Ushauri kuhusu changamoto ninazopitia

Happy happy

Member
Joined
Jul 3, 2023
Posts
13
Reaction score
19
Wana JF habari,
Hivi kuna anayepitia changamoto kama ninazopitia? Dah kuna muda natamani nipige kelele kwa ninayopitia labda nitapunguza machungu. Kazini changamoto, nikirudi nyumbani nako changamoto, mahusiano changamoto. Nahisi kichwa kizito jamani, sijui hata niwaelezaje labda mtanielewa.
 

KATAA NDOA
 
Haujasema changamoto gani sasa watakushauri nini
 
hujazitaja ni changamoto zipi.
 
eleza changamoto uliyonayo watu tunapitia makubwa huwezi jua utapata msaada gani bt jipambanue weka wazi
 
Pole yako wewe. Matatizo yako unaweza kujitatulia.

Tulioipenda Simba, tumepigwa tano. Na bahati mbaya sana huna cha kuwafanya wachezaji. Huwezi kumfukuza kocha. Yaani kichwa kinalia tiiiiiiiiiiii kama umechapwa keleb.

Tupambane tu Mkuu.
 
Nina wasiwasi, huenda una nyege.

Zikijaa, kila kitu kinageuka kuwa na changamoto.
 
Bora we una kazi,una mahali pa kupaita nyumbani,una mahusiano...KUNA WENGINE HAWANA HATA KIMOJA,NA HAWANA AFYA PIA..mshukuru MUNGU hata kwa hayo unayopitia.

Before you ask GOD for anything,thank him for everything.

Muda mwingine MUNGU huwa anataka unyenyekevu tu,na moyo wa shukrani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…