Ushauri kwa Kamishna wa uhamiaji

Ushauri kwa Kamishna wa uhamiaji

bategereza

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2013
Posts
3,314
Reaction score
1,072
Ndugu kamishna naomba kwa heshima na taadhima requirements za kupatiwa passport ziwekwe wazi kwenye ile fomu ya maombi na hata katika ofisi zote za uhamiaji. watendaji wako wannaomba vitu vya ziada ilimradi tu wamtoe mtu upepo. nijuavyo mie tunatakiwa kuambatanisha. cheti cha kuzaliwa changu. cha baba na cha mama na barua ya mjumbe soke serkali za mitaa pamoja na barua ya mdhamini. cha ajabu utamkuta ofisa anaomba pasport ya babako. benki akaunti card na benki statement pamoja na cheti cha ndoa na leseni ya biashara. wengine huomba matokeo ya mtihano kwa wanaosomea nje. hivi viambatanisho vinavyotakiwa no vipi. Nitawataja maofisa wako kama utataka majina yao na vituo vyao vya kazo. Nawasilisha
 
Kuna ofisa mmoja wa ngazi ya chini pale mambo ya ndani (Dar) anaitwa SWEDI yuko dirisha la nne upande wa kulia ukiingia. huyu mmulikeni. Alimuomba binti mmoja matokeo yake ya mitihani waqt kila kiambatanisho kilikua kipo.
watu wa uhamiaji hawajagundua kua pasipoti ni haki ya mtanzania. pale utaona wasomali hata wasiojua kiswahili wanahudumiwa chap chap waqt mwenye haki yake anaombwa benki account.
 
Back
Top Bottom