Ushauri: Mwanaume wake kabadilika hana muda nae

Ushauri: Mwanaume wake kabadilika hana muda nae

morning

Member
Joined
Sep 21, 2016
Posts
8
Reaction score
4
Kuna rafiki yangu yupo katika mahusiano takribani miaka 4 sahivi, na toka waanze uhusiano na huyo kaka, walipendana sana yani na huyo rafiki yangu siyo mtu mwenye tamaa ya hela kitu ambacho wasichana wengi wa siku hizi wanaangalia sana.

Alikuwa anamsaidia huyo kaka hata akiwa na shida ya hela lakini siku hizi huyo rafiki yake wa kiume ameonekana kubadilika sana kwani hata akipiga simu atamwambia subiri halafu hampigii tena au hata wakiwa wanaongea kwenye simu anamkatia bila sababu na wala hasemi na hamtafuti. Akimtumia sms hazijibiwi yaani ameonekana kubadilika tofauti na alivokuwa mwanzo.

Ameniomba ushauri afanyaje nami nimeona ni vema nilete uzi huu kwenu wana JF tumsaidie ushauri huyu rafiki yangu maana binti anampenda sana na ndugu zake huyo kaka wanamfahamu na wanampenda sana huyo dada ila huyo kaka ndo tatizo afanyaje?.

Karibuni sana.
 
Huyo mtu atakua kapata mwngne ukimwona mwanaume amebadilika ujue hapo kuna mwngne, cha kufanya ajitahid kupigania hayo mahusiano yake mpka pale atakapoona ameshindwa kabsa zen ajitahid kuachana nae, sio rahis ila itabd ajitahid tuu, siku huyo mtu akiona umuhim wake atarud, asipo rud bas mungu hajapanga wawe wote
 
Kwa ushauri mzuri..kwa kuwa honest kabisa, huyo kapata mtoto wa kike mwingine. Sasa huwa vinatokea na asipoangalia they can end up in a bad break up. Ajiandae kisaikolojia kwamba anytime it could end. Then, aanze maandaliz ya Ku nurse a wound. Jamaa atamfanyia vituko lakini at the end atakuja kukubali there is no love between the two anymore. Hiyo relationship haina future tena. Truly, the Lady should be prepared to grow through what she will go through very soon.

Sent from my TECNO P5 using JamiiForums mobile app
 
Hapo hana chake tena.

Kupunguza maumivu mwambie amtamkie jamaa kwamba "IT'S OVER!!" kabla ye hajaambiwa. That way yeye ndo atakuwa amemuacha huyo mwanaume na hiyo itamsaidia kufanya maumivu yawe kidogo kuliko akipewa taarifa ya kuachwa yeye. Na huyo mwanaume itamuuma maana kawahiwa kuachwa na hatojua anaachwa kwasababu gani..hivyo itamtatiza sana.
 
kapata muongaji mzuri zaidi yake .. ampige chini atafute mwanaume anayejua kutunza mwanamke
 
Kuna rafiki yangu yupo katika mahusiano takriban miaka 4 sahivi, na toka waanze uhusiano na huyo kaka, walipendana sanaaa yaani na huyo rafik yangu siyo mtu mwenye tamaa ya hela kitu ambacho wasichana wengi wa siku hizi wanaangalia sana.

Alikuwa anamsaidia huyo kaka hata akiwa na shida ya hela lakini siku hizi huyo rafiki yake wa kiume ameonekana kubadilika sana kwani hata akipiga simu atamwambia subiri halafu hampigii tena au hata wakiwa wanaongea kwenye simu anamkatia bila sababu na wala hasemi na hamtafuti. Akimtumia sms hazijibiwi yaani ameonekana kubadilika tofauti na alivokuwa mwanzo.

Ameniomba ushauri afanyaje nami nmeona ni vema nilete uzi huu kwenu wana JF tumsaidie ushauri huyu rafiki yangu maana binti anampenda sana na ndugu zake huyo kaka wanamfahamu na wanampenda sana huyo dada ila huyo kaka ndo tatizo afanyaje.

Karibuni sana.
Mdada, mpe pole yake, hicho kinacho mpata mm nina true story yake, rafiki yangu kabisa true best frd, alikuwa na msichana, huyo mdada si haba mambo safi, wameenda kipindi kirefu mpka yule dada akaamua kumsimesha best angu chuo furani cha ualim

Mdada alikuwa anatoa service zote unazozijua za kijamii kwa ndugu na jamaa wa hyo best angu, kunasiku nlikuwa nataka kwenda kumuona hyo best chuon, yule mdada alinitoa mkoa wangu(dar)mpaka musoma alikokuwa anasoma best wangu,

Nlipofika nkamkuta yupo na mrembo mwingine, nlipo muuliza y, akaniambia yule anae tu ila hamfurahii,

To short a story, dada aliachwa na jamaa sasa anamke mwingine, nlichojifunza ni kuwa ukimuona mkaka anaanza mabadiliko na kama ulikuwa unatoa service kuwa makini maana hakika utaachwa tu, havutiwi nawe ila anavutiwa na pesa,

Mwambie ajiandae kisaikolojia ndo amekwisha achwa hivyo, hakina namna...
 
Hao wahongaj wazur wanapatkana wap na mi nkatafute jaman[emoji13]
Nenda new Africa hotel utawakuta kibao siku za alhamis kwene live band... ila kiukwel wahongaj wamekimbia sku izi mana sio kwa hali ngum hii mkuu
 
Hapo hana chake, kuishi kwenye mahusiano miaka minne ni kipaji maalum
 
Yaan nlimwonea huruma sana kwani anampenda sana lkn ndo hvo
 
Dalili ya mvua ni mawingu.
Ajiandae tu pschologially mana siku si nyingi ataujua ukweli.
 
Kuna watu wanakuwa na bahati lkn wanashndwa kuitumia wakat wenzio wanatafuta
 
Back
Top Bottom