USHAURI KWA WALIMU ...

USHAURI KWA WALIMU ...

Tutor B

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2011
Posts
9,025
Reaction score
6,614
Huu ni ushauri kwa walimu ...

Namna gani unaweza utumia UALIMU wako kuongeza kipato na kubadilisha maisha yako?

Kama mko sehemu moja mnafanya kazi jiungeni kikundi kulingana na masomo kwa mfano kuwe na mwalimu PHYSCIS, MATHEMATICS, CHEMISTRY.

Muwe mnafundisha O-LEVEL & A-LEVEL , fundisheni kwa kujirekodi video na ku upload youtube(Nikisema m burn kwenye cd itakuwa gharama sana).

Mnaweza mkajichanga kwa pamoja na kununua camera ya kurekodi vipind. Tafuteni mtaalam wa camera na video editing mnakuwa mnamlipa kwa kuchangishana kama group.
Mkifanya hivyo ndani ya mwaka mmoja kwa muda wa ziada jmos na jpili , nawa hakikishia ajira lazima mtawachia wengine. Mkitaka mfanikiwe zaidi fanya haya yafuatayo ;
1. Vuta wateja au viewers kupitia instagram kwa kupost video ya training fupi.
2. Fungua akaunti youtube na kuweka nembo yako ili watu watape kuwajua kama ndo nyingi wa instagram.
3. Tengeneza video kama series na kila epside isizidi 15min. Chukulia kila topic ni season 1. Hakikisha ni HD/4K
4. Weka matangazo ya GOOGLE Ads kupata pesa ya watu kuangalia video.
5. Tenga kipind cha kusolve past paper za necta( Practical Only). Kama mtaweza kukodi LAB kwa ajiri ya practical ya chemistry na biology.
6. Tengeneza tshirt zenu muwe mnavaa mara nyingi mkiwa kwenye mkusanyiko watu au maeneo ya shule
7. Muwe mnatoa maswali na atakaye jibu na kupata A , anapewa tshirt .
Au jaribu kuongea na walimu mkuu wa shule mbalimbali muwe mnapeleka mithian yenu kwa lengo la kushindanisha na kutoa zawadi. Ila usisahau kusema
"Lengo letu ni kukuza elimu na kupunguza ZERO nchi nzima"-Slogan
8. Tengenezeni tshirt yenye slogan ambayo itagusa fikra za watu wengi especially walimu wakuu pamoja na waziri wa elimu kwa ujumla.
9. Panga ratiba baada ya kuongea na walimu wakuu wa shule mbalimbali kuhusu mashindano ya mitihani lenu kwa wanafunzi wao.
10. Dili na shule zenye wanafunzi wengi(O-level & A-level), ili kuwe na impact kubwa kwenye channel yenu ya youtube.
11. Nyinyi vaeni form6 badala ya tshirt ili msionekane wahuni. Maana mavazi yana mata sana kwenye AGREEMENT au PRESENTATION. Kokote unapoenda husisahau kuvaa form 6 lenye nembo.

Kwa ushauri zaidi waweza kunipata kwa kutuma e-mail kwenye anuani hii ... jnb14enterprises@gmail.com

12. Mkiona youtube kwenu miyeyusho tengenezeni ANDROID APP.
"Thinking is hardest discipline of ALL"
 
Ushauri mzuri kabisa. Asante sana.
 
Good advice buddy.
Kazi kwao waalim kuichangamkia hiyo fursa japokuwa ina changamoto kubwa mno kulungana na kwamba watoto wa O- level na A-level ni vigum kufika YouTube na Instagram. Labda ukigonga matirio ya chuo hapo sawa
 
Good advice buddy.
Kazi kwao waalim kuichangamkia hiyo fursa japokuwa ina changamoto kubwa mno kulungana na kwamba watoto wa O- level na A-level ni vigum kufika YouTube na Instagram. Labda ukigonga matirio ya chuo hapo sawa
A-level wengi wana start phone mkuu.
 
Fursa ya walimu ni kuanzisha shule tu , munaungana walimu 10 wamasomo tofauti munaanzisha munachanga mtaji kwa walimu 10 let say 500,000/= kilamoja ni 5MiL munaanzisha centre yakufundisha, then ikikuwa kubwa munaandaa proposal wawezeshaji kibao tu naamini ukimfata mtu kama Late Mengi, Mo nk na slogan zenu za kukuza elimu mzee hachomoi, mwisho wasiku munamiliki shule yenu.

