Chaser
Member
- Jul 6, 2011
- 23
- 3
Ndugu zangu, kidumu chama chetu! Nawapa pole kwa kazi ngumu, tunayoifanya bila kusinzia, kupeleka ujumbe kwa kueleza mazuri na mema ya Serikali yetu. Kazi hii haijawa na haitakuwa rahisi hata kidogo kwani wakati huohuo pia tunawajibika kuimarisha chama na kukipa nguvu zaidi. Ndiposa nawaandikia ujumbe huu nikiwa safarini Meatu, safari ambayo itanirudisha mpaka Ruvu ili kujenga Chama. Wana CCM wenzangu, kila mmoja kwa umoja wake, naomba sana ili kuonekana hatujazidiwa nguvu na JF. Basi kila mmoja afungue ID angalau 5 kwa majina tofauti. Hii njia, japo yaonekana nyepesi na ya kitoto, itasaidia sana kupunguza makali yao na pia tutafanya hoja zao zisiwe na mvuto kwa kuzipinga kwa nguvu zote. Kwa wingi wetu hakika tutashinda. Mungu ibariki CCM