ushauri juu ya ndoa hii

gfsonwin

JF-Expert Member
Apr 12, 2012
18,274
20,673
Habari zenu wanajf.

Leo nimepata ugeni wa jirani yangu kuja kumsalimia kichanga wangu. wakati naongea naye nikagundua kuwa hana raha ndipo nilipomuuliza kulikoni mama,...................? Jirani ilibidi anisimulie yaliyomkuta na akataka nimshauri lakin binafsi sikuwa na namna nzuri ya kushauri hivyo nikamwambia aje kesho jion, nia yangu niimwage hii stori jamvini kisha wale wenye busara zao washauri halafu mimi ni compile nimpe nondo.


Iko hivi mama................ ameolewa a mume wake ana miaka 64, wiki moja iliyopita huyu baba alimlawiti mvulana(13) wa jirani yetu hapa kwenye mtaa huu, ilikuwa ni mishale ya jioni saa 12 jioni ndani ya duka lake lililoko km mita chache kutoka nyumbani. kwa ushirikianio wa raia wema alikamatwa na kupelekwa polisi na mapa sasa hvi yuko lupango huyu baba. Sasa kijana aliyelawitiwa anaendelea vizuri na kwa udaku wa kitaa huyu kijana ni mchezo wake. Toka aende lupango huyu mama hajafanya jitihada yeyote ya kumuwekea dhamana, wala nini. sasa machoni pa ndugu wa mume hil limekuwa baya wanadai huyu mama anataka muewe afie gerezani ili mke awafaidi watoto kwakuwa wameshakuwa wakubwa. tena wanamsea kwa kashfa kuwa nia yake ni anataka kumuua mumewe. na tene wakadai mbona alipofanya haya mara ya kwanza alimtoa na kufuta kesi?

kwa upande wa mama .............. hii siyo nia yake ila amechoka kweli kumuwekea mumewe dhamana kwani siyo mara ya kwanza kufanya haya. ni kwamba huyu baba alishawahi kumlawiti houseboy wake na akakakamatwa, alipopelekwa polis mama alimuwekea dhamana na kisha akauza eneo ili amtoe huko lupango. na wakati anafanya haya watoto walikuwa wadogo wanasoma. hivyo hakupenda wanawe kuendelea kuuia kuwa babayao yuko gerezani.

stori ni ndefu na ukiiskia utasikitika sana kwa mama aliyeolewa, lakini wewe mwana jf unamshauri nini huyu mama?
afanyeje katika hali kama hii/ huyu anayehitaji ushauri huu ni mtu wa miaka 55. kwa wajuzi wa sheria pia toeni saada wa kisheria manake hata ndugu wa ume wanakuwa mwiba kwa huyu mama.
 
Duuh!! Story ndefu sana kila nikishuka chini nasahau juu nimesoma nin.Embu ngoja niikariri kwanza halafu ndo nitoe mawazo yangu
 
Haya ni mambo ya Court of law, na mhalifu kama huyo mahali pake anapostahili ni jela na bahati nzuri umesema siyo mara yake ya kwanza.

Ni kuwapotezea muda Members kuomba ushauri kuhusu mtu wa namna hiyo, by the way kesi za kulawiti huwa hazina dhamana mfano hai Babu Seya na kifungo chake ukikoswa miaka 30 basi ni life sentence. wacha akalawitiwe yeye sasa huko na vidume.
 
It is a family issue! Na family hustick together katika nyakati zote!

Ila wataalamu wa sheria watuambie; kuna mdhamana kwenye sexual abuse ya underage? I hope not!

Du huyo babu kweli ni hatari, hata nyumbani; l am sure kukiwa na wajukuu anaweza kuwaabuse hata na wao!
 
hao ndugu wa mume wamefanya nini kumtoa huyo muhalifu? Mbona simple mke alipaswa awaambie wakamtoe wao wenyewe.

Janaume lenyewe lilawiti!
 
Mungu mkubwa sana,hapo ni justice ilikuwa inatafutwa of previous victims.......since he escaped more than once......mungu alitaka mzee aendelee kubobea ili aje ampe kibano kizuri.......this tym mzee hatoki,akitoka mtoa mada ni PM ntajitoa JF!
 