Niamini mimi hakuna nyanja rahisi kuwezeshwa endapo mushajiwezesha kama education.

Mimi mwalimu nitalifanya tu hili.
 
Fursa ya walimu ni kuanzisha shule tu , munaungana walimu 10 wamasomo tofauti munaanzisha munachanga mtaji kwa walimu 10 let say 500,000/= kilamoja ni 5MiL munaanzisha centre yakufundisha, then ikikuwa kubwa munaandaa proposal wawezeshaji kibao tu naamini ukimfata mtu kama Late Mengi, Mo nk na slogan zenu za kukuza elimu mzee hachomoi, mwisho wasiku munamiliki shule yenu.

Niamini mimi hakuna nyanja rahisi kuwezeshwa endapo mushajiwezesha kama education.

Mimi mwalimu nitalifanya tu hili.
Mkuu hilo wazo lako ninalo kitambo sana. Sema tu kila nikiongea wa graduates wanachomoa yaan wananiona kamasipo serious
 
Mkuu hilo wazo lako ninalo kitambo sana. Sema tu kila nikiongea wa graduates wanachomoa yaan wananiona kamasipo serious
Haha hili linawaitaji wajasiriamli na Risk takers tu wenye malengo makubwa ila graduates hawa wakutaka upenyo wa ajira.
 
ushauri mzuri ila ukianza kuweka tutorials youtube,utakuwa hutafutwi...watu wanauliza maswali humo humo…………LOL……..

Labda,mtu awafungulie website,walimu wajiandikishe na masomo wanayofundiisha then wanafunzi wachague wanamtaka mwalimu gani,atoe availability yake...then wafundishane ………
 
ni wazo zuri sana. changamoto kubwa ni kwamba walimu wengi (sio wote) bado hawajawa tayari ku take risk. wengi bado waoga na wanaamini sana katika kuajiriwa kuliko kujiajiri. kingine walimu wengi wanatanguza hila na wivu wa wenzao wanaofanikiwa badala ya kujifunza badala ya kutumia mafanikio hayo kama fursa. wakuu wengi wa shule wanawakataza hadi watoto kwenda tuition centre kisa matokeo yanapotoka vizuri anayesifiwa ni mwenye tuition centre na sio mkuu wa shule husika. hilo wataliweza?
 
Fursa ya walimu ni kuanzisha shule tu , munaungana walimu 10 wamasomo tofauti munaanzisha munachanga mtaji kwa walimu 10 let say 500,000/= kilamoja ni 5MiL munaanzisha centre yakufundisha, then ikikuwa kubwa munaandaa proposal wawezeshaji kibao tu naamini ukimfata mtu kama Late Mengi, Mo nk na slogan zenu za kukuza elimu mzee hachomoi, mwisho wasiku munamiliki shule yenu.

Niamini mimi hakuna nyanja rahisi kuwezeshwa endapo mushajiwezesha kama education.

Mimi mwalimu nitalifanya tu hili.

Wazo lako zuri ila wazo la mtoa mada lipo byee sana kwani limekaa kisasa sana hata ukiwa na shule yako bado lipo valid
 
Huu ni ushauri kwa walimu ...

Namna gani unaweza utumia UALIMU wako kuongeza kipato na kubadilisha maisha yako?

Kama mko sehemu moja mnafanya kazi jiungeni kikundi kulingana na masomo kwa mfano kuwe na mwalimu PHYSCIS, MATHEMATICS, CHEMISTRY.

Muwe mnafundisha O-LEVEL & A-LEVEL , fundisheni kwa kujirekodi video na ku upload youtube(Nikisema m burn kwenye cd itakuwa gharama sana).

