Ushauri please

MKAMUAJI

New Member
Joined
Mar 24, 2014
Posts
2
Reaction score
0
Ninaishi na mwanamke ambaye nimezaa naye mtoto mmoja ila hatujafunga ndoa.

Home kwetu wanamfahamu, kwao pia wananifahamu.

Kiukwel kwa sasa nimefall sana kwa mwanamke mwingine ambaye ndiye hasa natamani awe mke wangu wa ndoa.

Tatizo linakuja, huyu wa pili ni dini tofauti na mm japo yu tayari hata nikafunge naye ndoa ya Kiserikali, japokuwa na yeye anawasiwasi kama wazazi wake watalikubali hilo kwani wameishika dini yao kweli kweli.

Huyu wa home naye kila kukicha ananiuliza vp ndoa, nampiga calendar.

Yule mwingine kanipa Go ahead niende kwao natest ali kama wazee wake watakubali.

Nimeshidwa kwenda sijui nitaanzia wapi kumuacha huyu ninayeishi naye.

Kwa mawazo yangu, hata kma nitafunga ndoa na huyu ninayeishi naye, nitamcheat siku zote a maisha yangu sababu ninayempenda ndo hivyo kuna vikwazo kati yetu.

Nifanyeje wandugu?
 
usishtuke, kila mtu kapitia hiyo stage, muoe uliyenae , endelea kuiba kwa unayempenda, usirogwe kuoa unayempenda, utakufa kwa presha
 
sa kwanini ulimzalisha kama humpendi..! watu wengine bhana.... haya mambo sijui yataisha lini
 
Kweli unampenda huyo mwingine?
Kwa sababu u can move heaven and earth..destroy families and relationships. Hurt souls and hearts. Break hopes and reasons to believe in goodness of men.
Mwisho wa siku unakuta it was just a spur of the moment, na yeye humpendi kihivyo and u'll cheat on her too.
Hebu kaa chini ujiulize is that what u want?
Kumbuka hata huyo unayeishi naye ulimpenda. Tena kwa sababu nyie ndo mnaonana kila siku na bado anataka umuoe unakuja kujua she is the only one who has even gave all up for u. Who truly love u. Kwenye hii dunia iliyojaa utapeli it really is important kuishi na someone u can count on. Hata kama upendo umeshuka, are u sure u have done everything u could to save ur relationship? ama ulikuwa busy kwa huyo mwingine?
Do u know hata ukiwa na huyo bado usipoulea upendo utaisha pia?

Kaka mkubwa mwisho wa siku utakuja gundua haya mambo bana unaangalia unayeweza kuishi naye. Love is choice. Hata walio ndoani kuna kipindi upendo hushuka. Haina maana ndoa ndo imeisha.
 
Acha uzinzi. Acha kuharibu future yako. Acha kutafuta umaskini kwa lazima. Acha kumharibia binti wa watu na mtoto uliyepata future yao. Huwezi jua huyo mtoto atakuja kua nani badae. Acha mawazo na tamaa zisizokua na maana.

Hilo ni pepo la ngono linakusumbua.

#Ushauri wangu wa kawaida; Komaa na huyo uliyezaa nae.....funga nae ndoa. Kua karibu na familia yako. Mpende mkeo na mtoto wako. Hakikisha unajengea mazingira mazuri...amani na furaha vitawale.


#Ushauri wa kiroho: Kuwa karibu na Mungu, kemea kabisa hilo pepo la ngono; Hakikisha unaongea na mwenzi wako mama mtoto wako. Tubu kwa dhambi chafu uliyoifanya.
-Funga ndoa nae; Hapo ndipo utaona baraka katika familia yako.



#Angalisho : Achana kabisa na huyo ambae hujazaanae. Atakuharibia maisha. Utajuta sana. Na itakua too late.

Wanawake wazuri wapo kila siku. Acha tamaa na epuka uzinzi. Huyo mama watoto wako usimdharau...ndio Mungu kakupa huyo.
 
