Ushauri kwa wana CCM wenzangu

Chaser

Member
Jul 6, 2011
23
3
Ndugu zangu, kidumu chama chetu! Nawapa pole kwa kazi ngumu, tunayoifanya bila kusinzia, kupeleka ujumbe kwa kueleza mazuri na mema ya Serikali yetu. Kazi hii haijawa na haitakuwa rahisi hata kidogo kwani wakati huohuo pia tunawajibika kuimarisha chama na kukipa nguvu zaidi. Ndiposa nawaandikia ujumbe huu nikiwa safarini Meatu, safari ambayo itanirudisha mpaka Ruvu ili kujenga Chama. Wana CCM wenzangu, kila mmoja kwa umoja wake, naomba sana ili kuonekana hatujazidiwa nguvu na JF. Basi kila mmoja afungue ID angalau 5 kwa majina tofauti. Hii njia, japo yaonekana nyepesi na ya kitoto, itasaidia sana kupunguza makali yao na pia tutafanya hoja zao zisiwe na mvuto kwa kuzipinga kwa nguvu zote. Kwa wingi wetu hakika tutashinda. Mungu ibariki CCM
 
Sawa mkuu,hiyo mbona tunaifahamu siku nyingi tuu..............si kama kuleee..........eti eeh?Ilitusaidia sana hasa kwenye majimbo yaliyokuwa yameshikiliwa na Wasema Kweli..........:pound:.....:pound:.......:pound:

Sasa mkuu.......,unaonaje kila mtendaji akapewa kijicomputer chenye mtandao.....:typing: ,jenereta ya kuzalisha umeme na vocha ili wanakijiji waweze kuhamasika?.............................au umelenga wa mjini tu..........tutawaweza kweli hawa mkuu?...........................Bora huko ambako ndio wanaanza kutoka usingizini..........au unasemaje mkuu?

Aaaah................nilitaka kusahau mkuu...........................nadhani mngeandaa na tshirt/kofia/khanga za chama.....na kifuta jasho(si unajua ofisi zetu hazina AC mkuu?),ili kila anayekuja kubofya asitoke bure.............teh teh teh...:dance::dance::dance:.............si unawajua tena?.........watajaa kama nzi kwenye MZOGA!

.............samahani mkuu,si unajua mdomo tena..............najua.............najua...... HAKIJAFA......hata mimi niliwahi kupelekwa ICU:sick:.....................lakini nilipona mkuu.....................

Ni hayo tu mkuu,KIDUMU!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom