Ushauri wangu kwa MH Kigwangala

Ushauri wangu kwa MH Kigwangala

MESOYA

Senior Member
Joined
Aug 19, 2014
Posts
150
Reaction score
168
Mheshimiwa Kigwangala, Ukiwa waziri wa maliasili na utalii, binafisi napenda kutumia nafasi hii kukupongeza kwa kuteuliwa kwako kuwa waziri wa wizara hii nyeti na yenye maslahi makubwa kwa rasilimali za taifa letu.

Lakini katika hili niseme kwamba napata wasiwasi na mashaka makubwa juu ya utendaji wako. Na hii yote ni kutokana na mfumo mbaya wa utendaji kazi wenu wa kutumia vyombo vya habari. Ili kuwalaghai wananchi angali sheria za maliasili zikivunjwa . kwa faida ya rasilimali hii asilia ni vyema ukabadilika na kuacha siasa katika wizara hii, simamia sheria za wanyamapori kwa maana ya hifadhi zetu na sio kufuata kiu ya siasa chafu kwa kukwamisha juhudi za watendaji na wataalamu wa maliasili. Nimekuona Loliondo si jambo jema sana, badilika.

Na nikuambie kutunza mapori haya si kazi ndogo ila ni dhamira njema ya waasisi na hivyo ni vyema kuilinda tunu hii kwa masilahi ya vizazi vya sasa na vijavyo.
 
Mheshimiwa Kigwangala, Ukiwa waziri wa maliasili na utalii, binafisi napenda kutumia nafasi hii kukupongeza kwa kuteuliwa kwako kuwa waziri wa wizara hii nyeti na yenye maslahi makubwa kwa rasilimali za taifa letu.

Lakini katika hili niseme kwamba napata wasiwasi na mashaka makubwa juu ya utendaji wako. Na hii yote ni kutokana na mfumo mbaya wa utendaji kazi wenu wa kutumia vyombo vya habari. Ili kuwalaghai wananchi angali sheria za maliasili zikivunjwa . kwa faida ya rasilimali hii asilia ni vyema ukabadilika na kuacha siasa katika wizara hii, simamia sheria za wanyamapori kwa maana ya hifadhi zetu na sio kufuata kiu ya siasa chafu kwa kukwamisha juhudi za watendaji na wataalamu wa maliasili. Nimekuona Loliondo si jambo jema sana, badilika.

Na nikuambie kutunza mapori haya si kazi ndogo ila ni dhamira njema ya waasisi na hivyo ni vyema kuilinda tunu hii kwa masilahi ya vizazi vya sasa na vijavyo.
Vyombo vya habari vinatafuta habari ili kuhabarisha umma kinachoendelea kuhusu maliasili yao tena wewe mtoa mada hutaki tena.

Kwahiyo hutaki watanzania wajue kabisa kinachoendelea katika hiyo wizara au?

Ni sheria gani hizo umeshuhudia zinavunjwa mbele ya Waziri?

Na imani Waziri anafuata sheria za maliasili
 
Lakini katika hili niseme kwamba napata wasiwasi na mashaka makubwa juu ya utendaji wako. N
mwezi mmoja tu umeshamuhukumu?

wewe utakuwa na bifu naye, si bure
 
Back
Top Bottom