wakipitia magazeti. Msomaji alipokuwa anasoma gazeti fulani nikamwona amechomoa Tanzania Daima chini ya hilo gazeti alilokuwa anasoma akaweka pembeni. Kwa hiyo hakusoma vichwa vya habari vya Tanzania Daima. Nikawa curious nikaingia kwenye tovuti ya Tz Daima lakini nikakuta hawajapost habari za gazeti la leo. Nimetuma gazeti bahati nzuri ndo limeingia na ninaona hiyo habari.

Kwa nini TBC1 hawakuisoma?
 
Hivi lini' Wadanganyika' mtaachana na label hiyo? Lini mtakuja kuamini kwamba alichofanya Judge Makame ni kile kile alichokifanya Samuel Kivuitu kule Kenya mwaka 2007, au yule mwingine wa Ivory Coast mwaka jana? Afrika ni moja, na mambo ya viongozi weao ni mamoja tu -- hiyo ndiyo African Union (AU).

Waarabau hao wa kaskazini wamo wamo tu katika AU, na ndo maana sasa wameamua kufanya vitu vyao.
 
Ukweli una tabia ya kujiweka hadharani wazi wazi. Slowly sasa inajulikana ni jinsi gani siasa za kuchagua viongozi TZ zinavyochezewa na wajanja wachache ndani ya system...the issue is for how long????
 
Uchaguzi kwa maana ya upigaji kura ulikuwa huru kwa hakukuwa na matukio ya watu kulazimishwa kumchagua kiongozi wasiyemtaka. Ila uchaguzi haukuwa wa haki kwani baadhi ya watu majina yao hayakuonekana na hawakusaidiwa na tume. Ila matokeo si ndo Dr Slaa amekua akiwaambia siku zote kuwa yalichakachuliwa watu wakawa wanabeza...

Katika mazingira ya kawaida haiwezekani watu mjifungie chumbani kujumlisha matokeo peke yenu. Ikumbukwe kuwa Kiravu alishapania kuiba kura muda mrefu na kauli zake kuelekea uchaguzi zilionyesha dhamira ya wizi.
 
Uwezekano mkubwa upo wa kuibiwa kula lakini sisi wapiga kura na waangalizi walilala sana na kukazania kura za wabunge wakasahau za rais ndipo Makame kafanya vitu alivyoagizwa na Msheshiwa wa sasa sijui anaitwa Rais
 
dah!
sioni hata sababu za kulazmisha kuingia ikulu,hebu angalia masuala mazito yanavowashnda
 
Mkuu Zak nashukuru umeniwahi.

Asubuhi nilikuwa natazama TBC1 wakipitia magazeti. Msomaji alipokuwa anasoma gazeti fulani nikamwona amechomoa Tanzania Daima chini ya hilo gazeti alilokuwa anasoma akaweka pembeni. Kwa hiyo hakusoma vichwa vya habari vya Tanzania Daima. Nikawa curious nikaingia kwenye tovuti ya Tz Daima lakini nikakuta hawajapost habari za gazeti la leo. Nimetuma gazeti bahati nzuri ndo limeingia na ninaona hiyo habari.

Kwa nini TBC1 hawakuisoma?

Mkuu bado unaishangaa na kuangalia TBC1, nimeshawaandikia mara nyingi uchakachuaji wao wa habari za magazeti, hawajawahai kusoma hata message yangu moja kwenye kipindi chao cha Jambo, nimeacha kuangalia TBC1
 
Mungu anawaumbua ufisadi wao walioufanya kuwadhulumu Watanzania haki yao ya kumchagua mtu wanayemtaka na Makame kumchagua mtu Mwengine tena Fisadi. Mungu atakuangamiza wewe Makame kwa haya matatizo tunayoyapata kwa Ufisadi wako
 
Mkuu bado unaishangaa na kuangalia TBC1, nimeshawaandikia mara nyingi uchakachuaji wao wa habari za magazeti, hawajawahai kusoma hata message yangu moja kwenye kipindi chao cha Jambo, nimeacha kuangalia TBC1

Yes, I did as you did and results are as yours.
Labda wanaogopa ku- Tidoliwa kama Tido Mhando the former tbc mkurugenzi
 
Hivi lini' Wadanganyika' mtaachana na label hiyo? Lini mtakuja kuamini kwamba alichofanya Judge Makame ni kile kile alichokifanya Samuel Kivuitu kule Kenya mwaka 2007, au yule mwingine wa Ivory Coast mwaka jana? Afrika ni moja, na mambo ya viongozi weao ni mamoja tu -- hiyo ndiyo African Union (AU).

Waarabau hao wa kaskazini wamo wamo tu katika AU, na ndo maana sasa wameamua kufanya vitu vyao.

wa ivory coast hakuchakachua..yeye alimtangaza Alassane mshindi kwa 54% lakini Gbagbo alikataa na badili yake akatumia constituional council kufuta matokeo ya tume(yaliyompa ushindi Alassane na kumtangaza yeye Gbagbo kuwa mshindi):wink2:
 
Mkuu bado unaishangaa na kuangalia TBC1, nimeshawaandikia mara nyingi uchakachuaji wao wa habari za magazeti, hawajawahai kusoma hata message yangu moja kwenye kipindi chao cha Jambo, nimeacha kuangalia TBC1

Nilichelewa kuamka mkuu nikawa desparate kutafuta magazeti yameandika nini nikakuta TBC wanayasoma. Sasa hawakujua kwamba kama sijajua Mwananchi na TZ Daima wameandika nini hayo mengine wanapoteza airtime yao bute. Wangechakachua gazeti lingine wala nisingeshtuka
 
Yes, I did as you did and results are as yours.
Labda wanaogopa ku- Tidoliwa kama Tido Mhando the former tbc mkurugenzi

Kuna wakati wanachakachua meseji uliyowatumia wanaigeuza kuwa na ujumbe wanaoutaka wao. Ni kweli nilishaachana nao, ndo maana tunasubiri kwa hamu television ya Chadema
 
wamemtimua tido , mwanamapinduzi kamili sasa unafikiri nani tenayupo huko TBC1?
WALIOPOWOTE WAMEPANDIKIZWA,
WANAMUMIKIA KAFIRI.
 
Ni kweli utawajua tu kwa matendo yao wameshaanza kujitokeza na kuanza kusema kama mnavyoweza kumwona huyu mmoja wao amekuja na malalamiko "Uchaguzi umekwisha na Vyombo vya Uongozi -Bunge, Serikali na Mahakama kusimikwa na kufanya kazi. Kulikoni unaruhusu baadhi ya wachangiaji kumwita mgombea alieshindwa Rais Wao? Huoni kama huu ni uasi na chanzo cha uchochezi. Haya ni matumizi mabaya ya mitandao. Uhuru wa kujieleza usipitilize mipaka na Moderator uone unajukumu- Moral Resposibility kwa hili. Najua kuna waliokwenye mlengo huo hawatakubaliana na haya." said by bahari55

Hivyo bado wanahaha sana, nchi hiyo haitawaliki kwa mabavu.
 
Back
Top Bottom