Ni ukweli ulio wazi kwamba umefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuvuka changamoto ya kuupeleka mziki wako ukubalike nje ya Tanzania
Hivi sasa mpenda muziki yeyote Africa anajua muziki wako na kukufatilia kwa karibu sana
Najua unatengeneza pesa nzuri kuliko msanii yeyote Ea Afica kwa sasa lakini binafsi naona bado hujafanikiwa kutengeneza pesa kulingana na jina lako na muziki ulijitengenezea
Najaribu kuangalia wasanii ambao upo nao level moja angalau kwa sasa wanvyopiga shows all over the Africa
Angalia acc za insta za psquare au davido
Sioni ukipiga matour ya maana ukiachilia kenya uganda tz burundi rwanda
Natamani nikuone unajaza nyomi cameruni au ghana au misri south africa nk
Show za usa na uk zinalipa sawa lakini himaya yako ipo Africa wanakokutambua, wapige hela bana
Hii ni changamoto kwa Fela na team yako yote, tafuteni mapromota wa nchi husika mkapige hela bana
Shows za tz Pekee hazitoshi, andaa tour moja matata Africa, huu ni wakati wako na hauta kaa juu milele
Ni hayo tu
Naamini unakatiza mitaa hii kuchungulia na kama sio wewe basi wapambe wako