Ushawahi kuchukia mtu bila sababu

Ushawahi kuchukia mtu bila sababu

kateli

Member
Joined
Feb 3, 2014
Posts
70
Reaction score
28
Unaweza kujikuta kuna mtu unamchukia bila sababu na yeye pia anakuchukia.Yaani mnachukiana bila sababu na hamko compatible kabisa ila mnakutana kila wakat.Hamuongei mengi labda ya lazima au endapo kuna mtu kati.

Hivi huwa ni nini?
 
Na hata kwa ndugu wa tumbo moja inatokea sana, na hata kwa wazazi inatokea kumpenda zaidi mtoto fulani kati ya watoto/wanawe wake wote
 
Inatokeaga tu, mi pia kuna mtu namchukia hapa wakati hata simjui teh huu si uchizi
 
Hata (kutokuwa compatible, wivu, attitude ya mtu, appearance, unsocial behaviour, damu ya kunguni..) nazo pia ni sababu... (kwahio sababu zipo)
 
Unaweza kujikuta kuna mtu unamchukia bila sababu na yeye pia anakuchukia.Yaani mnachukiana bila sababu na hamko compatible kabisa ila mnakutana kila wakat.Hamuongei mengi labda ya lazima au endapo kuna mtu kati.

Hivi huwa ni nini?

Noooo!
Sababu ni lazima iwepo! Sema inawezekana sababu isiwe ya msingi!
 
^^
Kuna elimu ya namba hutaja mambo haya, mf 1 na 9 hazipatani
^^
 
kama mimi ninavyomchukia Lukuvi na nape nnnauye just bila sababu teh teh
 
Mimi mwenzenu nachukia rangi ya kijani na njano sijui kwanini.
 
Inatokea na sababu inakuwepo ila inaweza isiwe ya msingi mpaka uone haya hata kuisema hadharani kama ukiulizwa sababu.
 
Tatizo ni pesa tu... hakuna la ziada hapo!

mnunie bosi wako uone!
 
Nilipokua mdogo nilikua nikiangalia filamu za bongo najikuta nawachukia sana wale wanao act wachawi, mama wakambo, makatili, na watu wabaya
 
Moyo ndicho kiungo pekee mungu amekipa kazi ya kupenda na kuchukia, hivyo moyo ndio chombo pekee kinachohifadhi upendo na chuki....kuna aina mbalimbali za upendo na chuki...... Kumpenda mtu na kumchukia mtu hautokei tu bila sababu..kuna sababu ambazo mtu humfanya mtu kumchukia au kumpenda mtu fulani....... Unaweza kumchkia mtu kwa vile huyo mtu amefanana sura na mtu ambae alishawahi kukufanyia ubaya basi unaweza kumchukia mtu huyo...hiyo ni moja ya sababu.

Vilevile mungu amewaumba wanadamu tofauti na mfanano ndani ya mioyo yao.....unaweza ukakutana na mtu kwa mara ya kwanza wote mkajikuta mnapendana hapo inaonesha mfanano wa mioyo yenu pia unaweza ukakutana na mtu kwa mara ya kwanza wote mkajikuta kuna uzito flani ndani ya moyo wa kila mmoja juu ya mwanzake hapo kunautofauti mkubwa wa mioyo yenu hivyo mnajikuta mnachukiana tu bila sababu.

Vilevile namna mtu anavyojiweka na anavyochukuliwa na mwenzake hufanya kujenga chuki ndani ya moyo mfano: mtu kupenda usharobaro uliopitiliza,nyodo, dharau na kujiona,ukali vyote hivyo hufanya moyo kumchukia mtu.
 
Ishanitokea wakati na mimba halfu nikazaa mtoto kuna vitu wamefanana huwaga nacheka nikikumbuka na kwanini nilimchukia sielewi.
 
Back
Top Bottom