Ushauri tafadhali

white rose

Member
Joined
May 24, 2015
Posts
61
Reaction score
22
Habari ya weekend wapendwa, mm ni mwanamke mwenye umri wa miaka 27 nna mtoto mmoja na mm ni single parent. Nashukuru Mungu nna kazi nzuri inayonilipa vizuri(private sector). Nimejiwekea vijipesa vyangu na sasa angalau nina amount kubwa. Nlikuwa naomba ushauri ndugu zangu, eti nifanye kipi kati ya haya
* ninunue kiwanja nianze kujenga
*ninunue gari nliyokuwa natamani kwa muda mrefu
*nitafute biashara ya kufanya
NB:hyo pesa inatosha kufanya kimoja tu kati ya hivyo

Natanguliza shukrani.
 
Tafuta biashara uendelee kukuza kipato cha kuweza kujenga na badae gari
 
Kwanza hongera sana kwa kuwa na mawazo ya kimaendeleo ni wanawake au wasichana wachache sana wenye fikra pevu kama hizo kabla sijakushauri kufanya kimoja kati ya hivyo ningependa kujua uko mkoa ngani na wilaya gan?
 
Biashara inahitaji usimamizi na time
ukiachia watu hela yako wataila ulie hadi kamasi nje

Nyumba na kiwanja ni idea nzuri sababu ukiwa na nyumba kwa jina
lako utaweza hata kukopa benki ufanya biashara yoyote ile

Gari pia kama unaishi Dar lina umuhimu wake
lakini pia litakuongezea gharama za matumizi....
ingawa linaweza pia kukurahisishia mambo mengi mengine

kazi kwako
 
Jenga tu pindi utakapokua na muda wa kutosha ndio ufanye biashara

ardhi inapanda bei siku baada ya siku tofauti na biashara au gari
 
Kwanza hongera sana kwa kuwa na mawazo ya kimaendeleo ni wanawake au wasichana wachache sana wenye fikra pevu kama hizo kabla sijakushauri kufanya kimoja kati ya hivyo ningependa kujua uko mkoa ngani na wilaya gan?[/QUOT]..... Npo dar es salaam
 
Nunua kiwanja ujenge nyumba.

Biashara Ina uncertainty nyingi sana na haina uhakika. Kwavile umeajiriwa na biashara inahitaji usimamizi, sikushauri kuingiza pesa yako huko kwanza.

Nyumba ni asset ya maana zaidi. Ukijenga unakua na uhakika zaidi.... Biashara utafanya tu
 
Kuna mtu tu na akili zake za Ijumaa, atakuja hapa akushauri uolewe. We subiri tu.
 
Naomba kutia neno. Sijui una sh ngapi hasa! Lakini nakupa haya maneno, na assume una si chini ya 5mln!

1. Nunua kiwanja walau kidogo hata kama kipo mbele ya chanika mbelembele huko just 20x20 almost sio zaidi ya 2mln. I can help kama utaridhia!

2. Achana na gari kwa sasa, lakini weka balance walau sh 1mln akiba kwa ajili ya gari. Usidharau

3. Anzisha biashara ndogo tu walau usidharau kuishia kupata sh 10,000 kwa siku kama faida. Kama hili litakushinda mtafute best yako unaelewana naye vema then team up muongeze nguvu ya mtaji na usimamizi. Hakikisha ana business mentali kama mimi!

Baada ya miaka 3 njoo mtafute UNDENIABLE kwa ajili ya kumtunuku shukrani!

NB:
Chukua hii jioni ya leo!

1. Never rely on one source of income, Never!
2. Dont forget number 1
 
Last edited by a moderator:
 
Bado akijenga nyumba na akakopa pesa ya biashara kama hakuna muda wa kuisimamia bado italiwa na nyumba itakua mashakani.
 
Kama hauna nyumba, anza na nyumba. Mengine baada ya nyumba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…