Ushauri: Wana Kilimanjaro rudini CCM muungane na Anna Mghwira kufufua uchumi; msibaki nyuma

Kididimo

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
3,791
3,360
Kwa tulio mbali na Mkoa wa Kilimanjaro, tumepokea kwa hisia tofauti kwa yaliyotokea pale Dodoma. Mkuu,huyo (Mama Anna Mghwira) amehamia rasmi Chama Tawala na kuachana na upinzani. Ni ushauri tu, wanamkoa huo wamuunge mkono pia kiitikadi ili kusukuma maendeleo mbele.

Siyo siri,kwa muda mrefu sasa, Mkoa wa Kili umekuwa ngome kuu ya siasa za upinzani kwa Chama Tawala. Ukiangalia kwa jicho la pembeni,huenda Mkoa ukawa umejirudisha nyuma kutokana na aina ya siasa za upinzani zenye uelekeo wa ubishi zaidi kuliko tija.

Tumeona mikoa mingi ikianza kuimarika zaidi ya hata Mkoa huo uliokuwa ukisifika kuwa wa mfano kwa maendeleo hapa nchini.

Ninaamini,Mkuu wa Mkoa Anna Mghwira ameona mbali katika mageuzi ya uchumi lazima aendane na itikadi ya ChamaTawala,hivyo ni vyema aungwe mkono.

Njia nzuri ya kumuunga mkono, ni kwanza, wananchi wa mkoa huo kwa wingi wao,kuweka mwelekeo mmoja wa kiitikadi ili kumtia moyo, yeye,chama chake, na Viongozi wake waliomteua na wanaomsimamia.

Hayo ni maoni yangu binafsi.
 
Mbona kuna wilaya nyingi sana ambazo zipo chini ya utawala wa ccm tangia uhuru mpaka sasa ni maskini mara 100 na zaidi kuliko Kilimanjaro.
Mfano mzuri ni wilaya za mikoa ya Dodoma, Mtwara, Lindi, Songea, Rukwa, Sumbawanga n.k au tembelea wilaya ya Ileje iliyopo Songwe kwa maelezo zaidi
 
Mimi huwa naupenda sana Upinzani wa Mkoa wa Kilimanjaro

1) Hukuti wakifanya Maandamano ya Ghasia
2) Kwny Shughuli za Maendeleo hushiriki kwa Njia zote bila ya kususa
3) Hawafanyi vurugu Siku za Uchaguzi

Mh.Mbowe awafundishe Wapinzani wa Maeneo Mengine
 
Mbona kuna wilaya nyingi sana ambazo zipo chini ya utawala wa ccm tangia uhuru mpaka sasa ni maskini mara 100 na zaidi kuliko Kilimanjaro.
Mfano mzuri ni wilaya za mikoa ya Dodoma, Mtwara, Lindi, Songea, Rukwa, Sumbawanga n.k au tembelea wilaya ya Ileje iliyopo Songwe kwa maelezo zaidi
Baadhi ya hizo Wilaya ulizotaja,nimetembelea kwa karibuni mfano Nkasi Rukwa,maendeleo yako full supported na serikali,na wako speed kuanzia barabara (lami),afya nk.
 
Kwa tulio mbali na Mkoa wa Kilimanjaro, tumepokea kwa hisia tofauti kwa yaliyotokea pale Dodoma. Mkuu,huyo (Mama Anna Mghwira) amehamia rasmi Chama Tawala na kuachana na upinzani. Ni ushauri tu, wanamkoa huo wamuunge mkono pia kiitikadi ili kusukuma maendeleo mbele.

Siyo siri,kwa muda mrefu sasa, Mkoa wa Kili umekuwa ngome kuu ya siasa za upinzani kwa Chama Tawala. Ukiangalia kwa jicho la pembeni,huenda Mkoa ukawa umejirudisha nyuma kutokana na aina ya siasa za upinzani zenye uelekeo wa ubishi zaidi kuliko tija.