Mnaweza mkajichanga kwa pamoja na kununua camera ya kurekodi vipind. Tafuteni mtaalam wa camera na video editing mnakuwa mnamlipa kwa kuchangishana kama group.
Mkifanya hivyo ndani ya mwaka mmoja kwa muda wa ziada jmos na jpili , nawa hakikishia ajira lazima mtawachia wengine. Mkitaka mfanikiwe zaidi fanya haya yafuatayo ;
1. Vuta wateja au viewers kupitia instagram kwa kupost video ya training fupi.
2. Fungua akaunti youtube na kuweka nembo yako ili watu watape kuwajua kama ndo nyingi wa instagram.
3. Tengeneza video kama series na kila epside isizidi 15min. Chukulia kila topic ni season 1. Hakikisha ni HD/4K
4. Weka matangazo ya GOOGLE Ads kupata pesa ya watu kuangalia video.
5. Tenga kipind cha kusolve past paper za necta( Practical Only). Kama mtaweza kukodi LAB kwa ajiri ya practical ya chemistry na biology.
6. Tengeneza tshirt zenu muwe mnavaa mara nyingi mkiwa kwenye mkusanyiko watu au maeneo ya shule
7. Muwe mnatoa maswali na atakaye jibu na kupata A , anapewa tshirt .
Au jaribu kuongea na walimu mkuu wa shule mbalimbali muwe mnapeleka mithian yenu kwa lengo la kushindanisha na kutoa zawadi. Ila usisahau kusema
"Lengo letu ni kukuza elimu na kupunguza ZERO nchi nzima"-Slogan
8. Tengenezeni tshirt yenye slogan ambayo itagusa fikra za watu wengi especially walimu wakuu pamoja na waziri wa elimu kwa ujumla.
9. Panga ratiba baada ya kuongea na walimu wakuu wa shule mbalimbali kuhusu mashindano ya mitihani lenu kwa wanafunzi wao.
10. Dili na shule zenye wanafunzi wengi(O-level & A-level), ili kuwe na impact kubwa kwenye channel yenu ya youtube.
11. Nyinyi vaeni form6 badala ya tshirt ili msionekane wahuni. Maana mavazi yana mata sana kwenye AGREEMENT au PRESENTATION. Kokote unapoenda husisahau kuvaa form 6 lenye nembo.

Kwa ushauri zaidi waweza kunipata kwa kutuma e-mail kwenye anuani hii ... jnb14enterprises@gmail.com

12. Mkiona youtube kwenu miyeyusho tengenezeni ANDROID APP.
"Thinking is hardest discipline of ALL"
Wakumbuke kabla ya kuappload video YouTube ni lazima kusajili TCRA na kulipia kwanza. Tofauti na hapo utasombwa mahakamani kama walivyofanya kwa MC pilipili
Option ya kuandaa Android Apps ni nzuri zaidi endapo utapata mtaalamu
 
Ni wazo zuri la kijasiliamali kwa wajasiliamali. Vinginevyo tutaishia kudai nyongeza na kupandishwa madaraja
 
Kampun yako yakuprint t-shirt na kutengeneza website bei gan
 
Fursa ya walimu ni kuanzisha shule tu , munaungana walimu 10 wamasomo tofauti munaanzisha munachanga mtaji kwa walimu 10 let say 500,000/= kilamoja ni 5MiL munaanzisha centre yakufundisha, then ikikuwa kubwa munaandaa proposal wawezeshaji kibao tu naamini ukimfata mtu kama Late Mengi, Mo nk na slogan zenu za kukuza elimu mzee hachomoi, mwisho wasiku munamiliki shule yenu.

Niamini mimi hakuna nyanja rahisi kuwezeshwa endapo mushajiwezesha kama education.

Mimi mwalimu nitalifanya tu hili.
Hapo kwenye bold ndo kuna mtihani mkuu. Walimu wengi wanapenda kuajiliwa ili walipwe mshahara hata wasipofanya kazi.

Hapa nina centre ina madarasa makubwa matatu, ofisi, mbao za kufundishia pamoja na viti. Walimu wanaokuja kwa ajili ya kuanzisha centre swali lao la kwanza ni mshahara. Sasa niwapangieje mshahara wakati hata wanafunzi hawajakuwepo? Wao wanataka mimi ni-take risk ya kuwalipa kabla hawajafanya kazi. Ikumbukwe kwamba sisi kama taasisi tulishatake risk ya kujenga hayo majengo, kuweka miundo mbinu ya umeme na maji n.k
 
Mkuu hilo wazo lako ninalo kitambo sana. Sema tu kila nikiongea wa graduates wanachomoa yaan wananiona kamasipo serious
Hawawazi nje ya box.

Komaa ipo siku ndoto yako itapevuka mkuu.
 
Back
Top Bottom