Napenda kutoa ushauri kwa CHADEMA waache kujibizana na mamluki wa CCM hasa Prof Lipumba na Mbatia. Huu ni ujanja uliosukwa ili kuanzisha malumbano na vyama hivi maslahi ili kuitoa CDM kwenye mstari. Hawa jamaa wamesha poteza mwelekeo na kiukweli tangu zamani hawa si wapinzani kazi yao walionayo sasa ni kuharibia wale wanaopendwa na kuungwa mkono na wananchi. Prof Lipumba ni msomi mzuri ila kwa sasa yupo kimaslahi zaidi. Mbatia yeye ni kazi yake tangu zamani kubomoa vyama kwa kudandia hoja asizo zijua kwa ufadhili wa CCM.