Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,146
- 48,381
David Kafulila a.k.a "Tumbiri" amejipa jukumu la kuwa msemaji wa watawala kuonesha kuwa uchumi wa Tanzania upo Imara na himilivu kuliko hata wale wenye jukumu Hilo.
Kafulila anaongea sana kuhusu Hali ya uchumi wa Tanzania kuliko hata Waziri wa fedha au Gavana wa Benki Kuu ambao ndiyo wenye wajibu huo.
Ushauri wangu kwake ni kwamba siyo kweli kuwa watanzania wanalalamika uchumi wao mbaya kwa sababu hawajui nadharia za uchumi.
Mtanzania anayeshindwa kulipa ada ya shule kwa mtoto wake, anaposhindwa kulipa bili za matibabu yake, anapokosa uwezo wa kununua chakula na kadhalika, huo kwake ni uhalisia wala siyo hisia anazojenga kwa kuwa hajui nadharia za kiuchumi.
Kafulila ajue tu kuwa nadharia zote za kiuchumi ni tafsiri tu ya binadamu kuhusu maisha na zenyewe siyo zinazojenga maisha.
Nadharia za kiuchumi zimewekwa angalau kujaribu kupunguza minyukano ya binadamu kwenye kujipatia mahitaji yao dhidi ya rasirimali zilizopo.
Kwa ivo watanzania wanaposema uchumi wao ni mbaya hawazushi bali ndiyo uhalisia wa maisha yao.
Labda yeye hana utofauti na yule malkia aliyesema "kama hawana mikate si wale keki?".
Kafulila anaongea sana kuhusu Hali ya uchumi wa Tanzania kuliko hata Waziri wa fedha au Gavana wa Benki Kuu ambao ndiyo wenye wajibu huo.
Ushauri wangu kwake ni kwamba siyo kweli kuwa watanzania wanalalamika uchumi wao mbaya kwa sababu hawajui nadharia za uchumi.
Mtanzania anayeshindwa kulipa ada ya shule kwa mtoto wake, anaposhindwa kulipa bili za matibabu yake, anapokosa uwezo wa kununua chakula na kadhalika, huo kwake ni uhalisia wala siyo hisia anazojenga kwa kuwa hajui nadharia za kiuchumi.
Kafulila ajue tu kuwa nadharia zote za kiuchumi ni tafsiri tu ya binadamu kuhusu maisha na zenyewe siyo zinazojenga maisha.
Nadharia za kiuchumi zimewekwa angalau kujaribu kupunguza minyukano ya binadamu kwenye kujipatia mahitaji yao dhidi ya rasirimali zilizopo.
Kwa ivo watanzania wanaposema uchumi wao ni mbaya hawazushi bali ndiyo uhalisia wa maisha yao.
Labda yeye hana utofauti na yule malkia aliyesema "kama hawana mikate si wale keki?".