Ushauri Mchumba Mkurya Mbabe

Sema tu ni wewe mkuu tukushauri. Iko hivi unachokiona kwa shemeji habahatshi, ndivyo wakurya walivyo. Aina yao ya mazungumzo unaweza sema anakufokea au anakulazimisha, ila hapana ndio walivyo na ndivyo wanavyolelewa.

Sasa iko hivi, kama huo ubabe ni ule tu wa kikurya huo wala hauna shida, ni jambo la kumzoea tu na kusonga. Ila kama ana ka ubabe ka tabia binafsi ambako sio ka kikabila ambako angeweza kuwa nako mwanamke wa kabila lingine tukasema hafai basi huyo pia hafai. Ila kama kale ka ubabe ka kabila lao hako hakana shida ndivyo walivyo mkuu.

Nawaelewa sana wakurya. Ni moja ya makabila machache yalitobaki tz ukipata mwanamke una enjoy kwa sababu ya tamaduni zao, hawanaga kudeka hao eti umemtolea mahari halafu aanze kusema nina kwetu nirudishe waala.

Zingatia niliyokuambia mkuu, mchunguze kwenye hizo pande mbili ukigundua ni ule ubabe wa asili yao tu, oa huyo mke mkuu, utakuja kunishukuru.
 
kiongozi asante kwa ushauri
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…