Wanaume bwana,umemzalisha then unaishi nae kabisa unataka kumuacha umfate mwingine,chozi atakalolia huyo dada mwenye mtoto wako ni la thaman sana na for sure,nakwambia litakucost kwenye maisha yako na huyo wa nje,usiteme bigjii kwa karanga za kuonjeshwa kaka utakwenda na maji.baki na huyo mwenye mtoto na umuoe kama unampenda sana huyo wa nje cheat naye lakin huyo wa ndani asijue,wanaume mnaumiza sana umeshamwaribia muelekeo wa maisha kwa kuzaa kabla ya ndoa,umeshamtumia utakavyo then unataka umdump kisa mwingne,na utalaaniwa na Mungu kwa ujinga,unyanyasaji na unyama unataka kuufanya!plz kaka angu nataman hata nipate wasaa wakuzungumza na wew usifanye unachotaka kufanya.
 
acha tama kijana ,na huyo wa sasa ukishamzoea utaanza kumtamani wa tatu...hizo ni tama za kimwili tu bwana mdogo ...kama unaona wa kwanza hana mvuto mboboreshe ..
 
Kumbe unaendekeza michepuko. hahhahahaah...... utakufa ndg yangu.

hapo hakuna unaempenda.

In short:

huyo mpya ni kwa sababu hajazaa ila akishakuzalia nae pia utamuoana mzee utatafuta watatu. Huyo watatu ukimzalisha utatafuta wanne .........................................ukija kuzinduka una watoto ishirini na maisha haya magumu.

Muoe huyu uliezaanae mulee huyo mjukuu wangu, na huyo wa pembeni kwakuwa umeshamuonja na umeshaongeza idadi ya chupi ulizozivua achananae kiistaraabu.

Michepuko sio dili baki njia kuu.
 
Ulianzaje kuanza kuishi nae kama humpendi? tena mpaka mkazaa, ndo haya niliyosema kwenye ile thread ya come we stay sina hakika sana kama nimepatia jina la thread ila kibongo bongo usijaribu wengi wao mwisho huwa ndo huu. we umeamua tu kuchepuka basi sema kinachokupa jeuri ni kwmba hujafunga ndoa na huyo mwanamke kwahiyo unajiona uko free kumfanyia lolote
 
KARMA IS REALLY A BI.TCH! Mtu kajizalilisha kukuganda mpaka kuingia labor kwa ajili yako all for nothing!
 
Bako njia kuu....huko unapoenda utaumia.
 
Kwanini mnaziona hisia za wenzenu kama vile kitu kisichokuwa na thamani?

Kwanini hamzithamini hisia za wenzenu?

Mnaziona kama inyesi tu eehhh????

Watu kama nyie hamfai kabisa

Namuonea huruma huyo dada wa watu

Kila uchao anakupikia kukufulia akijua wewe ni mume mwema kwake kumbe kila ukitembea mimacho imekutoka kwa wanawake wengine huku ukidhani ni sawa

Hata huyo unaedai unampenda wala humpendi na kama akijua na akajua kuwa kuna mwanamke mwingine anapigwa chini lazima nae atakimbia kama anafikiria vyema!
 

nimeipenda sana
 
Hicho ni kitu cha kawaida kutokea kwa wanaume walio katika mahusiano, yaani kuna mda unakuta unaona kama ulie nae humpendi na unampenda mngine, that is the lie.

Ndugu your a man of mission and direction not intmacy.

Usifanye hisia za mapenzi ziharibu misheni zako aisee, just let it go mkuu.


Ulie nae anakuamini asilimia zote na anakupenda/anakukubali mwanzo mwisho.

Ukija kumuacha huyo ulie nae ataumia na atazoea tu (nnaimani anauwezo huo) ila utapata tatizo kwa huyo utakae mfuata maana atakudharau kwa sababu atakuana wewe ni mwanamume usie na maamuzi sahihi juu yako mwenyewe, na unajua ni nini kitafuata?

Baada ya hapo ataanza kutoa amri ndani ya nyumba na hauta kuwa na sauti kwake, na utaishi maisha ya kujilaumu mwanzo mwisho.



Mkuu let it go, muoe huyo ulie nae utaishi kwa amani na uhuru maisha yako yote.
 
Pole ndugu,
Sikiliza moyo wako unakutuma nini. Usijeoa mke kisa ana mimba yako ama ana mtoto wako. Hutaishi kwa raha maisha yako yote, Hebu fikiria upendo wa kweli unatoka moyoni, Mimi nakushauri ufanye kile moyo kinachokutuma asee. Huyo mdada ilikuaje hata ndoa bado akajiozesha mwenyewe? Asee pole yake.
 
Eti mrsleo Hebu niambie inakuaje mdada mpaka unahamia kwa mwanaume hali yakua hata ndoa hujafunga naye? Halafu na mimba unabeba. Hivi inakuaje?
 
Last edited by a moderator:
Muoe aliokuona wa thaman mpk akakuzalia mtoto, thn ebu tuekee picha kwanza
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…