Ushauri wangu kwa vijana 854 waliofukuzwa jeshini na ombi langu kwa Rais Samia Suluhu na Mkuu wa Majeshi

Gwappo Mwakatobe

JF-Expert Member
Nov 22, 2019
1,494
1,874
Nawashauri vijana wote 854 waandike barua rasmi kwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu Samia Suluhu Hassan na nyingine kwa Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo; waombe msamaha na kujutia makosa yao au uasi wao. Waahidi kuwa raia wema na ikiwapendeza Rais na Mkuu wa Majeshi wawasamehe na kuwarudisha jeshini.

Kwa upande mwingine, na kwa heshima na unyenyekevu mkubwa; nitoe ombi rasmi kwa Rais wangu na dada yangu Samia Suluhu Hassan pamoja na Mkuu wa Majeshi na kaka yangu Venance Mabeyo, wawaone vijana hao kuwa ni watoto wao. Wamekosea sana kwa taifa na kwao wenyewe, lakini Rais na Mkuu wa Majeshi nawajua sana kuwa pia ni wazazi na walezi wenye huruma, wapole na waungwana kwa watoto wanapotubu makosa yao na kujirudi.

Aidha, huku mitaani kumejaa vijana wengi wasio na ajira na wamechanganyikiwa, hawajui la kufanya, hawana mitaji, wengine hawana hata ndugu wa kuwasaidia na wamekosa ubunifu. Wamekata tamaa!

Tusiwaongeze wengine waliokata tamaa mitaani, tena wanaojua kutumia silaha za moto. Vijana waliokata tamaa wako tayari kufanya lolote maana hawana cha kupoteza zaidi ya kutuachia uchungu na madhara pindi wafanyapo uhalifu.

Wengine husema ni mabomu yanayotembea. Naomba sana, tena sana; tuwasamehe, tuwafunde na kuwapatia ajira ili wasiwe mabomu yanayotembea yanayoweza kulipuka wakati wowote!
 
Huo utaratibu wa kuomba msamaha kwa maandishi unatambulika/unakubalika kwa taratibu za kijeshi? Na kwani wakirudi mtaani, tatizo liko wapi? Mbona unawatisha hao vijana na wakati wana fani zao mbalimbali! Mfano hiyo fani ya ufundi ujenzi, nk.

Kwani wasiporudishwa watakufa na njaa mtaani? Mimi nawashauri hao vijana warudi tu mtaani na waendeleze maisha yao. Huwezi kujua Mungu amewaandalia nini kwa siku za usoni. Muhimu wachague kuishi maisha ya kawaida, kama sisi raia wengine.
 
Nawashauri vijana wote 854 waandike barua rasmi kwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu Samia Suluhu Hassan na nyingine kwa Mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo; waombe msamaha na kujutia makosa yao au uasi wao. Waahidi kuwa raia wema na ikiwapendeza Rais na Mkuu wa Majeshi wawasamehe na kuwarudisha jeshini...
Kongole! Maneno yako mubashara
 
Hivi tumeshawahi kujiuuliza kwanini kila siku zinavyoenda ukosefu wa Ajira ni tatizo lililo mbele yetu?

Tunamjua kuwa haya ni matokeo ya mitaala mibovu tuliyonayo?

Suluhu yake ni ipi? Au tunaweka measures gani kuzuga kuendelea kutokea kwa tatizo hili??
Usikute kuna watu wananufaika na huu ubov
 
Vijana hawajafukuzwa jeshini bali serikali imeshindwa kuwaajiri. Mapunguani peke yake ndiyo yamedanganywa kuwa vijana wamefukuzwa jeshini kwa kuasi. Muwe mnapenda kutafuta habari na kufanya tafiti, tofauti na hapo tutaendelea kuwa na kizazi mbumbumbu.
 
Walishaonywa mpaka na mkuu wa jeshi la kujenga taifa hawakusikia tatizo vijana wa jkt miongoni no wajeuri Sana tunawaona Sana wakiwa mtaani acha waungane na mgambo mitaani mbona mgambo wanajua kulenga na sio majambazi.
 
Back
Top Bottom