Ushauri: Nimeshindwa kumsahau dada huyu

Ushauri: Nimeshindwa kumsahau dada huyu

vnn

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2015
Posts
3,030
Reaction score
7,497
Wakuu,

Kuna msichana nimetokea kumpenda yani kumpenda kweli kweli sio utani,
kama ni kuteka hisia basi yeye kateka asilimia 80 ya hisia zangu na nilipanga awe wangu wa maisha, dada huyu nasoma nae college moja na mda si mrefu tunagraduate lakini huyu dada yeye hayuko tayari kua na mimi na ameshanitamkia kabisa ila akili yangu imeshndwa kumsahau kabisa, kila nikikaa namuwaza yeye, nikimuona hata na wavlana wengine ndo kabisa moyo unaniumaa sana.Nimeshndwa nifanyeje.

Naombeni ushauri wenu maana akili yangu imeshindwa kumsahau!
 
mmmmmmmmm,hatari unaempenda hakupendi na amekwambia hakupendi lakini still unampenda,je uko tayari akudanganye akuchune au bora kakwambia ukweli utaumia lakini utasahau?
 
dah mkuu ye mwenyewe kanambia nivumilie2 maana hakuna namna awezi kua nami
 
wakuu

kuna msichana nimetokea kumpenda yani kumpenda kweli kweli sio utani!
kama ni kuteka hisia basi yeye kateka asilimia 80 ya hisia zangu na nilipanga awe wangu wa maisha

dada huyu nasoma nae college moja na mda si mrefu tunagraduate

lakini huyu dada yeye hayuko tayari kua na mimi na ameshanitamkia kabisa
ila akili yangu imeshndwa kumsahau kabisa, kila nikikaa namuwaza yeye,nikimuona hata na wavlana wengne ndo kabisaa moyo unaniumaa sanaa

nimeshndwa nifanyeje, naombeni ushauri wenu maana akili yangu imeshndwa kumsahau!
fanya haraka tafuta ubavu wako kabla haujanywewa supu, kwann unganganie
 
Dont force love brother. Just let love come to you. Kama hakupendi brother dont force it. Nilikuwa kwenye situation kama yako.. nikiwa chuo. Lakin baadae nilijifunza kuukubali ukweli. Sawa inauma kwa sababu moyo umependa.. lakin mwache aende. Usipoteze muda
 
Acha kupoteza muda, yupo wa kwako aliyetoka ubavuni mwako utaletewa. Ni suala la muda tu.
 
Unashindwaje kumsahau MTU ambaye hajawahi kukupa nafasi moyoni mwake?? Be strong...Fanya mambo yako.
 
Acha mambo yako tafuta wako, huyo atajileta mwenyewe baadae na wewe umwambie nafasi yake haipo
 
Usiwaze kijana, ukimaliza chuo mtatengana kwahiyo hutamwona tena na itakua dozi nzuri ya kumsahau
 
Una upendo sana kijana..endelea kujikondesha na mtu ambae hakuhusu..
 
Tena amekufanyia wema kumwambia hakuitaji kuliko angekudanganya na kukulia visenti vyako..
 
Dah me binafsi dem akishanitamkia kuwa hanipendi/ haniitaji huwa nampotezea kuanzia mda huo so nashangaa wewe unakuwa naujasiri gani kumpenda, kumuwaza acyekupenda acyekuhitaji ?
 
Back
Top Bottom