Ushauri kwa wabunge wa CHADEMA

Ushauri kwa wabunge wa CHADEMA

PAMBANA

Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
73
Reaction score
21
Naomba nianze kwa kusema hakuna aliyemkamilifu chini ya jua na siku zote mtu mwenye hekima anapotambua mwenyewe kuwa amekosea au kuonyeshwa na mtu mwingine kosa hujirekebisha na kisha kusonga mbele. Wabunge wangu wa CHADEMA inaonekana ninyi ndio hamtumii vizuri kanuni za Bunge.Tunafahamu kuna propaganda za wabunge wa CCM zinazorushwa kwenu na saa nyingine lugha za maudhi lakini mimi binafsi nawaomba na kuwashauri mtumie vizuri kanuni za bunge na mahali inastahili kutumika mnapotaka kujibu hoja za wenzenu wa CCM.Kwa mfano ktk kikao cha leo Mbunge wa Iringa mjini alionekana kutumia kanuni isivyo alipokuwa akitoa taarifa yake (badala ya kutumia kanuni ya kutoa taarifa alitoa kanuni ya kuomba mwongozo).Tunaomba msifanye vitu ambavyo vitawaondolea heshima yenu kwa wananchi ambao wanawaamini. Pia nafahamu mna kuna mambo ya kuwaudhi humo bungeni wakati vikao vinapokuwa vinaendelea kama kejeli na mambo mengine mengi na saa hamuwezi kukaa kimya na ni vizuri kuwajibu, binafsi nawashauri mjikite kwenye mambo ya kuwatetea wananchi na mambo yanayoleta maendeleo kwa taifa letu. Mwisho nawatakia kazi njema mnayoifanya hapo bungeni.
 
TUMEPOKEA USHAURI WAKO,HATA SISI UNATUGUSA SANA,TUNAUPITIA TUTAUFANYIA UPEMBUZI YAKINIFU IKIBIDI TUTAUNDA TUME KUUCHUNGUZA HALAFU LIWALO NA LIWE LAZIMA MWISHO WA SIKU UDHAIFU UTACHUKUa MKONDO WAKE
 
ukiomba mwongozo haupewi nafasi, ukisema huu sio utaratibu hausikilizi wala kupewa nafasi, inabidi mbunge wa chadema ajifanye ana taarifa kumbe ni mwongozo au huu sio utaratibu ili mradi tu apate nafasi, kwa taarifa yako wabunge wa chadema wanalazimika kutumia kanuni zisizo ilimraadi wapate nafasi, ccm hata wakikohoa tu makinda anaitikia akidhani wameomba mwongozo. dawa ya moto ni moto, wabunge wangu endeleeni kutumia kila njia kuwanyosha hawa magamba
 
Sikutegemea kama lengo lango ni kutoa ushauri wa matumizi ya kanuni ndugu yangu, hawa wabunge wa CHADEMA wanasimamia mambo makubwa sana kwa niaba ya watanzania, wanasimamia maslahi ya watu wa Mwanza,Mara,Kagera,Kigoma,Shinyanga.Tabora,Singida,Geita,Simiyu,Arusha,Kilimanjaro, Dalesalama, Tanga.Lindi,Mtwara.Iringa,Mbeya.Songea,Unguja na Pemba.

wanafanya hivyo huku wakitambua kwamba maeneo hayo mengine yanawawakilishi waliochaguliwa na wananchi kuwapigania kutoka vyama vingine, ni bahati mbaya sana kwamba wamefika bungeni na kuanza biashara zingine, katika mazingira kama haya bado unataka kuifanya issue ya kukosea kanuni kuwa issue kweli kweli?
 
Wabunge wa Chadema pia ni binadamu, wanakutana na maudhi mengi sana, na wanafanywa kama watoto wa kambo... nawasifu sana kwa kuweza kuvumilia upuuzi wa hali ya juu ambao kwa utu wa kawaida hauvumiliki. nwakubali sana hawa makanda!
 
Simbachawene amepona mkono alioumia kule Singida?viongozi wa Mjengoni(wanaoliendesha) ni Dhaifu
 
nakubaliana na micho mnayotoa na nilikuwa sifahamu kama saa nyingine inawalazimu kufanya hivyo maana wanapoomba miongozo, utaratibu na taarifa hawapewi nafasi.
 
kwa hali iliyosasa hata Spika anasema anatumia kanuni za Bunge Lakini ukweli ni huu kuwa hata mtu yeyote anajua kuwa kuna upedeleo wa wazi kuhusu utendaji wa spika na Wenyeviti wake.
Mbunge wa Sikonge alisema kuwa " mwenye uchungu akazae" aliyasema haya huku akichangia bajeti kila mytu anajua mbunge huyu hakuwa anachangia suala la Afya lakini Naibu Spika akasema si tusi wala si kosa.
Jana Mwenyekiti anapombwa mwongozo kwa kanuni yeye anatoa mwongozo kuwa Tundu Lisu anataka umaarufu
Baadaye anamtukana Mnyika kuwa "anawashwa" huyu ni mtu anayeonekana kuwa mzee wa kuaminika ndani ya CCM na kwa taifa anatumia misemo ya mateja mitaani.
Wabunge wetu endeleeni kusimamia hoja mjikaze ili kuepusha hasira katika haya mazingira WANANCHI TUNAONA,TUNASIKIA,TUNAJUA na sasa tumeshatoa hukumu ambayo munaiona katika mikutano yenu kwa imani inayooneshwa na WANANCHI juu yenu.
 
