GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,548
- 108,882
Hilo Kosa naliona linajirudia mara kwa mara na pengine ama Yeye mwenyewe ( Mheshimiwa Rais ) au Wasaidizi wake ( Washauri ) wanadhani ni jambo jema ambalo litawaisidia ' Kisiasa ' zaidi ila kwa mtazamo wa ' Kiuwerevu ' zaidi halileti maana na sana sana linadhalilisha tu ' hadhi ' ya Urais na kuonekana ni ya Kiswahili Kiswahili sana.
Hoja yangu kama GENTAMYCINE ni ndogo sana kwamba siyo kila ' matukio ' lazima Mheshimiwa Rais wa JMT awepo. Binafsi yangu kuna ' matukio ' ambayo huwa hayana sana ' hadhi ' ya Rais kuwepo au kuhudhuria au kuyazindua lakini huwa namwona Mheshimiwa Rais Dr. Magufuli akihudhuria.
Kwa maoni yangu naomba Wasaidizi wa Rais walibadili hili na badala yake Mheshimiwa Rais awe anatokea au anaonekana tu katika yale mambo ya msingi, nyeti na muhimu ya Kitaifa na haya ' matukio ' mengine amwachie Makamu wake au Waziri Mkuu.
Yawezekana kabisa kwamba sasa ameshazoeleka na kuonekana ni wa kawaida kwa Wananchi hatya wengine kumuona ni wa kawaida sana au ni mwenzao tu wa ' Kijiweni ' hivyo kupelekea kushusha heshima / hadhi yake katika Jamii.
Uzinduzi wa:
Sifurahishwi na Kitendo cha Mheshimiwa Rais JPM kuhudhuria kila aina ya matukio kwani haitendei hadhi hadhi ya ' Presidency ' ambayo kokote pale duniani inatakiwa iheshimike na ikibidi hata ' Kuogopwa ' vile vile kwakuwa Yeye ndiyo wa mwisho Kimaamuzi.
Kuna nchi ambazo siku ukisikia tu Rais wao anazungumza au anatembelea mahala fulani jua ya kwamba kuna ' Kitu ' cha muhimu sana na Wananchi wote hukaa tayari kumsikiliza na hata kile ambacho ama atakisema au atakifanya kitapokelewa kwa umuhimu wake mkubwa tofauti na sasa nchini ambapo Mheshimiwa Rais ameshaonekana ni Mtu wa kawaida sana ndani ya macho na fikra za Watanzania wengi.
Nimeumbwa kusema ukweli, kutoa maono yangu na kamwe kutokuwa ' Mnafiki ' hivyo kama kuna ambaye nitamkwaza katika hili nililoliandika hapa ' mnisamehe ' ila nimelipima hili kwa marefu na mapana yake na kuona kuwa kuna ' tatizo ' mahala hivyo kama Mtu mwenye mapenzi mema na Rais wangu wa JMT Ndugu Dr. John Pombe Joseph Magufuli nimeona nilisemee na nitashukuru kama ' Wahusika ' watalifanyia ' tathmini ' kisha ushauri wangu ufanyiwe Kazi.
Nimemaliza yangu na moyoni na GENTAMYCINE nawatakieni nyote Wiki njema inayoanza leo.
Nawasilisha.
Hoja yangu kama GENTAMYCINE ni ndogo sana kwamba siyo kila ' matukio ' lazima Mheshimiwa Rais wa JMT awepo. Binafsi yangu kuna ' matukio ' ambayo huwa hayana sana ' hadhi ' ya Rais kuwepo au kuhudhuria au kuyazindua lakini huwa namwona Mheshimiwa Rais Dr. Magufuli akihudhuria.
Kwa maoni yangu naomba Wasaidizi wa Rais walibadili hili na badala yake Mheshimiwa Rais awe anatokea au anaonekana tu katika yale mambo ya msingi, nyeti na muhimu ya Kitaifa na haya ' matukio ' mengine amwachie Makamu wake au Waziri Mkuu.
Yawezekana kabisa kwamba sasa ameshazoeleka na kuonekana ni wa kawaida kwa Wananchi hatya wengine kumuona ni wa kawaida sana au ni mwenzao tu wa ' Kijiweni ' hivyo kupelekea kushusha heshima / hadhi yake katika Jamii.
Uzinduzi wa:
- Kiwanda cha Kibiriti na Njiti zake anakuwepo
- Uzinduzi wa dawa ya mbu na masalia yake anakuwepo
- Uzinduzi wa Tairi mpya za magari na zenye Pancha anakuwepo
- Uzinduzi wa Uwekaji Viraka na mchanga barabarani anakuwepo
- Uzinduzi wa Visima vya Maji yasiyo masafi anakuwepo
- Uzinduzi wa Watu kunywa Maziwa hata ya Popo anakuwepo
- Uzinduzi wa Watu kujua kunawa mikono wakitoka msalani anakuwepo
Sifurahishwi na Kitendo cha Mheshimiwa Rais JPM kuhudhuria kila aina ya matukio kwani haitendei hadhi hadhi ya ' Presidency ' ambayo kokote pale duniani inatakiwa iheshimike na ikibidi hata ' Kuogopwa ' vile vile kwakuwa Yeye ndiyo wa mwisho Kimaamuzi.
Kuna nchi ambazo siku ukisikia tu Rais wao anazungumza au anatembelea mahala fulani jua ya kwamba kuna ' Kitu ' cha muhimu sana na Wananchi wote hukaa tayari kumsikiliza na hata kile ambacho ama atakisema au atakifanya kitapokelewa kwa umuhimu wake mkubwa tofauti na sasa nchini ambapo Mheshimiwa Rais ameshaonekana ni Mtu wa kawaida sana ndani ya macho na fikra za Watanzania wengi.
Nimeumbwa kusema ukweli, kutoa maono yangu na kamwe kutokuwa ' Mnafiki ' hivyo kama kuna ambaye nitamkwaza katika hili nililoliandika hapa ' mnisamehe ' ila nimelipima hili kwa marefu na mapana yake na kuona kuwa kuna ' tatizo ' mahala hivyo kama Mtu mwenye mapenzi mema na Rais wangu wa JMT Ndugu Dr. John Pombe Joseph Magufuli nimeona nilisemee na nitashukuru kama ' Wahusika ' watalifanyia ' tathmini ' kisha ushauri wangu ufanyiwe Kazi.
Nimemaliza yangu na moyoni na GENTAMYCINE nawatakieni nyote Wiki njema inayoanza leo.
Nawasilisha.