Samboko
JF-Expert Member
- Oct 30, 2011
- 5,421
- 7,877
Habari zenu wana jamvi.
Kuna mwanamke tuliwahi kuwa wapenzi miaka 8 iliyopita, tulipendana sana kipindi hicho ila alikuja kuolewa na mwanamme mwingine ambae alikua anamtaka tangu tukiwa wote na alifanikiwa kumuoa baada ya wazazi wake kuwa wakali wakimwambia kwanini alikua hataki kuolewa na huyo jamaa maana jamaa alipeleka barua kwao binti alipokataa wakamwambia tunajua upo kwenye mahusiano na mtu fulani kwanini asije kujitambulisha? kama ana nia nzuri nawe?, mama yake alikua anajua natoka na bintie.
Sasa wakati hilo sekeseke likiendelea nkapata safari nikaenda Dom kibiashara sisi tulikua tupo Dar, ilinichukua miezi mitatu kurejea Dar nikakuta demu wangu kishaolewa na jamaa, demu akadai ilibidi akubali baada ya baadhi ya marafiki zangu kumwambia nimeenda kuoa na kipindi hicho si mimi wala yeye aliekua na simu na nilipokua mimi kulikua hamna mawasiliano kabisa ya simu.
Baada ya hapo ikapita miaka minne bila kuonana, siku moja nipo kwa rafiki yangu kuna kazi nilikua naifanya geto kwake, alipokutana na rafiki yangu akamwambia nipo kwake akaja pale kwa rafiki yangu tukawa tunapiga stori za hapa na pale nikajikuta hisia zinapanda juu yake lkn sikumwambia, kumbe nae amekutwa na hali kama yangu akaniambia nimekuona nimeishiwa nguvu kabisa na siwezi kuondoka hivihivi aidha tumalizane hapa kwa rafiki yako au twende gesti, tukajikuta tumevunja amri ya sita palepale.
Ikabidi nimkatie mawasiliano kwa sababu niliona tungeishia pabaya. Ila kila nikimuona nashinkwa na msisimko wa hali ya juu nae ni hivyohivyo.
Kilichonifanya niombe ushauri, wamehamia karibu na ninapoishi na familia yangu na anadai nimekua namkwepa ila sasa hivi amehamia karibu atanifata hadi home kama ntamkimbia tena.
Sio kwamba siwezi kumpotezea ila tunapokutana tuu naishiwa nguvu kama yeye.
Naombeni ushauri wa kufanya ili hali hii isinikute tena maana sipendi kumsaliti mke wangu, maana kila tukionana na huyu mwanamke tunakua na hisia za hali ya juu sana.
Ushauri tafadhali.
Kuna mwanamke tuliwahi kuwa wapenzi miaka 8 iliyopita, tulipendana sana kipindi hicho ila alikuja kuolewa na mwanamme mwingine ambae alikua anamtaka tangu tukiwa wote na alifanikiwa kumuoa baada ya wazazi wake kuwa wakali wakimwambia kwanini alikua hataki kuolewa na huyo jamaa maana jamaa alipeleka barua kwao binti alipokataa wakamwambia tunajua upo kwenye mahusiano na mtu fulani kwanini asije kujitambulisha? kama ana nia nzuri nawe?, mama yake alikua anajua natoka na bintie.
Sasa wakati hilo sekeseke likiendelea nkapata safari nikaenda Dom kibiashara sisi tulikua tupo Dar, ilinichukua miezi mitatu kurejea Dar nikakuta demu wangu kishaolewa na jamaa, demu akadai ilibidi akubali baada ya baadhi ya marafiki zangu kumwambia nimeenda kuoa na kipindi hicho si mimi wala yeye aliekua na simu na nilipokua mimi kulikua hamna mawasiliano kabisa ya simu.
Baada ya hapo ikapita miaka minne bila kuonana, siku moja nipo kwa rafiki yangu kuna kazi nilikua naifanya geto kwake, alipokutana na rafiki yangu akamwambia nipo kwake akaja pale kwa rafiki yangu tukawa tunapiga stori za hapa na pale nikajikuta hisia zinapanda juu yake lkn sikumwambia, kumbe nae amekutwa na hali kama yangu akaniambia nimekuona nimeishiwa nguvu kabisa na siwezi kuondoka hivihivi aidha tumalizane hapa kwa rafiki yako au twende gesti, tukajikuta tumevunja amri ya sita palepale.
Ikabidi nimkatie mawasiliano kwa sababu niliona tungeishia pabaya. Ila kila nikimuona nashinkwa na msisimko wa hali ya juu nae ni hivyohivyo.
Kilichonifanya niombe ushauri, wamehamia karibu na ninapoishi na familia yangu na anadai nimekua namkwepa ila sasa hivi amehamia karibu atanifata hadi home kama ntamkimbia tena.
Sio kwamba siwezi kumpotezea ila tunapokutana tuu naishiwa nguvu kama yeye.
Naombeni ushauri wa kufanya ili hali hii isinikute tena maana sipendi kumsaliti mke wangu, maana kila tukionana na huyu mwanamke tunakua na hisia za hali ya juu sana.
Ushauri tafadhali.