Tumeona mikoa mingi ikianza kuimarika zaidi ya hata Mkoa huo uliokuwa ukisifika kuwa wa mfano kwa maendeleo hapa nchini.

Ninaamini,Mkuu wa Mkoa Anna Mghwira ameona mbali katika mageuzi ya uchumi lazima aendane na itikadi ya ChamaTawala,hivyo ni vyema aungwe mkono.

Njia nzuri ya kumuunga mkono, ni kwanza, wananchi wa mkoa huo kwa wingi wao,kuweka mwelekeo mmoja wa kiitikadi ili kumtia moyo, yeye,chama chake, na Viongozi wake waliomteua na wanaomsimamia.

Hayo ni maoni yangu binafsi.

Maendeleo ya Kilimanjaro yalikuwepo kabla ya hicho chama kuwepo, iweje leo ufikirie kuwa hicho chama ndicho kitaendeleza Kilimanjaro? Kianzie kuleta maendeleo kule kilikozaliwa - Dodoma na Wilaya zake!!!
 
Kwa tulio mbali na Mkoa wa Kilimanjaro, tumepokea kwa hisia tofauti kwa yaliyotokea pale Dodoma. Mkuu,huyo (Mama Anna Mghwira) amehamia rasmi Chama Tawala na kuachana na upinzani. Ni ushauri tu, wanamkoa huo wamuunge mkono pia kiitikadi ili kusukuma maendeleo mbele.

Siyo siri,kwa muda mrefu sasa, Mkoa wa Kili umekuwa ngome kuu ya siasa za upinzani kwa Chama Tawala. Ukiangalia kwa jicho la pembeni,huenda Mkoa ukawa umejirudisha nyuma kutokana na aina ya siasa za upinzani zenye uelekeo wa ubishi zaidi kuliko tija.

Tumeona mikoa mingi ikianza kuimarika zaidi ya hata Mkoa huo uliokuwa ukisifika kuwa wa mfano kwa maendeleo hapa nchini.

Ninaamini,Mkuu wa Mkoa Anna Mghwira ameona mbali katika mageuzi ya uchumi lazima aendane na itikadi ya ChamaTawala,hivyo ni vyema aungwe mkono.

Njia nzuri ya kumuunga mkono, ni kwanza, wananchi wa mkoa huo kwa wingi wao,kuweka mwelekeo mmoja wa kiitikadi ili kumtia moyo, yeye,chama chake, na Viongozi wake waliomteua na wanaomsimamia.

Hayo ni maoni yangu binafsi.
Kamwe haitotokea,sababu watu wa moshi wanajitambua
 
Habadiliki MTU kiitikadi na maendeleo yeye mwenyewe Raisi anasema kila Leo maendeleo hayana chama inakuaje mseme wanakilimanjaro tubadilike kiitikadi tutaendelea wenyewe kwani tangu awali tunaendelea kwa juhudi zetu wenyewe hamtaki kuungana nasi tuachieni mkoa wetu mpambane na huko kwingine mnakopenda
 
Habadiliki MTU kiitikadi na maendeleo yeye mwenyewe Raisi anasema kila Leo maendeleo hayana chama inakuaje mseme wanakilimanjaro tubadilike kiitikadi tutaendelea wenyewe kwani tangu awali tunaendelea kwa juhudi zetu wenyewe hamtaki kuungana nasi tuachieni mkoa wetu mpambane na huko kwingine mnakopenda
Ingekuwa vyema,kama ungesikiliza sababu alizotoa za kwa nini Mkuu huyo wa Mkoa,ameamua kubadili chama. Of course,ameona mbali na ni jambo zuri pia.
 
Kwa mtizamo wa mtoa mada amethibitisha pasi na shaka kuwa serikali ya CCM inaubaguzi wa kisiasa.

