Ushauri, maoni yenu wanajamvi

Ushauri, maoni yenu wanajamvi

McNair

Senior Member
Joined
Mar 18, 2017
Posts
182
Reaction score
130
Salaam

Niende moja kwa moja kwenye mada

Wakuu naomba kujuzwa

Iv ni mambo gani au vitu gani unashauriwa kumfanyia au kumpa demu ambaye unaenda kukutana naye kwa mra ya kwanza kwa muda ambao mtaweza kupiga stories na kuzungumza mambo mkiwa wawili kwa muda wakutosha?

Nimeuliza hivo sababu huyu demu nilikutana naye njiani nikampenda kwa sababu tofauti tofauti nikaomba namba zake akanikubalia kunipa baada ya wiki moja hivi nilipopata muda baada ya shughuli zangu za hapa na pale nilimuibukia kumtongoza na akanikubali. Ila sasa mpaka muda huo nilikuwa nishaanza kumsahau alivyo ambapo na yeye alisema hivo kwamba hanikimbuki nilivo ashaanza kunisahau hivyo tukaahidiana tutenge muda na tufanye tukio la kukutana tena ili kutazamana upya na kufahamiana, kupiga stories zaidi na kufurai pamoja.

Hivyo basi tunatarajia kukutana na ninajiuliza nimwandalia mapochopocho gani ili maongezi yetu yanoge? Nimpelekee zawadi ya namna gani? Etc.

Nawasilisha...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah.... Mbona unaonekana mgeni sana ...

Uko Shule!!?
 
Kiukweli ningekushauri kama ningeona upo serious ila kwa post yako wewe beba condom tu..wewe na yeye akili zenu zinawaza sawa!

Walau usituongee watoto wasiotarajiwa kisha mkawakana!
 
Kama uko Dar, zama Mwenge pale ukamnunulie raba moja au moka moja saafi. Pia mfungie vitu vya kutafuna tafuna kama chocolate, biscuts za eat some more n.k... Pia kabla hamjakutana mchek kwenye simu umtumie elfu ishirini ya kukodi bajaji. Mkikutana itakuwa ni bashasha mwanzo, mwisho...
 
Kama uko Dar, zama Mwenge pale ukamnunulie raba moja au moka moja saafi. Pia mfungie vitu vya kutafuna tafuna kama chocolate, biscuts za eat some more n.k... Pia kabla hamjakutana mchek kwenye simu umtumie elfu ishirini ya kukodi bajaji. Mkikutana itakuwa ni bashasha mwanzo, mwisho...
Asee tukutane basi next week
 
Kama uko Dar, zama Mwenge pale ukamnunulie raba moja au moka moja saafi. Pia mfungie vitu vya kutafuna tafuna kama chocolate, biscuts za eat some more n.k... Pia kabla hamjakutana mchek kwenye simu umtumie elfu ishirini ya kukodi bajaji. Mkikutana itakuwa ni bashasha mwanzo, mwisho...
Hahahaa...
Asisahau na apple..lol
 
Back
Top Bottom