Dangire
JF-Expert Member
- Oct 5, 2011
- 221
- 68
hatimaye ccm kimeamua kupita kusawazisha nyayo za chama cha ukombozi ( kama ilivyo kawaida yao tangu wawe maji ya shingo). kuna msemo usemao "deal with your character, not reputation". inachojaribu kukifanya ccm ni kujisafisha kwa kusema 'mimi ni msafi', ilhali kila mtu anauona uchafu wao;'mimi ni makini', ilhali uzumbukuku wao u dhahiri; 'chama ni imara' wakati udhaifu wao unaonekana. na 'sisi ni wachapakazi' wakati ni dhaifu kupindukia.
hii haijawahi kuwa 'permanent solution' mahali popote, hata kidogo. wataalam wa 'PR' -mahusiano ya uma, wanafahamu kuwa, njia sahihi ya kupata na kuimarisha image ya kampuni sio kuongea hovyo kwa kujibu kila hoja za upande wa pili huku ukiwa hakuna improvement yoyote unayoifanya. bali kusahihisha yale yanayosemwa ili public ijenge imani na kampuni/bidhaa zako.
ccm, kwa kutumia rasilimali nyingi -pesa, muda, nk. kujibu hoja zenye mashiko za chadema, ambazo wananchi zimewagusa, mni kupoteza muda na rasilimali zingine. matokeo yake hayatakuwa kama chama kinavyofikira. unasema hali ya uchumi imeimarika, huku wananchi hawaoni mabadiliko, unategemea nini hapo?
cha kufanya:
1. ccm iache mara moja program yao ya kufanya mikutano eti ili kuelimisha uma kile serikali inakifanya! serikali ni zaidi ya taasisi, kila inachokifanya wananchi wanakiona. huhitaji kuwaambia.mf. kama serikali imejenga barabara, shule 'zenye ubora', hospitali nzuri 'zenye dawa na wataalam', nk. huhitaji kuwaambia eti tumefanya sisi! they are visible 2 everyone, my goodness!
2. ikishaacha kufanya mikutano yake, ianze sasa kutekeleza kwa vitendo yale yote waliyoahidi tangu uchaguzi mkuu wa 2005, 'maisha bora kwa KILA mtanzania'. wakifanikiwa hilo, wananchi wataona, na hivyo imani itarejea.
NB;# wananchi hawahitaji ahadi mpya, ama kuaminishwa juu ya dhahania fulani.wanahitaji kuona na kuguswa kwa dhati na matokeo ya wanachokiona (hasa kwa watz wa leo).
# changamoto kubwa iliyoko mbeleni ni, je ccm itaweza kuleta mabadiliko yale wananchi wanayataka -kiuchumi, siasa, sayansi, na utamaduni? je si sharti kwamba mfumo uliopo (ikiwemo chama) ubadilishwe ili kufikia mapinduzi ya kweli?
hii haijawahi kuwa 'permanent solution' mahali popote, hata kidogo. wataalam wa 'PR' -mahusiano ya uma, wanafahamu kuwa, njia sahihi ya kupata na kuimarisha image ya kampuni sio kuongea hovyo kwa kujibu kila hoja za upande wa pili huku ukiwa hakuna improvement yoyote unayoifanya. bali kusahihisha yale yanayosemwa ili public ijenge imani na kampuni/bidhaa zako.
ccm, kwa kutumia rasilimali nyingi -pesa, muda, nk. kujibu hoja zenye mashiko za chadema, ambazo wananchi zimewagusa, mni kupoteza muda na rasilimali zingine. matokeo yake hayatakuwa kama chama kinavyofikira. unasema hali ya uchumi imeimarika, huku wananchi hawaoni mabadiliko, unategemea nini hapo?
cha kufanya:
1. ccm iache mara moja program yao ya kufanya mikutano eti ili kuelimisha uma kile serikali inakifanya! serikali ni zaidi ya taasisi, kila inachokifanya wananchi wanakiona. huhitaji kuwaambia.mf. kama serikali imejenga barabara, shule 'zenye ubora', hospitali nzuri 'zenye dawa na wataalam', nk. huhitaji kuwaambia eti tumefanya sisi! they are visible 2 everyone, my goodness!
2. ikishaacha kufanya mikutano yake, ianze sasa kutekeleza kwa vitendo yale yote waliyoahidi tangu uchaguzi mkuu wa 2005, 'maisha bora kwa KILA mtanzania'. wakifanikiwa hilo, wananchi wataona, na hivyo imani itarejea.
NB;# wananchi hawahitaji ahadi mpya, ama kuaminishwa juu ya dhahania fulani.wanahitaji kuona na kuguswa kwa dhati na matokeo ya wanachokiona (hasa kwa watz wa leo).
# changamoto kubwa iliyoko mbeleni ni, je ccm itaweza kuleta mabadiliko yale wananchi wanayataka -kiuchumi, siasa, sayansi, na utamaduni? je si sharti kwamba mfumo uliopo (ikiwemo chama) ubadilishwe ili kufikia mapinduzi ya kweli?