Siyo siri kuwa Mwenyekiti wa CDM Mh. Freeman Mbowe ameweza kuongoza chama kwa uweledi mkubwa hasa ukizingatia kwamba chama kina vijana wengi katika uongozi ambao wana mitazamo tofauti na ambao wangependa mambo yafanyike kwa kasi kwa kadri wanavyofikiri. Tunampongeza kwa hilo. Hata hivyo ningependa kutoa ushauri kidogo. Mnaweza kuuchukua au msiuchukue. Ni vizuri kuelewa kwamba watu wanatofautiana ki mtazamo na si lazima au siyo rahisi tukawa na fikra sawa. Ni muhimu basi, kama chama cha demokrasia mkavumiliana au kuheshimu mawazo ambayo ni tofauti na ya kwako. Pia, ningependa kusema kuwa, hakuna mtu ni "perfect". Kila mtu ana madhaifu (weaknesses) na mazuri (strengths) yake. Ni vizuri kulenga kwenye mazuri na kusahau madhaifu, kwa hivyo mtaweza kujenga umoja na chama chenye nguvu. Ninaamini kwamba; kila mtu amekuwa na mchango kwa hapo chama kilipofika. Kwa hivyo basi lenga kwenye mazuri ya kila mtu mtafika mbali. Kama kuna kukosoana ifanyike kwa hekima. Na nina amini viongozi wa juu wa CDM wana hekima kubwa. Hawakurupuki.
Nawaasa vilevile wale walio na mitazamo tofauti. Ni vizuri kila mara mfikie "win -win situation". Badala ya upande mmoja kupoteza ("win - loose situation"). Na kama kila mara wewe utajiona au utajikuta uko tofauti na wenzako kimsimambo, lazima kutakuwa na tatizo. Tafuta njia ya kurekebisha. Mimi naamini mnahitajiana wote na kila mtu ana mchango.
Nawakilisha.
Nawaasa vilevile wale walio na mitazamo tofauti. Ni vizuri kila mara mfikie "win -win situation". Badala ya upande mmoja kupoteza ("win - loose situation"). Na kama kila mara wewe utajiona au utajikuta uko tofauti na wenzako kimsimambo, lazima kutakuwa na tatizo. Tafuta njia ya kurekebisha. Mimi naamini mnahitajiana wote na kila mtu ana mchango.
Nawakilisha.