Nimefikiri Sana kuhusu nanna bora ya kuongeza ufanisi wa utoaji huduma muhimu kwa wananchi kupitia mashirika mbalimbali ya Serikali. Lengo hasa na kuondoa ukiritimba unaonekana katika mashirika hayo.
Leo niongelee kuhusu huduma ya umeme, maji, na hifadhi ya jamii
1. UMEME
Tumeshuhudia juhudi za Serikali kutengeneza bwawa la kuzalisha umeme la Stigllers Geoge kwa lengo lla kuongeza kiwango Cha uzalushaji wa umeme nchini jambo litakalosaidia kupunguza Bei ya umeme hivyo kuchochea uanzishwaji wa viwanda nchini, pia Serikali imekuwa ikisimamia uzalishaji wa umeme katika mabwawa mbalimbali Kama vile Kidatu, Mtera, Nyumba ya Mungu nk
Ni Jambo jema Sana Ila mfumo uliopo wa uzalishaji umeme na usambazi wake unaruhusu ukiritimba unaoondoa ufanisi wa upatikanaji wa umeme nchini, Shirika la TANESCO ndilo pekee linalohusika kusimamia uzalishaji na usambazaji wa umeme kwa walaji, hii kwa mtazamo wangu sio sawa, ushauri wangu ni kuwa TANESCO ihusike katika uzalishaji tu na swala la usambazaji yawepo mashirika mengine ambayo yatahusika katika kutafuta wateja, kuongeza miundominu rahisi, kuwawekea umeme na kutoza bill kulingana na huduma waliyotoa.
Jambo Hilo litachochea ushindani ambao kwa nanna Moja au nyingine utaongeza ufanisi, utaongeza ajira na kupunguza ukiritimba Sana, Serikali ichukue Kodi na kuwekaa vigezo katika usajili wa mashirika hayo, ninaamini utafiti muhimu ukifanyika hapa Serikali itapunguza majukumu na fedha zinazotumika Sasa katika usambazaji wa umeme zingeelekezwa katika kuboresha elimu,afya na huduma nyingine muhimu kwa wananchi.
2. MAJI
Mfumo uliopo Sasa umegawanyika katika sehemu mbili kwa mtazamo wangu, Moja Serikali kuu inahusika katika kutafuta vyanzo vya maji na kuweka miundo mbinu ya uzalishaji wa maji katika Kila mkoa na hata usambazaji wa miundombinu hiyo katika maeneo mbalimbali.
Pili Serikali inakabidhi kazi ya kusimamia miundominu hiyo ambayo hukabidhiwa kwa mamlaka za.maji Mjini na za vijijini kwa mfabo, Mwanza Kuna Mwuwasa na Ruwasa, Iringa Kuna Iruwasa na Ruwasa Arusha Kuna Aruwasa na Ruwasa nk. Mfumo huu una kasoro kidogo kwa kuwa una ukiritimba kaatika upatikanaji wa maji kwa wananchi. Ushauri wangu ni kutokuwa na mamlaka badala yake Serikali ihusike katika uzalishaji wa maji na kuyauza maji hayo kwa mashirika ya usambazaji wa huduma za maji kwa wananchi ambayo yanaweza kuwa zaidi ya Moja
Mashirika haya yatakuwa na wajibu wa kutunza miundombinu na kuongeza mingine itakayowezesha upatikanaji wa maji kwa wananchi, Jambo Hilo litaongeza ufanisi na kuondoa ukiritimba uliopo, lakini pia litaongeza ajira kwa wahitimu wa ufundi katika njanja za maji. Lakini pia Kuna kasoro kubwa kwa jumuiya za maji vijijini ambazo Sasa zinasimamiwa na Ruwasa, hizi jumuiya hazina wataalamu wa kusimamia huduma za maji.
Jambo Hilo linazorotesha juhudi za Serikali na kuongeza migogoro katika maeneo husika, Naamini mashika hayo yatakuwa na wataalamu na mwananchi atabaki kuchagua Shirika lenye ufanisi katika utoaji wa huduma, nashauri utafiti ufanyike ili kufanya mapinduzi makubwa katika upatikanaji wa huduma hii muhimu.
3. HUDUMA ZA UHIFADHI WA JAMII
Hapa nashauri Serikali irudie mfumo uliokuwepo awali wa kufufua mashirika ya NSSF, NPF, LSSF nk mfumo wa Sasa umemfanya mfanyakazi kutokuwa na Uhuru wa kuchagua Shirika linalomfaa kutokana na huduma inayotolewa,
Naamini inawezekana Kama vile ilivyo kwa huduma za Barabara, Serikali inatengeneza miundombinu na wasafirishaji wa mizigo na abiria imebaki kwa wafanyabiashara, huduma Kama za mawasiliano nk Serikali iweke vigezo na itoze kodi kwa mashirika hayo.
