Ushauri wenu Wadau

Ushauri wenu Wadau

Tulio jr

Member
Joined
Feb 6, 2013
Posts
6
Reaction score
0
Mimi ni mkazi wa Kigamboni,km wiki 3 zilizopita kulitokea la uvunjaji nyumbani kwangu,na kuibiwa baadhi ya vitu,nilitoa taarifa kituo cha polisi Kigamboni.Kwa gharama zangu nilikodi gari kwa ajili ya kufanya msako kuwapata wahalifu wa tukio hilo.Tulibahatika kuwakamata watuhumiwa watatu(3)kati ya saba(7)siku hiyo, akiwemo mtoto anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 12-14 na yeye ndo 'master plan' sababu ndiye anayejichanganya na watoto kusoma mazingira sehemu wanayotaka kwenda kufanya tukio na ndiye anayetumika kupenya madirishani kabla ya kufungua milango.Huyu mtoto ndiye aliyetoa ushirikiano wa kupatikana hao watuhumiwa wengine,Siku ambayo tulipaswa kwenda mahakamani niliambiwa huyo mtoto yuko nje kwa dhamana pamoja na mtuhumiwa mwingine,na hawajahudhuria mahakamani kwa mara ya pili,na yeye naweza sema ndiye kichwa cha hii kesi(mtoto) sababu hawa wengine walikana kuhusika na tukio hili pale kituo cha polisi licha ya kutajwa na huyu mtoto,anayepandishwa mahakamani ni mtuhumiwa mmoja tu.Nilitaka kujua hapa kweli kuna kesi? Na kama ndiyo nini kifanyike? Naomba ushauri wenu wadau.Mana hawa vijana ni wasumbufu hapa kwenye kitongoji chetu na wana kawaida ya kulipiza kisasi wakirudi uraiani.
 
Pole sana mkuu!
Lkn kuna wakati unatakiwa kujua kuwa kuna baadhi ya mapolisi wanakula na majambaz!! Kilichotakiwa sio ni siku hi yo hiyo uliyokamata mbaya wako na kakubali kuwa ni mmoja wao, kwann polis wasimbane mpaka akaonyeshe walipoficha vitu vyako?za kuambiwa changanya na zako!!

Kwanza siku nyngine usiendo kituo cha kitongojin kwenu vuka mipaka na iman hao polisi watakuwa hawawajui/kuwafahamu vbaka wenu...


ni mawazo yangu tu!!
 
Kazi unayo.
Inabidi uwe na ushahidi/mashahidi.
Nenda kwa mjumbe, serikali za mitaa.
Police wakamkamate tena, wamtie ndani.
Je huyo mtoto anaishi na nani, na wazazi? anasoma?
Maana huyo ni mtoto, inawezekana kesi ikasitishwa mpaka afike miaka 18.
Akifika miaka 18 ndio unaenda tena mahakamani kukumbusha ama kufufua kesi.
Na pengine kesi ikaffutwa, kama mtoto alilaghaiwa je?

Ukitaka mkamate huyo mtoto, mbane sana na record video bila yeye mwenyewe kujua.
ili utumie mahakamani hiyo video kama ushahidi.
 
Back
Top Bottom