Dada, kitu kikubwa kinachofanya watu wazoee dhambi fulani ni kwa sababu wanaepushwa na adhabu stahili. na ndio maana waswahili wakasema, mchelea mwana kulia hulia mwenyewe. Hii ina maana bora tu umchape mwanao na uvumilie kuona anaumia ili umuepushe na makubwa ya baadaye ambayo maumivu yake hayachukuliki kirahisi. Huyo baba amwache afungwe na huko akiona yanayomstahili mtu mchafu kama yeye anaweza kumrudia muumba wake kabla haijamkuta ile adhabu kuu ya mwisho.
Hao ndugu awaache tu waseme. kwa sababu if you are displining someone you love never let anyone interfere. And if u cant stand up to your decisions you are hopeless
 
bora aozee huko huko jela.akitolewa,atarudia tena tu.babu zima,hao wanaomlaumu huyo mama,jee wangelawitiwa watoto wao wangejisikiaje?dhambi zake mwenyewe mzigo abebeshwa mwengine
 
It is a family issue! Na family hustick together katika nyakati zote!

Ila wataalamu wa sheria watuambie; kuna mdhamana kwenye sexual abuse ya underage? I hope not!

Du huyo babu kweli ni hatari, hata nyumbani; l am sure kukiwa na wajukuu anaweza kuwaabuse hata na wao!

kauga hata mimi nafikiri hata wajukuu anawwea kuwafanyia hayo. ila sasa huyu mama kinachomtesa sasa ni ngugu wa mume manake wanadai mama anataka aungwe ili awafaidi watoto can you imagine?
 
Dada, kitu kikubwa kinachofanya watu wazoee dhambi fulani ni kwa sababu wanaepushwa na adhabu stahili. na ndio maana waswahili wakasema, mchelea mwana kulia hulia mwenyewe. Hii ina maana bora tu umchape mwanao na uvumilie kuona anaumia ili umuepushe na makubwa ya baadaye ambayo maumivu yake hayachukuliki kirahisi. Huyo baba amwache afungwe na huko akiona yanayomstahili mtu mchafu kama yeye anaweza kumrudia muumba wake kabla haijamkuta ile adhabu kuu ya mwisho.
Hao ndugu awaache tu waseme. kwa sababu if you are displining someone you love never let anyone interfere. And if u cant stand up to your decisions you are hopeless

umenena vyema sasa pana ishu hapa kuwa anataka afaidi watoto na mali mumewe akiwa gerezani. Nafikiri unajua maisha ya kimatumbi je huoni kama mzee akichukua miaka 36 ndugu watamtoa mama kwenye mji wake? tuongee uhalisia manake hii ndiyo hofu kubwa ya mama
 
bora aozee huko huko jela.akitolewa,atarudia tena tu.babu zima,hao wanaomlaumu huyo mama,jee wangelawitiwa watoto wao wangejisikiaje?dhambi zake mwenyewe mzigo abebeshwa mwengine

kisukari jambo nililoliona mm ni kwamba kumbe mpaka leo wapo ndugu wa mume ambao wanategemea kunyanyasa shemeji zao. Kimeniuma sana kuona hawaoni aibu ambayo mama kaipata la wanataka ndugu yao atoke huko gerezani, tena eti auze shamba sasa atauza mara ngapi? na siku ya kiisha itakuwaje?
 
Hao ndugu wanaomlaumu wao wamechukua hatua gani kumsaidia ndugu yao??
Kama watoto wao wameshakua wakubwa nao wamelichukuliaje hili??
Pamoja na kwamba mume ni mume mi naona huyo mama aache sheria ichukue mkondo wake,kama ni tabia yake akitoka atawafanyia hata wajukuu zake,ni vyema abaki huko huko sheria imfunze!
Duh ila huyo babu hana hata haya loh!
 
Kwanza asimtoe wala kumuwekea mzamana, huyo ni muhalifu na Hilo latosha. Apate Habari yake! Ila yeye sasa Kama anaweza kuondoka hayo mazingira itakuwa vema hao Ndugu waste muua.