Naamini inawezekana, mwisho naunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma mbalimbali kwa wananchi wa Tanzania.
Ahsanteni
Leo niongelee kuhusu huduma ya umeme, maji, na hifadhi ya jamii
1. UMEME
Tumeshuhudia juhudi za Serikali kutengeneza bwawa la kuzalisha umeme la Stigllers Geoge kwa lengo lla kuongeza kiwango Cha uzalushaji wa umeme nchini jambo litakalosaidia kupunguza Bei ya umeme hivyo kuchochea uanzishwaji wa viwanda nchini, pia Serikali imekuwa ikisimamia uzalishaji wa umeme katika mabwawa mbalimbali Kama vile Kidatu, Mtera, Nyumba ya Mungu nk
Ni Jambo jema Sana Ila mfumo uliopo wa uzalishaji umeme na usambazi wake unaruhusu ukiritimba unaoondoa ufanisi wa upatikanaji wa umeme nchini, Shirika la TANESCO ndilo pekee linalohusika kusimamia uzalishaji na usambazaji wa umeme kwa walaji, hii kwa mtazamo wangu sio sawa, ushauri wangu ni kuwa TANESCO ihusike katika uzalishaji tu na swala la usambazaji yawepo mashirika mengine ambayo yatahusika katika kutafuta wateja, kuongeza miundominu rahisi, kuwawekea umeme na kutoza bill kulingana na huduma waliyotoa.
Jambo Hilo litachochea ushindani ambao kwa nanna Moja au nyingine utaongeza ufanisi, utaongeza ajira na kupunguza ukiritimba Sana, Serikali ichukue Kodi na kuwekaa vigezo katika usajili wa mashirika hayo, ninaamini utafiti muhimu ukifanyika hapa Serikali itapunguza majukumu na fedha zinazotumika Sasa katika usambazaji wa umeme zingeelekezwa katika kuboresha elimu,afya na huduma nyingine muhimu kwa wananchi.
2. MAJI
Mfumo uliopo Sasa umegawanyika katika sehemu mbili kwa mtazamo wangu, Moja Serikali kuu inahusika katika kutafuta vyanzo vya maji na kuweka miundo mbinu ya uzalishaji wa maji katika Kila mkoa na hata usambazaji wa miundombinu hiyo katika maeneo mbalimbali.
Pili Serikali inakabidhi kazi ya kusimamia miundominu hiyo ambayo hukabidhiwa kwa mamlaka za.maji Mjini na za vijijini kwa mfabo, Mwanza Kuna Mwuwasa na Ruwasa, Iringa Kuna Iruwasa na Ruwasa Arusha Kuna Aruwasa na Ruwasa nk. Mfumo huu una kasoro kidogo kwa kuwa una ukiritimba kaatika upatikanaji wa maji kwa wananchi. Ushauri wangu ni kutokuwa na mamlaka badala yake Serikali ihusike katika uzalishaji wa maji na kuyauza maji hayo kwa mashirika ya usambazaji wa huduma za maji kwa wananchi ambayo yanaweza kuwa zaidi ya Moja
Mashirika haya yatakuwa na wajibu wa kutunza miundombinu na kuongeza mingine itakayowezesha upatikanaji wa maji kwa wananchi, Jambo Hilo litaongeza ufanisi na kuondoa ukiritimba uliopo, lakini pia litaongeza ajira kwa wahitimu wa ufundi katika njanja za maji. Lakini pia Kuna kasoro kubwa kwa jumuiya za maji vijijini ambazo Sasa zinasimamiwa na Ruwasa, hizi jumuiya hazina wataalamu wa kusimamia huduma za maji.
Jambo Hilo linazorotesha juhudi za Serikali na kuongeza migogoro katika maeneo husika, Naamini mashika hayo yatakuwa na wataalamu na mwananchi atabaki kuchagua Shirika lenye ufanisi katika utoaji wa huduma, nashauri utafiti ufanyike ili kufanya mapinduzi makubwa katika upatikanaji wa huduma hii muhimu.
3. HUDUMA ZA UHIFADHI WA JAMII
Hapa nashauri Serikali irudie mfumo uliokuwepo awali wa kufufua mashirika ya NSSF, NPF, LSSF nk mfumo wa Sasa umemfanya mfanyakazi kutokuwa na Uhuru wa kuchagua Shirika linalomfaa kutokana na huduma inayotolewa,
Naamini inawezekana Kama vile ilivyo kwa huduma za Barabara, Serikali inatengeneza miundombinu na wasafirishaji wa mizigo na abiria imebaki kwa wafanyabiashara, huduma Kama za mawasiliano nk Serikali iweke vigezo na itoze kodi kwa mashirika hayo.
Naamini inawezekana, mwisho naunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha huduma mbalimbali kwa wananchi wa Tanzania.
Ahsanteni