Ushauri wa bure kwa watanzania hasa vijana

Ushauri wa bure kwa watanzania hasa vijana

ss3

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
213
Reaction score
98
Ndugu zangu vijana
Naimani kila mmoja popote alipo anahangaika kujitafutia riziki. Wengine kwenye jua na wengine kwenye kivuli. Wengine wamejiajiri na wengine wameajiriwa. Napenda kutambua pia wale ambao wapo makwao wamepumzika wakiwaza maisha yatakuwaje maana hawajajiajiri wala hawajaajiriwa. Wala msijali kama mtafanya maamuzi sahihi sasa hamtajuta kwa muda uliosalia.
Naomba nitoe mifano michache;
Kuna vijana wako pale bank wanahesabu fedha lukuki na nadhani toka asubuhi washahesabu zaidi ya bilioni na kuweka taarifa sahihi kwa ajili ya ukaguzi baadae. Bank itafungwa saa kumi alafu wao watabaki ndani wakibalance hadi saa 11 au 12 jioni ndipo watoke wengine wapande gari za umma na wale wenye za mkopo wapande kurudi makwao. Mwisho wa mwezi watapokea 1,000,000.
2. Kuna wale waliopo kwenye makampuni ya simu hawa hali yao ndio mbaya zaidi kwani wao kuna wanaotoka mchana na wengine wanaingia na wengine wanaingia midnight. Wengi hulipwa kwa masaa na salary before tax Mara nyingi ni laki 4!.
3. Kuna walioko viwandani hawa jamani tupige magoti tusali maana kuna wengine hata sasa wako mahospitali kwa ajili ya afya zao kuwa duni kutokana na mazingira duni ya kazi. Naomba anayesoma akifika hapa akae dakika moja unyamavu kuwaombea.
4. Wapi wale walioko manyumbani wakijaribu kuviziavizia hawa walioko kwenye haya mateso waachie angalau na wao mkono uende kinywani. Hawa hata ukiwaam is wakafanye kazi ya kuchanganya sumu kwa mkono wataenda hata kwa sh500.000 kwa mwezi.
Nini chanzo cha yote haya? Ajira ajira ajira hakuna!!
Ni kweli ajira za kuajiriwa hakuna na kama ziko ni zile mbaya zisizoweka kukaliwa na binadamu anayejitambua.
Ushauri Wangu kwa wote kabisa ni kwamba jitahidini kuunda partnership mjipange mjitahidi kujiajiri kwa kweli muache kutegemea cost of production kuran maisha yenu mtateseka sana. Hii dhana ya kujiajiri inabezwa sana lakini hebu ingia utaona utamu wake. Jiulize hiyo kampuni unayoifanyia kazi inaingia shilingi ngapi kwa siku! Alafu wewe unachukua shilingi ngapi? Ni asilimia ngapi? Usilie bali jitahidi kuwajibika.
Ni kweli wakati meingine kitachukua muda Ila in a long run utakuja kuwashangaa sana walioajiriwa.
Wakati namaliza chuo cha dodoma na kuamua kufungua organization yangu ya kilimo watu waliniona vuvuzela Ila Leo wakipita wanasema huyu jamaa jembe! Mwezi uliopita kwenye branch yetu tumetoa nafasi tano za marketing officer na kuna baadhi nilisoma nao 2012 pale dodoma nimewaona bado wanatafuta kazi. Niliwaonea huruma Ila ndio nimeona niwaandikie haya .
Mwenye masikio na asikie mwenye macho na aone!
Maisha ni ujumla wa maamuzi unayofanya kila uchao
 
Kujiajir vigumu saana ngoja tusubir kuajiliwa tuu...
 
Kama ni ngumu basi subiri hiyo raisi maana ndio haitakuto jasho
 
Ndugu zangu vijana
Naimani kila mmoja popote alipo anahangaika kujitafutia riziki. Wengine kwenye jua na wengine kwenye kivuli. Wengine wamejiajiri na wengine wameajiriwa. Napenda kutambua pia wale ambao wapo makwao wamepumzika wakiwaza maisha yatakuwaje maana hawajajiajiri wala hawajaajiriwa. Wala msijali kama mtafanya maamuzi sahihi sasa hamtajuta kwa muda uliosalia.
Naomba nitoe mifano michache;
Kuna vijana wako pale bank wanahesabu fedha lukuki na nadhani toka asubuhi washahesabu zaidi ya bilioni na kuweka taarifa sahihi kwa ajili ya ukaguzi baadae. Bank itafungwa saa kumi alafu wao watabaki ndani wakibalance hadi saa 11 au 12 jioni ndipo watoke wengine wapande gari za umma na wale wenye za mkopo wapande kurudi makwao. Mwisho wa mwezi watapokea 1,000,000.
2. Kuna wale waliopo kwenye makampuni ya simu hawa hali yao ndio mbaya zaidi kwani wao kuna wanaotoka mchana na wengine wanaingia na wengine wanaingia midnight. Wengi hulipwa kwa masaa na salary before tax Mara nyingi ni laki 4!.
3. Kuna walioko viwandani hawa jamani tupige magoti tusali maana kuna wengine hata sasa wako mahospitali kwa ajili ya afya zao kuwa duni kutokana na mazingira duni ya kazi. Naomba anayesoma akifika hapa akae dakika moja unyamavu kuwaombea.
4. Wapi wale walioko manyumbani wakijaribu kuviziavizia hawa walioko kwenye haya mateso waachie angalau na wao mkono uende kinywani. Hawa hata ukiwaam is wakafanye kazi ya kuchanganya sumu kwa mkono wataenda hata kwa sh500.000 kwa mwezi.
Nini chanzo cha yote haya? Ajira ajira ajira hakuna!!
Ni kweli ajira za kuajiriwa hakuna na kama ziko ni zile mbaya zisizoweka kukaliwa na binadamu anayejitambua.
Ushauri Wangu kwa wote kabisa ni kwamba jitahidini kuunda partnership mjipange mjitahidi kujiajiri kwa kweli muache kutegemea cost of production kuran maisha yenu mtateseka sana. Hii dhana ya kujiajiri inabezwa sana lakini hebu ingia utaona utamu wake. Jiulize hiyo kampuni unayoifanyia kazi inaingia shilingi ngapi kwa siku! Alafu wewe unachukua shilingi ngapi? Ni asilimia ngapi? Usilie bali jitahidi kuwajibika.
Ni kweli wakati meingine kitachukua muda Ila in a long run utakuja kuwashangaa sana walioajiriwa.
Wakati namaliza chuo cha dodoma na kuamua kufungua organization yangu ya kilimo watu waliniona vuvuzela Ila Leo wakipita wanasema huyu jamaa jembe! Mwezi uliopita kwenye branch yetu tumetoa nafasi tano za marketing officer na kuna baadhi nilisoma nao 2012 pale dodoma nimewaona bado wanatafuta kazi. Niliwaonea huruma Ila ndio nimeona niwaandikie haya .
Mwenye masikio na asikie mwenye macho na aone!
Maisha ni ujumla wa maamuzi unayofanya kila uchao

Thanx for ure inspiring words..nmekupenda bure
 
Kila mtu akijiajiri nanai ataajiriwa? wewe mbona umeajiri? sasa kila mtu angejiajiri ww ungepata wa kumuajiri?
Be realistic.
 
Nimekuelewa mkuu ila mtaji ni tatizo sana

Tatizo La Mtaji Limekuwa Ni Kama Kichaka Tu Kwa Wavivu Na Wasiofikiri Sana Kujifichia. Utakuta Mtu Analalama Hakuna Mtaji Ila Ukimuuliza Kama Ameshaandaa Project Au Business Plan Na Kuiprint Au Kuisave Kwenye Computer Yake Ili Akipata Mtaji Tu Aifanye - Hata Nayo Pia Hana! Jamani Vijana Wenzangu, Let's Go That Extra Mile. Hata Kama Hauna Mtaji Kuwa Na Plan Iliyokamilika Na Inayoeleweka Na Uanze Kuifanya Kidogo Kidogo. Pesa Za Mtaji Zitakukuta Mbele Ya Safari. Kwa Mtu Mwenye Determination Na Focus Hata 100,000/= Ni Mtaji Tosha Kabisa. Tujipange Jamani
 
asante sana mkuu unifungua sana macho
 
Ahsante kwa ushauri wako lkn maisha mazuri sio tu kwa kujiajiri wapo walioajiriwa na wana maisha mazuri hata ww umeadmit kuajiri watu so watu wote wangejiajiri ungepata wapi man power?..tatizo la vijana Tanzania ni investment... We should know how to invest on different things...ukiangalia bakhressa ame invest katika vitu vingi ambavyo mwisho wa siku vinamletea pato kubwa ..mwangalie Dangote yupo kwenye cement,gas hata vyakula...hata bahari imekuwa kubwa kwasababu mito yote inamwaga maji huko....hoja yako nzuri lkn inamapungufu maana unaweza kujiajiri na at the same time ukiwa umeajiriwa...lkn still utahitaji watu wa kuajiri
 
Kwa weweunaedai mtaj wa lak moja unatosha, heb twambie unatosha kwa kufanyia aina ip ya biashara? Mm pia sina kaz nataman kufanya biashara au kuajiriwa
 
Kwa weweunaedai mtaj wa lak moja unatosha, heb twambie unatosha kwa kufanyia aina ip ya biashara? Mm pia sina kaz nataman kufanya biashara au kuajiriwa

Shida Ni Kwa Watu Waliosoma Na Kupata Angalau Ka Certificate Tu Au Ka Diploma, Akili Zao Zoote Zipo Benki Na Ofisi Kubwa Kubwa Ili Wapigwe Na Viyoyozi - In Short WHITE COLLAR JOBS! Wasio Na Mapozi Na Wenye Long Term Plan Wanaanza Na Kitu Kidogo Tu Wanachoweza Kisha Wanakiendeleza Na Kufikia Makubwa Waliyokuwa Wanayawaza.
Hiyo Laki Moja Unaiona Ndogo Wakati Watu Wanaanza Kuuza Mboga Za Majani Kwa Mtaji Wa Sh 20,000/= Tu Na Kupata Faida Ya Sh 8,000/= Kila Siku. Sasa Mwenzangu Mpaka Lip Shine Na Powder Na Kuvaa Wig Kichwani Najua Hapa Hatanielewa Kabisa.
Huo Ni Mfano Tu Kuonesha Kwamba 100,000/= Inatosha Kabisa Kwa Mtu Mwenye Mipango Mizuri Na Aliyetayari Kuanza Na Kidogo. Ila Kwa Mtu Mvivu Wa Kufikiri Na Asiye Na Plan Nzuri Hata Shillingi 1,000,000/= Kwake Haitoshi Kama Mtaji.
UBONGO WAKO MAISHA YAKO!
 
Shida Ni Kwa Watu Waliosoma Na Kupata Angalau Ka Certificate Tu Au Ka Diploma, Akili Zao Zoote Zipo Benki Na Ofisi Kubwa Kubwa Ili Wapigwe Na Viyoyozi -

Post yako #9 umeenda vizuri ila hapa sidhani kama uko sahihi kwa jinsi ulivyo wasema



Hiyo Laki Moja Unaiona Ndogo Wakati Watu Wanaanza Kuuza Mboga Za Majani Kwa Mtaji Wa Sh 20,000/= Tu Na Kupata Faida Ya Sh 8,000/= Kila Siku. Sasa Mwenzangu Mpaka Lip Shine Na Powder Na Kuvaa Wig Kichwani Najua Hapa Hatanielewa Kabisa.

Una kitu ambacho kama ukipata muda yawezekana kikawa manufaa kwa muulizaji lakini kwa hilo hapo juu sidhani kama ataweza kutilia maanani huu ushauri
 
Lazima tuelewe uhalisia wa kile kinachoendelea kwenye soko letu la ajira. Uhitaji wa ajira ni mkubwa ukilinganisha na ajira zilizoko. Pia kuna tatizo la elimu na ujuzi kwamba kutokana na matumizi ya computer hata mtu ambaye hajasoma account au financial anaweza kuwa trained kwa siku mbili ukamwona anafanya kazi hizo kama anamjua mtu hapo bank. Pia sehemu nyingine zipo hivyo. Ukiendelea kulalamika utaachwa maana ni tatizo lililopo. Pia hutakuwa na wakumlalamikia. Pia kupata ajira nxuri nako ni ngumu sana kwani ndizo wanapeana maana kampuni nyingi haziact to the public. Kuna chache kama PWC hawa kweli hawawezi kuajiriwa hivihivi wanaajiri watu ambao ni qualified kwelikweli.
Mimi ninayeandika napass nzuri kwelikweli ngazi zoote Ila tatizo hili nililiona wakati na tafuta field niliteseka sana maana kuna mambo mengi ndani ya system. Nikaamua kujiajiri kila mtu alishangaa lakini wamekija kurealize halihalisi.
Hebu imagine nimemaliza mwaka wa pili na gpa ya 4.6 project planning and management alafu natafuta field sipati!!!! Nikasema kazi itakuaje?
Nikawaambia marafiki zangu wanne tuanze kutafuta kujiajiri. Tukavhangishana ikafika kama laki saba tukafungua kampuni yetu then tukawa tunaongeza na wabunge siku tukiwaona wakatupigapiga jeki tunanyanyuka sana tunaweza hata kuomba kamsaada nje cha miradi yetu tunapata.
Ni safari lakini ukiwa na malengo unatoboa. Wakati mwingine naona post za watu humu zinasikirisha sana. Eti mtu anaomba ku volunteer!!!!!
Kisa ni nini? Yaani unadegree au deploma yako ya halali alafu unaomba kumfanyia mtu kazi!!!!!
Hebu try another chance bhana. Jiorganizini mfungue association/company/ngo muandike proposal za miradi na kufanya consultant bhana. Nyie ni watu wa dhamani sana sema hamtaki kurealiza. Kuna consultant yuko hapa kwenye kampuni yetu juzi kuna mradi wa kigogo mmoja ameleta anataka afanyiwe cost/benefits evaluation kwa shilingi mil 2 mheshimiwa kakataa!! Ila ingekuwa wewe ungerukaruka si ndio. Wewe unadhamani sana.
Kila kitu kinawezekana
 
Wewe ulipata wapi mtaji?

Hii ndio point ya msingi. ni watz weng sana hupanda majukwaan kushaur juu ya swala zma la kujiajir ni kweli ni hoja ya msingi ila inaaply vp kwa capitalless kuitekeleza iyo dhana.mtoa mada ametumia mfano wake yeye ila ameshindwa kueleza wanajamv ni kwa vp amefkia alipo ili awe role modal kwa wengine.
 
Kabla hujafikiri capital hebu niweke akili yako yote kwenye biashara. Kuna rafiki yangu mmoja aliniomba ushauri nifanyeje mtaji ni shida. Nimemwambia ukiangalia kwa harak unaweza kuwa na sh ngapi? Akaniambia laki tatu. Nikamwambia aende pale handeni tanga kuna vijana wanaganya miradi ya kulima mboga na biashara za kuziuza awaombe kushirikiana nao ili wamsaidie japo kwa hiyo laki tatu. Sasa hivi wote wanamtegemea katika ushauri kwani anabidii sana katika kazi. Leo analeta mzigo wa shilingi milioni zaidi ya 25 hapo dar! Sasa jamani hii si rahisi tuu?
 
Kabla hujafikiri capital hebu niweke akili yako yote kwenye biashara. Kuna rafiki yangu mmoja aliniomba ushauri nifanyeje mtaji ni shida. Nimemwambia ukiangalia kwa harak unaweza kuwa na sh ngapi? Akaniambia laki tatu. Nikamwambia aende pale handeni tanga kuna vijana wanaganya miradi ya kulima mboga na biashara za kuziuza awaombe kushirikiana nao ili wamsaidie japo kwa hiyo laki tatu. Sasa hivi wote wanamtegemea katika ushauri kwani anabidii sana katika kazi. Leo analeta mzigo wa shilingi milioni zaidi ya 25 hapo dar! Sasa jamani hii si rahisi tuu?

Tatizo Letu Wengi Ni Kushindwa Kuwaza Vizuri Na Kuringa Kukataa Kuanza Japo Na Kitu Kidogo Tu. Kuna Miradi Midogo Midogo Mingi Sana Ya Kuanza Na Mtaji Wa Chini Ya Sh Laki 3 Lakini Watu Hawataki "kazi Za Kishamba". Mtu Hana Mtaji Wa Laki 2, Lakini Ana Laptop, Smartphone, Viatu Pea Kadhaa, Nguo Kedekede, Nguvu, Akili N.k.
 
Back
Top Bottom