minzakunza
Senior Member
- Oct 15, 2015
- 193
- 444
Habari wapendwa, nimekuja humu maalum kwa ajili ya kupata ushauri wenu ingawa sio mgeni kivile, mimi ni mdada mwenye umri wa miaka 30 ni muajiriwa katika shirika moja la serikali hapa jijini Mwanza, nimewahi kuwa kwenye mahusiano mara moja ambayo mahusioano hayo yalikoma mwaka 2010 kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wetu mimi na mwenzangu tangia hapo sikuwahi kumpenda mtu yeyote kiufupi ni kama moyo wangu ulipatwa na ganzi kuhusu mapenzi mpaka hivi majuzi miezi kama miwili nilipotokea kumpenda kijana mmoja ambae alihamishiwa hapa kazini kwetu si kijana sana kwani amenizidi miaka kama 7 hivi na kikazi ni Boss wangu kwani naripoti kwake, mwanzo sikuwa nimefikiria kabisa kama ningempenda mpaka yeye mwenyewe alivyoonyesha interest za kuvutiwa na mimi moyoni nikahisi hata mimi amenivutia,siku moja akaniomba nimsindikize kupata chakula ilikuwa jioni kama sa 12 kwa sababu mchana alikuwa hajala ndipo akaanza kunieleza kwamba amenipenda sikumpa jibu la moja kwa moja kuwa hata mi nimempenda ingawa sikukataa pia cha kushangaza akaomba tukalale pamoja siku hiyohiyo kiukweli sikuweza kumkubalia na hii ni kutokana tumefahamiana nadhani ilikuwa ni wiki 2, baada ya hapo ilifuatiwa kama mara mbili kwa siku tofauti kumbushia swala la kwenda kulala kwake na mimi bado sikukubali nikiamini kwamba tutakaa tuongee kwa sababu sijui maisha yake ya mapenzi na hata yeye hajui maisha yangu ya mapenzi ingawa alinambia alishawahi kuoa ila waliachana na mkewe miaka 5 iliyopita na ana mtoto mmoja, baada ya hapo kama kweli anamaanisha tukapime then vingine viendelee lakini kabla hatujafika huko kwa wiki mbili sasa namuona amebadilika mawasiliano hakuna tena hata nikijitahidi nimtumie sms hajibu yaani kiufupi amebadilika mwanzo ilikuwa tukitoka kazini tunaweza tukaongozana tukaa sehemu kuongea mawili matatu sasa hamna tena anaondoka tu haniagi au anaweza asije asinambie yuko wapi tofauti na mwanzo hata akichelewa tu ananiambia kusema ukweli naumia sana moyo ni kipindi kifupi lakini nahisi sijawahi kupenda hivi yaani sielewi nifanye nini nimekuwa kama mgonjwa siwezi kula wa kulala ni wiki mbili tu sasa tangu aanze vituko hivyo lkn nimepungua uzito kwa kiwango kikubwa muda wote nimekuwa mnyonge maswali ya kama naumwa yamekuwa kawaida sana naona siku zinavyoendelea nitashindwa hata kufanya kazi naomba mnisaidie nifanyaje kuondokana na kadhia hii kiukweli hali ni mbaya sana kwangu yaani muda wote usiku na mchana yupo kwenye mind yangu ninaweza kupata usingizi masaa 2 tu usiku nikishtuka usingizi hauji tena mpaka asubui msaada wenu pls maana huko ninakoelekea nahisi nitachanganyikiwa kabisa, ninaweza nikachukua simu hivi nasema nampigia nimuulize lakini najikuta natetemeka mwili wote jasho linanitoka nashindwa kabisa