Seneta Wa Mtwiz
JF-Expert Member
- Sep 23, 2013
- 3,643
- 4,182
Wakuu,
Pamoja na kuuona ugumu katika kutafuta nafasi ya Tutorial Assistant upande wa Kiswahili/Kiingereza,
Bado nina nia na malengo ya dhati ya kuwa mwanataaluma mbobezi wa ama Kiswahili au Kiingereza(Linguistics).
______
Matakwa yangu ya awali ni kufanya
M.A(Linguistics)
Kwani naiona ni kozi ambayo haina ushindani mkubwa kutokana na ukweli kuwa watu wengi hawapendi kuisomea kwa kuhofia ugumu wa hiyo kozi,
Hivyo uwezekano wa kupata fursa kama Assistant Lecturer waweza kuwa mkubwa.
Ila changamoto kubwa ni ada yake ipo juu (kwa uwezo wangu kiuchumi).
Mbadala wake,
Nafikiria kusomea M.A(Kiswahili) kwani ada yake ni affordable kidogo ikilinganishwa na ya M.A(Linguistics).
Ila wasiwasi wangu ni kwamba,
Hii M.A(Kiswahili) yaweza kuwa na watu wengi sana halafu ikaleta changamoto kubwa kwenye kupata nafasi ya Assistant Lecturer kwa upande wa Kiswahili.
OMBI:
1. Kwa anayejua asasi zinazotoa ufadhili wa kozi za Umahiri naomba anipe dondoo,
Ili nijaribu kuomba ufadhili kwa ajili ya M.A(Linguistics).
2. Mliopo kwenye hizi kada,
Uhalisia upoje hasa kwenye kupata nafasi (za kazi) za fani hizo huko vyuoni hasa kwa upande wa Kiswahili ambako naweza kuzichanga nikaanza masomo kwa mwakani.
3. Upi ni uhalisia kulingana na hizo fikra zangu?
Tanbihi:
KIUKWELI,
LENGO LANGU KUU LA KWENDA KUSOMEA MASTER NI KUTAFUTA NAFASI YA KUWA MHADHIRI WA ELIMU YA JUU.
NATARAJIA KUOMBA UDSM/UDOM MWAKANI TUKIJAALIWA.
Karibuni kwa ushauri, changamoto na mawazo wakuu.
Pamoja na kuuona ugumu katika kutafuta nafasi ya Tutorial Assistant upande wa Kiswahili/Kiingereza,
Bado nina nia na malengo ya dhati ya kuwa mwanataaluma mbobezi wa ama Kiswahili au Kiingereza(Linguistics).
______
Matakwa yangu ya awali ni kufanya
M.A(Linguistics)
Kwani naiona ni kozi ambayo haina ushindani mkubwa kutokana na ukweli kuwa watu wengi hawapendi kuisomea kwa kuhofia ugumu wa hiyo kozi,
Hivyo uwezekano wa kupata fursa kama Assistant Lecturer waweza kuwa mkubwa.
Ila changamoto kubwa ni ada yake ipo juu (kwa uwezo wangu kiuchumi).
Mbadala wake,
Nafikiria kusomea M.A(Kiswahili) kwani ada yake ni affordable kidogo ikilinganishwa na ya M.A(Linguistics).
Ila wasiwasi wangu ni kwamba,
Hii M.A(Kiswahili) yaweza kuwa na watu wengi sana halafu ikaleta changamoto kubwa kwenye kupata nafasi ya Assistant Lecturer kwa upande wa Kiswahili.
OMBI:
1. Kwa anayejua asasi zinazotoa ufadhili wa kozi za Umahiri naomba anipe dondoo,
Ili nijaribu kuomba ufadhili kwa ajili ya M.A(Linguistics).
2. Mliopo kwenye hizi kada,
Uhalisia upoje hasa kwenye kupata nafasi (za kazi) za fani hizo huko vyuoni hasa kwa upande wa Kiswahili ambako naweza kuzichanga nikaanza masomo kwa mwakani.
3. Upi ni uhalisia kulingana na hizo fikra zangu?
Tanbihi:
KIUKWELI,
LENGO LANGU KUU LA KWENDA KUSOMEA MASTER NI KUTAFUTA NAFASI YA KUWA MHADHIRI WA ELIMU YA JUU.
NATARAJIA KUOMBA UDSM/UDOM MWAKANI TUKIJAALIWA.
Karibuni kwa ushauri, changamoto na mawazo wakuu.