Ushauri kwa maafisa tawala wa mikoa (RAS)

Ushauri kwa maafisa tawala wa mikoa (RAS)

Joined
Jul 24, 2015
Posts
80
Reaction score
38
Napenda kutoa Ushauri kwa Maafisa Tawala wa Mikoa (RAS)

(1) Ni vyema Maafisa Tawala wa Mikoa (RAS) wakafanya kazi kwa karibu sana na wakuu wao wa mikoa kwa kuwashauri.

(2) RAS watumie vilivyo weledi wao katika mambo yanayohusikana na utaratibu za kisheria ama urasimu wa kiserikali (They need to use their expertise/skills on issues that needs legal expertise and government bureaucracy)

Naamini RAS wana ufahamu mkubwa wa masuala ya kiutawala (Public and Corporate Governance) anaweza tumia weledi wa kuwasaidia wakuu wao wa mikoa ambao uteuzi wao ni wa Kisiasa na hauhitaji vigezo vya kielimu.

La sivyo ma-RAS watajikuta matatani kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao. Na Rais hata waonea huruma atawatumbua tu.
 
Hao wakuu wa mikoa wenyewe wanasikiliza ushauri wa Maras? Hapo ndo kizunguzungu kinapoanzia, wakuu wa mikoa kwa sasa wapo busy na Media ili waonekane wanafanya kazi hata kama hakuna wanalofanya. Huoni mwingine anaamrisha bank impe waliokuwa wanapokea fedha za watumishi hewa? Jiulize kwa hilo suala dogo namna hiyo RAS alihusishwa japo kutoa ushauri tuu?
 
Hao Wakuu wa Mikoa ni wanasiasa na qualification zao hazieleweki, na hawapendi hasa kupata kwanza ushauri wanakurupuka tu. hawa ni wajumbe wa siasa wa mikoa wa chama wanafanya siasa full. mfano ulotoa ni mmoja angalia mwingine juzi tu huko Bunda mkuu wa mkoa tulisikia eti kamsimamisha mhandisi eti mradi wa umwagiliaji hautumiki ipasavyo sasa hapo mtaona hakusikiliza au kupata ushauri , nimesikia engineer yule ana mwaka mmoja jazini hata hajaidhinishwa kazini na mradi umejengwa tokea 2008 sasa hapo engineer anaingiaje na wanaohusika kutoa elimu ya kutumia mradi syo engineer bali ni maafisa wa maendeleo ya jamii na maafika kilimo na ugani. Kweli Katiba mpya muhimu sana kuangalia upya vyeo hivi.
 
Hao wakuu wa mikoa wenyewe wanasikiliza ushauri wa Maras? Hapo ndo kizunguzungu kinapoanzia, wakuu wa mikoa kwa sasa wapo busy na Media ili waonekane wanafanya kazi hata kama hakuna wanalofanya. Huoni mwingine anaamrisha bank impe waliokuwa wanapokea fedha za watumishi hewa? Jiulize kwa hilo suala dogo namna hiyo RAS alihusishwa japo kutoa ushauri tuu?
Pamoja na tamko la RC kwa mabenki bado RAS ndiyo mwenye wajibu wa kutekeleza kwa vitendo tamko la RC kwa kuandika barua kwa wahusika Takukuru na hlHazina, hapo ndipo RAS atumie weledi wake awasiliane na TAKUKURU na HAZINA hizo taasisi ndiyo zitawasiliana na BOT na COMMERCIAL BANKS. ma-RAS wasiwe waoga wafanye kazi.
 
Back
Top Bottom