Labda mleta mada atuambue kuwa pesa za maendeleo ya mkoa na majimbo ya Kilimanjaro zipo wapi?
Je, zimewekwa tu zinasubiri siku wakiwachagua wawakilishi wa CCM ndio zitolewe?

Na je ,hao wanachama walioko huko wanaoadhibiwa na kuunganishwa na ubaguzi huo wao haki yao wataendelea kuisubiri mpaka pale wote warakaporejea CCM au itakuaje?

Kwa kweli CCM ina watu waliolewa
Madaraka na hawataki kuona mbele hata miaka mitano ijayo.

Labda niwaambie kitu cha maana kabisa na huenda kama wanaCCM waliopo kuna mwenye hata chembe ya mbegu ya haradali ya fikra na maono ya Mwalimu Nyerere ataliona na kujua tumetoka wapi na tunakwenda wapi?

Ni hivi CCM inajiita sisi Chama Tawala kwa sababu kuna wale wapinzani.
Amini ,Amini ,Amini nawaambie enye wenye mioyo migumu ndani ya CCM siku mkifanikiwa kuua upinzani mtakua na sisi Wakristo na Wale Waislam.
Hapo ndipo vitakapoibuka vyama vya Kidini mana vitaambatana na Haki za kiimani na kupinga dhulma kiimani.
Uchumi utakosolewa kwa misingi ya kiimani halikadhalika siasa itazungumzwa kwa misingi ya kiimani.
Hapo ndipo litakapotimia lile neno linalosema kuwa wapi kushinda kwako ewe CCM ?
Na uwapi umaarufu wako na ule msemo wako wa wale wapinga pinga ?
Mana mtakua mmegawanyika mpaka ndani ya viti vya kukalia huko madarakani.
Nyerera alikua ni mwenye maono Makubwa sana.
Mungu hua anaweka maono yake kwa mtu mwenye juhudi ya kusimama katika kweli.
Nyerere kwa muda aliotawala na muda aliokaa pembeni alijifunza na kuona mengi!
Aliona mustakabali wa Nchi yetu na kujua nini kinachoweza kujitokeza endapo hatutaruhusu vyama vya kisiasa kuwa na ushindani ili vitumiwe na wale wenye mawazo tofauti kufikisha hoja zao.

Sasa CCM wao wanatizama utawala tu.
Hivi mbunge wa Upinzani anazuia vipi watu wasipatiwe dawa hospitalini au shule zisipelekewe walimu au reli isijengwe kwenye eneo hilo?
Diwani wa upinzani anazuia vipi watu kupatiwa maji safi na salama?
Mbunge wa upinzani anazuia vipi watu wasilime mashamba yao na kupata masoko?

Hivi tunapoijenga Dodoma wote tumezaliwa Dodoma?
Kuna watu wa Mbeya wanaishi Kilimanjaro kikazi na kibiashara au wameolewa huko hao haki yao inapatikana vipi kama patakua na watu wenye mitizamo finyu kama mleta mada
Kwa nini Kodi nayo isibaguliwe kwa namna hiyo kwamba kwa sababu kule hatukupata kura basi na kodi zao hatuchukui?

Kama kuna mtu yeyote mwenye mawazo kama ya huyu mleta mada kuwa eti maendeleo hayatapelekwa sehemu kwa sababu ya Itikadi za kisiasa basi mtu huyo hafai hata kuitwa mtanzania zaidi ya mbaguzi na kaburu.

Vyama tumeanzisha wenyewe lakini vimegeuka na kutufanya watumwa wa fikra na hata kufikia mahali pa kukatana mapanga na kuwaza mawazo hasi ya kunyimana maendeleo kwa sababu ya vyama tu.

Ujinga huo pia niliusikua wakati wa Kampeni za udiwani ,Chadema walikua wakitoa kauli hizo za kipuuzi na kijingwa kwamba eti sisi ndio wenye halimashauri mukimpa diwani mwanachama wa CCM atawaleteaje maendeleo ?
Ni siasa Mbaya sana.

