KATASAN'KAZA
JF-Expert Member
- Jul 24, 2013
- 3,097
- 1,356
- Thread starter
-
- #21
Huyu member mwenzetu Avemaria ndiyo muhusika uliyeahidi utamtaja jina?
Ok! Hamna uhusiano wa SCD na kusema uongo.
Vijitu viongo viongo hata kwa mambo madogo madogo huwa havifai kamwe , hutakaa uwe na furaha.
Kuhusu kujiua hiyo haipo.
Avemaria huyu ajui chaka hili la jf siyo mfuasi ata kidogo.
Nimekupata mkuu!
Nilidhani na wewe utakuwa miongoni mwa waliopotoka.
Jamani mwenzenu niko njia panda,yapata Mwaka sasa niko kwenye mahusiano na mdada fulani jina nitasema badae, jamani nampenda sana nae pia kiukweli ananipenda mno si kidogo, ila sasa amekuwa na tabia fulani ya kusema uongo wa vitu vidogo vidogo mfano amaweza kuwa yuko nyumbani akadanganya yuko kwenye Daladala huku unasikia mazingira yanaonesha siyo kwenye Gari ila yapo matukio mengi anakuwa anadanya ila ukimbana kidogo anakueleza ukweli na kuomba msamaha.
Shida imeanza leo baada ya kuwa amedanganya kaenda mahali afu akawa amerudi Nyumbani nilipompigia Simu kaanza uongo wake mara nipo kwenye Daladala sasa shisa ni kwamba mazingira ya kwao nayaelewa sana, nikaa nambishia baada ya kama dakika tatu za mabishano akaadimit na kukubali yupo home na kumuuliza anafanya hivyo akadai hana jibu.
Kwakweli nilichukia nikaamua kumtolea uvivu nilimpa masharti kadhaa na ili ayalidhi moja ilikuwa aniambie sababu ya kuwa muongo kwa vitu vya kijinga. Baada ya kuona yamekuwa makubwa akaamua kufunguka na sababu zake ni hizi:
1) Kwanza ili mchukua muda ila mwisho kasema kwa huzuni sana kuwa yeye ni mgonjwa( Sickle cell), unamfanya apende kudanganya ili kwasababu watu wa namna hii wanatabia ya kuogopa kutokubaliwa au kutojiamini muda wote.
2) Sababu ya pili kasema huwa ajui anachosema kama kitanikwaza sana, kwahiyo yeye anavyona hakuna tatizo, mimi nachukia.
Sasa waungwana wanajamvi embu nielezeni kuna uhusiano kati ya kuongopa na Sickle cell? Pili hii habari imenichanganya sana, nawaza nimwache maana huu ugonjwa ni mkubwa na si wakiza kimoja na pia nimesoma kwenye mtandao matunzo ya mtu wa sickle cell ni ghali sana! lakini hata muda wake wa kuishi ni akibahatika kuvuka 18 ni limit 50yrs.
Hapa nilipo nimechanganyikiwa sijui ata nifanyeje yeye kwasasa yupo 21, kama kuna mtu uelewa nisaidieni ameniambia hii siri baada yakuwa amelia sana. Na amevunja agano la mama yake alimwambia asije mweleza mtu ambaye ajui hili tatizo naona hofu ya mama yake ni kwamba mwanae atakosa mwanaume wa kumuoa na kanitishia nikimwacha anakunywa sumu. Nimeanza naye mapenzi alikuwa bado ajajua mwanaume nampenda Avemaria nifanyaje.
Hofu yako kubwa ni kwamba huyo bibie atafariki mapema wala sio suala la uongo.Kuhusu suala la ukimuacha atakunywa sumu, na wewe mwambie AKIKUDANGANYA utakunywa sumu.
Hahahah umenichekesha kweli wewe dah!!!
Kwahiyo ningekuwa ndo mimi jamaa angekuwa kakosea njia? LOL
kwi kwi kwi kwi kwi kwi
Hayo ndo yanaitwa mahaba ntie ngwala ning'oe meno ya barazani
Acha uoga kijana wanawake wako wengi kama vumbi la dhahabu geita
Mwambie unaachana naye halafu sikilizia baada ya wiki na nusu then call her uone kama hujaisikia sauti yake
Anayetaka kujiua hasemi ugali mtamu jamani!
Uongo siyo mzuri. Mtu muongo ni wa kumuogopa sana, inaonekana na bado kuna vingi sana anakudanganya. Ana mambo yake tu huyo, siku ukija kumfumania atkuambie alikuwa anakudanganya tu.
Kwanza, .sickle cell haingiiliani na uongo wake. Kuna dada nafanya nae kazi hapa ni good performer at work ana cheo cha umeneja wa kuaminika, Postgraduate na ni mama wa watoto 3 ila siku ikimbana ndo utamwonea huruma ni ICU kwenda mbele. Sasa angekuwa anatumia huo ugonjwa wake kama ni excuse sidhani kama angefika that far...ugonjwa ni mindset yake tu.
Pili, nahisi matatizo yanaweza kuwa kwako, wewe waonyesha kutokumwamini. Maana unapenda kumuuliza uko wapi kila mara, labda anakujua tabia yako na mazingira aliyopo unaweza ukakasika ndio anaishia kukudanganya. Acha kumuuliza uko wapi everyone now and then...labda you're controling freak!
Tatu, mtu mwenye Sickle cell anaweza kuolewa na kuzaa watoto salama, nendeni mkapime genetic zenu. Huyo dada nilioleza hapo juu mumewe sio sickler na ameweza kuwa na family ambayo haina maradhi. Shughuli jitaarishe na kuuguza when needed, na kama unampango wa family kubwa sidhani kama litawezekana kwa hawa watu.
mmmh labda nakushauri ukasikilize ule wimbo wa ambwene mwasongwe kwanza wa upendo then ndio urudi.Mungu anauwezo wakufanya pale ambapo hata sisi hatufikirii kama inawezekana.mwasongwe aliimba yule kijana alimpenda yule dada akiwa kichaa na Mungu alimponya yule dada ili yule kaka asiaibike na upendo wake.sasa unafikir mungu hawez mponya mtu mwenye siko cel?????pale kwenye mapungufu upendo ndio hupimwa.
Mimi nafikiri unatumia vibaya neno "Nakupenda", kama kweli una maanisha basi huo ugonjwa wake wala isingekuwa tatizo.
Wasiwasi wangu ni kwamba huenda hata hilo swala la yeye kuumwa sickle cell kakudanganya.
Ningekushauri hapo ulipotaja jina Avemaria ungeweka angalizo kwamba sio huyu wa jamvini.Licha ya kuwa umefafanua kwenye comment ila kuna wataoishia kusoma maada tu na kuconclude kuwa ni mimi au pengine anaweza asipaone hapo ulipokanusha maana si wote husoma kila comment.Bila shaka avemaria mwingine...!
Ningekushauri hapo ulipotaja jina Avemaria ungeweka angalizo kwamba sio huyu wa jamvini.Licha ya kuwa umefafanua kwenye comment ila kuna wataoishia kusoma maada tu na kuconclude kuwa ni mimi au pengine anaweza asipaone hapo ulipokanusha maana si wote husoma kila comment.