Naomba nianze kwa kusema hakuna aliyemkamilifu chini ya jua na siku zote mtu mwenye hekima anapotambua mwenyewe kuwa amekosea au kuonyeshwa na mtu mwingine kosa hujirekebisha na kisha kusonga mbele. Wabunge wangu wa CHADEMA inaonekana ninyi ndio hamtumii vizuri kanuni za Bunge.Tunafahamu kuna propaganda za wabunge wa CCM zinazorushwa kwenu na saa nyingine lugha za maudhi lakini mimi binafsi nawaomba na kuwashauri mtumie vizuri kanuni za bunge na mahali inastahili kutumika mnapotaka kujibu hoja za wenzenu wa CCM.Kwa mfano ktk kikao cha leo Mbunge wa Iringa mjini alionekana kutumia kanuni isivyo alipokuwa akitoa taarifa yake (badala ya kutumia kanuni ya kutoa taarifa alitoa kanuni ya kuomba mwongozo).Tunaomba msifanye vitu ambavyo vitawaondolea heshima yenu kwa wananchi ambao wanawaamini. Pia nafahamu mna kuna mambo ya kuwaudhi humo bungeni wakati vikao vinapokuwa vinaendelea kama kejeli na mambo mengine mengi na saa hamuwezi kukaa kimya na ni vizuri kuwajibu, binafsi nawashauri mjikite kwenye mambo ya kuwatetea wananchi na mambo yanayoleta maendeleo kwa taifa letu. Mwisho nawatakia kazi njema mnayoifanya hapo bungeni.

Ujumbe umefika najua wabunge wetu wataufanyia kazi kwani ni waelewa sana na ni watu makini!
 
Wabunge wa CDM pamoja na uchache wao wanastahili pongezi kwa kuwawakilisha wananchi wa Tanzania nzima. Kwani wabunge wa magamba wanakiwakilisha chama chao tu na wamewatelekeza wananchi waliowachagua na kuwatuma bungeni.
 
Naomba nianze kwa kusema hakuna aliyemkamilifu chini ya jua na siku zote mtu mwenye hekima anapotambua mwenyewe kuwa amekosea au kuonyeshwa na mtu mwingine kosa hujirekebisha na kisha kusonga mbele. Wabunge wangu wa CHADEMA inaonekana ninyi ndio hamtumii vizuri kanuni za Bunge.Tunafahamu kuna propaganda za wabunge wa CCM zinazorushwa kwenu na saa nyingine lugha za maudhi lakini mimi binafsi nawaomba na kuwashauri mtumie vizuri kanuni za bunge na mahali inastahili kutumika mnapotaka kujibu hoja za wenzenu wa CCM.Kwa mfano ktk kikao cha leo Mbunge wa Iringa mjini alionekana kutumia kanuni isivyo alipokuwa akitoa taarifa yake (badala ya kutumia kanuni ya kutoa taarifa alitoa kanuni ya kuomba mwongozo).Tunaomba msifanye vitu ambavyo vitawaondolea heshima yenu kwa wananchi ambao wanawaamini. Pia nafahamu mna kuna mambo ya kuwaudhi humo bungeni wakati vikao vinapokuwa vinaendelea kama kejeli na mambo mengine mengi na saa hamuwezi kukaa kimya na ni vizuri kuwajibu, binafsi nawashauri mjikite kwenye mambo ya kuwatetea wananchi na mambo yanayoleta maendeleo kwa taifa letu. Mwisho nawatakia kazi njema mnayoifanya hapo bungeni.

Ni kweli mkuu,lakini tambua kuwa kanuni zinakuwa zinaheshimika pale znapotumika ipasavyo bila kumkandamiza mtu!
 
Hakika yule mwenyekiti wa kikao cha jana jioni hasitahili hata kuongoza familia yake binafsi licha ya kupewa nafsasi ya kuonekana mjengoni.
Baada ya kuharibu mwishoni anajikosha o- wabunge naomba tutumie kanuni. Shame on you gamba!!!
 
wabunge wote should grow up and discuss issues kama watu wazima, do you realise even your own kids and grand kids watch you guys shouting at each other on the telly...its disgusting to say the least
 
kwa hali iliyosasa hata Spika anasema anatumia kanuni za Bunge Lakini ukweli ni huu kuwa hata mtu yeyote anajua kuwa kuna upedeleo wa wazi kuhusu utendaji wa spika na Wenyeviti wake.
Mbunge wa Sikonge alisema kuwa " mwenye uchungu akazae" aliyasema haya huku akichangia bajeti kila mytu anajua mbunge huyu hakuwa anachangia suala la Afya lakini Naibu Spika akasema si tusi wala si kosa.
Jana Mwenyekiti anapombwa mwongozo kwa kanuni yeye anatoa mwongozo kuwa Tundu Lisu anataka umaarufu
Baadaye anamtukana Mnyika kuwa "anawashwa" huyu ni mtu anayeonekana kuwa mzee wa kuaminika ndani ya CCM na kwa taifa anatumia misemo ya mateja mitaani.
Wabunge wetu endeleeni kusimamia hoja mjikaze ili kuepusha hasira katika haya mazingira WANANCHI TUNAONA,TUNASIKIA,TUNAJUA na sasa tumeshatoa hukumu ambayo munaiona katika mikutano yenu kwa imani inayooneshwa na WANANCHI juu yenu.

nakuunga mkono mkuu ,upo sahihi
 
Back
Top Bottom