Kama Ana watoto wakubwa anaogopa mini? Amlete hata Mmoja hapo Nyumbani ili wasije mdhulumu then yeye aondoke, huyo mtu ni Wa KUFIA gerezani, Shenzy taibu!


Habari zenu wanajf.

Leo nimepata ugeni wa jirani yangu kuja kumsalimia kichanga wangu. wakati naongea naye nikagundua kuwa hana raha ndipo nilipomuuliza kulikoni mama,...................? Jirani ilibidi anisimulie yaliyomkuta na akataka nimshauri lakin binafsi sikuwa na namna nzuri ya kushauri hivyo nikamwambia aje kesho jion, nia yangu niimwage hii stori jamvini kisha wale wenye busara zao washauri halafu mimi ni compile nimpe nondo.


Iko hivi mama................ ameolewa a mume wake ana miaka 64, wiki moja iliyopita huyu baba alimlawiti mvulana(13) wa jirani yetu hapa kwenye mtaa huu, ilikuwa ni mishale ya jioni saa 12 jioni ndani ya duka lake lililoko km mita chache kutoka nyumbani. kwa ushirikianio wa raia wema alikamatwa na kupelekwa polisi na mapa sasa hvi yuko lupango huyu baba. Sasa kijana aliyelawitiwa anaendelea vizuri na kwa udaku wa kitaa huyu kijana ni mchezo wake. Toka aende lupango huyu mama hajafanya jitihada yeyote ya kumuwekea dhamana, wala nini. sasa machoni pa ndugu wa mume hil limekuwa baya wanadai huyu mama anataka muewe afie gerezani ili mke awafaidi watoto kwakuwa wameshakuwa wakubwa. tena wanamsea kwa kashfa kuwa nia yake ni anataka kumuua mumewe. na tene wakadai mbona alipofanya haya mara ya kwanza alimtoa na kufuta kesi?

kwa upande wa mama .............. hii siyo nia yake ila amechoka kweli kumuwekea mumewe dhamana kwani siyo mara ya kwanza kufanya haya. ni kwamba huyu baba alishawahi kumlawiti houseboy wake na akakakamatwa, alipopelekwa polis mama alimuwekea dhamana na kisha akauza eneo ili amtoe huko lupango. na wakati anafanya haya watoto walikuwa wadogo wanasoma. hivyo hakupenda wanawe kuendelea kuuia kuwa babayao yuko gerezani.

stori ni ndefu na ukiiskia utasikitika sana kwa mama aliyeolewa, lakini wewe mwana jf unamshauri nini huyu mama?
afanyeje katika hali kama hii/ huyu anayehitaji ushauri huu ni mtu wa miaka 55. kwa wajuzi wa sheria pia toeni saada wa kisheria manake hata ndugu wa ume wanakuwa mwiba kwa huyu mama.
 
umenena vyema sasa pana ishu hapa kuwa anataka afaidi watoto na mali mumewe akiwa gerezani. Nafikiri unajua maisha ya kimatumbi je huoni kama mzee akichukua miaka 36 ndugu watamtoa mama kwenye mji wake? tuongee uhalisia manake hii ndiyo hofu kubwa ya mama

Its a known fact kwamba Mali waliyochuma mume na mke ni ya mume,mke na watoto...sasa hao ndugu wasiotafuta vya kwao na wanataka vya ndugu ni wa karne ya ngapi?
Mshauri aende ustawi wa jamii akaeleze yanayomkabili na atapewa protection from our good government (if there is anything good left in it). Yani there comes a time in your life where being strong is the only option.
Amuombe sana Mungu kwa sababu vita vingine not even the government can save you, Only God can.
 
Tuangalie pande zote mbili, hapa ndoa hii inaonekana ilikuwa haina AMANI, huenda ikawa ni set up case, si mnajua siku hizi binadamu tuna mbinu/akili sana za kuharibiana maisha, na mama huyu kwa maelezo ya mleta thread anaijua tabia ya huyo kijana na pia anajua tabia za mume wake, kwa hiyo ilikuwa rahisi kumtega mume wake aingie matatizoni, ndugu wa mume hawawezi tu kulalamika bila kuona tabia fulani mbaya kutoka kwa huyu mama. Ukiona moshi ujue moto upo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom