Ushauri wa Bure kwa Polisi barabara ya Ngara - Isaka Kipande cha Benaco Nyakanazi

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,854
35,862
Ni ajabu na kweli kuwa katika barabara hii polisi wamejizatiti na vi tochi kudhibiti mwendo na eti kuwa sasa hivi wako katika wiki ya nenda kwa usalama kukagua magari na hata kuthubutu kutoza mafaini magari yapitayo njia hii.

Tuwe fair serikali ilipaswa kufikishwa mahakamani kuwalipa fidia wote wanaopitisha magari yao katika njia hii huku wakilipa kodi zote stahili. Kuna haja gani ya kukagua magari kwenye njia yenye mashimo mashimo yenye ukubwa wa kushangaza katikati ya njia, labda kama ni kukagua ili kuthibitisha kuwa kweli kwa barabara kama ilivyo hakika yatakuwa yameharibika. Ukaguzi upi sasa? Wiki ipi ya usalama barabarani? Acheni ubabaishaji, shaurini barabara kutengenezwa kwanza kabla ya kuendekeza kuona vibanzi machoni pa wenzenu.

Tunakoelekea sasa ni kwenye mvua nyingi tu. Barabara kama iliyo kwenye hii clip itakuwa na tija gani kwa mwenye gari au mwenye kusafiri katika njia hii?

Wekezeni kwenye kutoa boriti kwenye macho yenu kabla ya kushadadia vibanzi kwenye macho ya wenzenu kimagumashi magumashi kumbe lengo lenu halisi ni pesa wala si usalama wa raia. Mengine yote kumbe ni machozi ya mamba tu hali kinachotafutwa ni kufikisha malengo ya faini mlizojiwekea ili mkajinufaishe wenyewe binafsi kwa mgongo wa serikali.

Angalia clip hii yenye hali ya ujumla ya barabara hii Benaco Nyakanazi yapata 90km.

Pathetic!

Pia soma; Sasa barabara ya Lusahunga – Rusumo yenye urefu wa kilomita 92, kujengwa kwa Bilioni 153
 
Barabara ile ukipita usiku alafu ukutane na kizuizi, unaweza sema umetekwa na majambazi, kumbe ni ukaguzi...kuanzia runzewe hadi shamba la nyege huwa sipaelewi kabisa
 
Barabara hii kiukweli inahitaji Marekebusho makubwa
Nimoja ya barabara zenye shida
tochi nisheria
haingalii Ubovu wala uzuri
jiulize kwanini zinasoma Overspeed?
 
Barabara hii kiukweli inahitaji Marekebusho makubwa
Nimoja ya barabara zenye shida
tochi nisheria
haiangalii Ubovu wala uzuri
jiulize kwanini zinasoma Overspeed?
 
Barabara ile ukipita usiku alafu ukutane na kizuizi, unaweza sema umetekwa na majambazi, kumbe ni ukaguzi...kuanzia runzewe hadi shamba la nyege huwa sipaelewi kabisa

Palikuwa na haja ya kuangalia namna ya kuwajibisha serikali hizi kwa hasara zinazowapa wananchi wake kwa kushindwa kutengeneza miundo mbinu iliyoko katika dhamana zake huku wakichukua kodi zote kama wanavyotaka na kila uchao.

Serikali gani hizi zisizowajibika lakini zinajua kutoza faini tu kwa ubovu unaoletwa na ubovu wa miundo mbinu yao?
 
Barabara hii kiukweli inahitaji Marekebusho makubwa
Nimoja ya barabara zenye shida
tochi nisheria
haingalii Ubovu wala uzuri
jiulize kwanini zinasoma Overspeed?

Mkuu hakuna overspeed inayoweza soma humu. Zaidi ya kuwa wanategea kwenye vi sehemu vyenye urefu wa 100m vyenye nafuu. Kumbuka tochi zinasoma capped speed siyo average speed.
 
Barabara hii kiukweli inahitaji Marekebusho makubwa
Nimoja ya barabara zenye shida
tochi nisheria
haiangalii Ubovu wala uzuri
jiulize kwanini zinasoma Overspeed?
Overspeed iwepo kwenye barabara ya mashimo makubwa kama alivyo eleza mleta mada.
By the way ipi logic ya kuweka matuta barabarani?
 
Hiyo barabara ilikuwa na lami yote kuanzia Kahama mpaka boader ya Rusumo Rwanda na boader ya Kobelo Burundi.

Kama kwa sasa iko hivyo kama clip inavyoonekana basi itakuwa katika matengenezo mapya kabisa.
 
Hizo faini wanazopiga zitumike basi kuboreshea miundombinu ya barabarani au nalo hili haliwezekani
 
Hizo faini wanazopiga zitumike basi kuboreshea miundombinu ya barabarani au nalo hili haliwezekani

Mkuu hilo haliwezekani kwani wanapata commissions kubwa tokea humo. Kwa maana nyingine wapo katika kukusanya pesa zao binafsi wala si za serikali tena. Cha kujiuliza sijui kwa nini wao tu wajimilikishe pesa za faini? Vipi faini za mahakamani, malipo hospitalini, faini TCRA nk wao commissions za faini hakuna?
 
Mkuu hilo haliwezekani kwani wanapata commissions kubwa tokea humo. Kwa maana nyingine wapo katika kukusanya pesa zao binafsi wala si za serikali tena. Cha kujiuliza sijui kwa nini wao tu wajimilikishe pesa za faini? Vipi faini za mahakamani, malipo hospitalini, faini TCRA nk wao commissions za faini hakuna?
Basi hapo ni shida mkuu...daaah
 
Hii road imenipasulia tairi juzi nikitoka Lusahunga tu nyakanazi!!! Mbovu sana!!!
 
Ni ajabu na kweli kuwa katika barabara hii polisi wamejizatiti na vi tochi kudhibiti mwendo na eti kuwa sasa hivi wako katika wiki ya nenda kwa usalama kukagua magari na hata kuthubutu kutoza mafaini magari yapitayo njia hii.

Tuwe fair serikali ilipaswa kufikishwa mahakamani kuwalipa fidia wote wanaopitisha magari yao katika njia hii huku wakilipa kodi zote stahili. Kuna haja gani ya kukagua magari kwenye njia yenye mashimo mashimo yenye ukubwa wa kushangaza katikati ya njia, labda kama ni kukagua ili kuthibitisha kuwa kweli kwa barabara kama ilivyo hakika yatakuwa yameharibika. Ukaguzi upi sasa? Wiki ipi ya usalama barabarani? Acheni ubabaishaji, shaurini barabara kutengenezwa kwanza kabla ya kuendekeza kuona vibanzi machoni pa wenzenu.

Tunakoelekea sasa ni kwenye mvua nyingi tu. Barabara kama iliyo kwenye hii clip itakuwa na tija gani kwa mwenye gari au mwenye kusafiri katika njia hii?

Wekezeni kwenye kutoa boriti kwenye macho yenu kabla ya kushadadia vibanzi kwenye macho ya wenzenu kimagumashi magumashi kumbe lengo lenu halisi ni pesa wala si usalama wa raia. Mengine yote kumbe ni machozi ya mamba tu hali kinachotafutwa ni kufikisha malengo ya faini mlizojiwekea ili mkajinufaishe wenyewe binafsi kwa mgongo wa serikali.

Angalia clip hii yenye hali ya ujumla ya barabara hii Benaco Nyakanazi yapata 90km.

Pathetic!
Kwani kuna ndugu zao wanaoitumia hii barabara?
 
Back
Top Bottom