ushauri kwa kina dada kuhusu ndoa !

Johnsecond

JF-Expert Member
May 4, 2010
1,076
211
Ili kuimarisha ndoa, kutokuelewana is part of it maana ni pale unaweza kuona reaction za mwenzako na pale ndipo ukweli husemwa na kila mmoja hubaki akiufikiria baada ya kutoelewana. Cha msingi usiongee sana wakati wa kutoelewana hata kama linataka kutoka kubwaaa lizuie kwa nguvu zooote na jifanye huoni maana baada ya ugomvi kila mtu huwa anarudia kila mstari tokea course mpaka usuluhisho. Kwa mwanamke usijibu nyamaza maana baada ya ugomvi mwanaume akianza kurudia atakuonea huruma pale akifika mwisho maana ataona kakuonea, kwa mume kama mkeo ni muongeaji sana we ishia home uje baadae maana atakufanya uongee usiyotarajia.

karibuni
 
Hahaaaaa umenikumbusha zamani nilishawahi kuhudhuria kitchen party moja bi arusi akawa anaambiwa mume ni babako rafiki yaani wamtania huku ukimheshimu na kama alivyo baba mzazi siku akichukia na kuanza kusema usifungue mdomo msikilize ............na hata kama kartika kusema kwake hacra zile zikampelekea ku-blow the wind..(cjui ni hasira za aina gani hizi) basi usikunje uso wala kuziba pua......mckilize akishamaliza basi we nenda zako nje hilo funda la mate ulilolikusanywa wakati wasikiza perfume ya wind wake libwage chini Pwhaaaaaaaaaaaaa.

Mwenzangu ni kweli kunyamaza kunasaidia ila pia inategemea na mtu...ukimkuta mwenye gubu mydia.....ukisema atakwambia una jeuri unamjibu wakati anakusema, ukinyamaza atasema unamdharau kwa kuwa anayoyasema kwako hayana maana.......mbona utakuwa nalo!!

Mimi nadhani kunyamaza tu haitoshi (hasa kwa wale wenye wenzi ambao wana magubu), we ukiona mwenzio kawaka kimbilia tena kwa speed kubwa kumwomba msamaha hata kama hukukosa wewe ...... then after kucool down mkalishe taratibu na kumweleza kilichojiri na jinsi ulivyoumia.
 
Ni ushauri wa kweli sana ila usikae kimya tu utaonekana unadharau ila jibu huku ukiomba yaishe yaani msamaha, na mume usiondoke tu atajua kuwa umemdharau mwambie kuwa mje muongee badae then ndo utoke. thanks
 
kimya ni busara but sometimes ni dharau. people are different. its better to talk. kuongea ni bora zaidi ya kukaa kimya ili mradi muongee kwa vituo na heshima bila kuundermine position ya yoyote pale ndani kwenu. kama jazba ya mmoja wenu iko juu sana, ni vizuri yule ambaye bado anajicontrol atake lead to reconciliation, aseme samahani (hata kama haoni kosa alilotenda) na ahakikishe anampoza mwenzie hadi anashusha temper na baada ya siku mbili hivi amuombe kwa upole amsikilize halafu atoe utetezi aliokuwa amepanga kuutoa siku ile, akimuelewa wayazungumze inside out kwa vituo, its done. kama bado ana hasia aombe tena msamaha... arudie process hiyohiyo hadi wameelewana, au ikishindikana a-give up na kumkabidhi Mungu mzigo huo kila siku na kuiombea nyumba yake bila kuuchoka. ieleweke hapa kuwa mashindano nyumbani yawe mwiko kabisa.. huu nao ni ushauri tu ila mbinu nzuri inategemea situation itakavyokuwa na ni lazima imshirikishe Mungu na itawaliwe na hofu ya Mungu
 
Ni kweli kabisa, kukaa kimya ni busara, kwa kawaida huwezi kuongea kwa vituo kama mnagombana coz yale siyo mazungumzo ule ni mtafaruku. Sasa ukiweza kunyamaza na kumsubiri mwezi wako apunguze hasira ndipo muongee kwa vituo hiyo ndiyo wanasema busara
 
dah kweli
asanten kwa kitchen party...minilizan suluhisho mkigombana hm ni kuapply u francis cheka..manundu yakiwa ya kutosha uson bas heshma itachukia mkondo wake...(jokes)
..:car:
 
Back
Top Bottom