Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,638
Nilipohamishiwa kanda ya ziwa kikazi toka Dar. nilimtafuta dalali ili anisaidie kunitafutia nyumba, kweli alipata nyumba ya mama mmoja hivi ambaye kiutamaduni ni mtani wangu na yeye ananiita mtani.
Sasa kwanza hana mume, mumewe alifariki mwaka jana mwezi wa 4 na ana watoto wakubwa tu wengine wapo vyuoni na mmoja anafanya kazi Dar.
Toka mwezi huu uanze ameanza kunionyeshea tabia fulani fulani, kila nikitoka kazini anakuja ndani mwangu anakaa na wakati mwingine kumbe anakuja amefunga kanga tu.
Jana nimetoka kazini nikapita Hotelini kula nikakaa hadi saa 2 usiku nimerudi home aliposikia nafungua mpango tu huyo akaja na chakula nikamwambia nimeshiba nishakula, akanilazimisha kuwa chukua ule, nikapokea nikakiweka mezani then akakaa, akaniambia niwashe TV nikawasha.
Nikaenda kuoga kurudi naingia chumbani na yeye huyo kafika akaniambia ngoja nikupake mafuta nikasema hapana sipaki mafuta usiku, aiseee si akakaa kitandani!! kumbe hakuwa na nguo ya ndani akabenua kanga mapaja hayo nje nje kweli nilipata mfadhaiko muda huo nikamwambia naenda sebuleni kuangalia kipindi fulani hivi cha ITV-KIPIMA JOTO, Akasema njoo kwanza nikarudi akaanza kunishika shika masikioni, nikamwambia nooo!!
Sipo tayari akauliza kwa nini? Nikamwambia leo sijisikii kufanya hicho unachotaka, akaniuliza ina maana mmii mbaya? Nikasema hapana ila leo sina hamu kabisa ki ukweli nilikuwa na hamu sana ila nikimwangalia huyu mama ni mtu mzima sana ni above 50 na mimi mwenyewe ndo nipo above 21 nikasema hapana.
Akaniambia njoo angalau mara moja tu tux nikampa moyo kuwa subiri kesho yaani leo. Sasa ndugu zangu leo nitamdanganyaje tena?
Huyu mama sitaki kutembea nae n coz ni kama mama yangu, pia, watoto wake japo wapo hostel chuoni kwao hapa hapa nahofia wakija jua kuwa namuondomola mama yao na tunaheshimiana sana.
wazo la kuhama limenijia usiku wa leo sana.
USHAURI WENU TAFADHALI