Tunawaomba CCM na Chadema watafute mbinu nyingine za kunadi sera lakini sio hizo mbinu na hoja Mufilisi za kuwanyima maendeleo wale wanaochagua wapinzani.

Mimi nadhani mtu anapoomba madaraka anaomba ili awatumikie wananchi wote kwa haki na kwa usawa.
Uchaguzi mkuu wa Taifa sio sawa na chaguzi nani ya vyama.
Sasa naona CCM wameanza kuufananisha uchaguzi wa viongozi wa serikali sawa na ule wa chama.
Ukishakua kiongozi wa umma kama waziri wa Tamisemi basi masuala ya maendeleo unapaswa kuyasimamia bila kuweka itikadi za vyama.
Ukishindwa kusimamia maendeleo kwa usawa basi unapaswa usijisumbue tena kuomba kura zaidi ya kiwaachia watu wanye kumheshimu Mungu na kujalia wanadamu wote ili wawatumikie watu kwa usawa na haki.

Ni wakati sasa kwa wabunge wetu kupigania maendeleo ya majimbo yao kwa nguvu zote na kuangalia kila mwaka kuwa ni kwa nini jimbo lake na Wilaya yake haipangiwi fungu la maendeleo kama majimbo mengine ili hali wananchi wake nao ni walipa kodi kama wengine!!
 
Kwa tulio mbali na Mkoa wa Kilimanjaro, tumepokea kwa hisia tofauti kwa yaliyotokea pale Dodoma. Mkuu,huyo (Mama Anna Mghwira) amehamia rasmi Chama Tawala na kuachana na upinzani. Ni ushauri tu, wanamkoa huo wamuunge mkono pia kiitikadi ili kusukuma maendeleo mbele.

Siyo siri,kwa muda mrefu sasa, Mkoa wa Kili umekuwa ngome kuu ya siasa za upinzani kwa Chama Tawala. Ukiangalia kwa jicho la pembeni,huenda Mkoa ukawa umejirudisha nyuma kutokana na aina ya siasa za upinzani zenye uelekeo wa ubishi zaidi kuliko tija.

Tumeona mikoa mingi ikianza kuimarika zaidi ya hata Mkoa huo uliokuwa ukisifika kuwa wa mfano kwa maendeleo hapa nchini.

Ninaamini,Mkuu wa Mkoa Anna Mghwira ameona mbali katika mageuzi ya uchumi lazima aendane na itikadi ya ChamaTawala,hivyo ni vyema aungwe mkono.

Njia nzuri ya kumuunga mkono, ni kwanza, wananchi wa mkoa huo kwa wingi wao,kuweka mwelekeo mmoja wa kiitikadi ili kumtia moyo, yeye,chama chake, na Viongozi wake waliomteua na wanaomsimamia.

Hayo ni maoni yangu binafsi.

Inaonekana wala hujui unazaungumza nini, wakati huo mkoa ukiwa na wapingaji kuna mkuu wa mkoa yeyote aliyewahi kuwa nje ya ccm? Mkoa wa kilimanjaro una maendeleo sio kwa upendeleo toka serekali bali kwa watu wake kuwa wachapa kazi.
 
Miaka zaidi ya 55 Tanzania haina umeme wa uhakika, hao Ccm unaowasema mbona wameshindwa kutuletea umeme wa uhakika?
Daktari mmoja anahudumia wananchi 25,000/- kwa mwaka, hiyo Ccm unaiotaja kwanini imeshindwa kuajiri madaktari na kupunguza tatizo la upungufu wa madaktari?
Shule za serikali za msingi zina wanafunzi zaidi ya milioni 5, lakini wana walimu laki 1 tu. Hiyo Ccm imeshindwa kuajiri walimu kupunguza tatizo la upungufu.
Huu upupu wako kadanganye wajinga wenzako.
 
Back
Top Bottom