Ushauri:ingekuwa ni wewe ungefanyaje???

Ushauri:ingekuwa ni wewe ungefanyaje???

activisty

JF-Expert Member
Joined
Apr 1, 2012
Posts
315
Reaction score
107
Habarini ndugu wana JF....
Naombeni ushauri wenu katika jambo hili linalonitatiza...kuna mwanaume nimekuwa nikiishi nae takribani miaka miwili sasa.
Kisheria ni kama Mume ila moyoni mwangu simuoni kama mume...baada ya kuchoshwa na Mambo yake mengi yanayoumiza moyo wangu.nimejaliwa kuzaa nae mtoto mmoja wa kiume(6 months old).
Tatizo la huyu bwana nashindwa kulielewa hata kidogo...hajawahi kwenda kwetu angalau hata kujitambulisha na anaonekana ni mtu ambaye hafikirii kwenda kutokana na maneno pamoja na matendo yake.Kwa upande wangu ni mtu ambaye nimekuwa nikienda kwao mara kwa mara na kuwachukulia nduguze kama ndugu zangu...kitu ambacho kwake hakipo kabisa.
Kadri siku zinavyozidi kwenda ule upendo niliokuwa nao juu yake unazidi kupotea kabisa na nikimuuliza ni lini ataenda kwetu ananijibu ovyo.
Wazazi wangu wamekuwa wakiniuliza kila siku kulikon?? nashindwa kuwapa jibu...niliwatumia namba zake za simu ila hapokei simu zao.
Ndugu zangu wanaJF najua nilifanya kosa kubwa maishani mwangu kuanza kuishi na mwanaume kabla ya ndoa na tena ambaye hata kwetu hawamjui.najutia sana hili kosa...ila nashindwa kufanya maamuzi yeyote sijui kwa nini huenda ni kwa vile nanuwazia sana my son.
Ninaweza kusema naishi na mwanaume asije na chembe ya aibu na asiye na fadhila hata kidogo kwa jinsi ninavyovumilia mambo yake,mara nyingine anarudi nyumbani asubuh...alipolala anajua mwenyewe na sijawahi kumuuliza.
Kipato cha kuniwezesha kumlea my son alone ninacho ila naona atakosa malezi ya baba pale nitapoamua kuondoka.
Naomben ushauri wenu wapendwa.Je ingekuwa wewe ndo mimi ungefanyaje???
 
:nono::nono::nono::nono::nono:

Its better to leave while you can!!!!!!!!!!!!!!! The leopard never changes its spots no matter how much he is washed!

After several years akishakuzalisha watoto wa 3 utakuja kujilaumu kwa kutokuondoka mapema! TRUST ME WHEN I TELL YOU IT ONLY GETS WORSE OVER TIME!!!!!!!!!!

Kama imeandikwa ni wako ni wako hata ukiondoka atakufata, na kama si wako hata ukibaki hatokuoa!

Obama kalelewa na single Mom itakuwa wewe!!!!!!!!!!??????????????
 
:nono::nono::nono::nono::nono:

Its better to leave while you can!!!!!!!!!!!!!!! The leopard never changes its spots no matter how much he is washed!

After several years akishakuzalisha watoto wa 3 utakuja kujilaumu kwa kutokuondoka mapema! TRUST ME WHEN I TELL YOU IT ONLY GETS WORSE OVER TIME!!!!!!!!!!

Kama imeandikwa ni wako ni wako hata ukiondoka atakufata, na kama si wako hata ukibaki hatokuoa!

Obama kalelewa na single Mom itakuwa wewe!!!!!!!!!!??????????????

thnx lara ulichoandika ni ukweli mtupu.Umenitia moyo sana khs Obama.
 
usiogope kuwa single mom......fanya maamuzi mapema.......na umlee mwanao kwa amani, furaha na mapenzi yote....
 
Kwanza kabisa, ukae na mwanaume sababu unampenda. Kama humpendi ondoka.
Pili, Unasema kosa lako lilikua kukaa nae bila ndoa. Kufanya kosa kunasameheka, ila kulidumisha, au kulirudia is avoidable. Umesha gundua lilikua kosa, kwanini usirekebishe?
Tatu unasema unaogopa mtoto atalelewa bila baba, this is nonsense. Watoto wangapi walilelewa bila baba zao na they did just fine? Obama kalelewa na baba wa kambo! Wengine tunao wajua na tusio wajua wanalelewa na mama zao tu and they do well. Ni wewe tu kuamua.
Nimalize kwa kusema it is not easy, maybe una-hope kua ukimtishia kuondoka atastuka na kukuoa, instead of kukupoteza but think about this: tayari mnaishi kama mtu na mume wake, what will that ring change? Hisia zako, kuchelewa kwake kurudi na mengine ni mchanga tayari, ndoa haito badili those things.
Kama unaweza, fanya maamuzi magumu, endelea na maisha yako. akikupenda aje kwenu, akuoe, na muanze maisha mapya (but usiwekei sana focus huku, be independant kwanza)
 
Achana nae, na waambie ndugu zako wampotezee,kama wanapiga hapokei nidharau hana nia njema na hafai katika jamii. Maana hata angekuwa hataki kukuoa angesikia wanasema nini angewaheshimu hata kwa ajili ya mtoto. Achana nae kabisa,kama wako atakutafuta baadae akili ikimrudia.
 
Kwanza kabisa, ukae na mwanaume sababu unampenda. Kama humpendi ondoka.
Pili, Unasema kosa lako lilikua kukaa nae bila ndoa. Kufanya kosa kunasameheka, ila kulidumisha, au kulirudia is avoidable. Umesha gundua lilikua kosa, kwanini usirekebishe?
Tatu unasema unaogopa mtoto atalelewa bila baba, this is nonsense. Watoto wangapi walilelewa bila baba zao na they did just fine? Obama kalelewa na baba wa kambo! Wengine tunao wajua na tusio wajua wanalelewa na mama zao tu and they do well. Ni wewe tu kuamua.
Nimalize kwa kusema it is not easy, maybe una-hope kua ukimtishia kuondoka atastuka na kukuoa, instead of kukupoteza but think about this: tayari mnaishi kama mtu na mume wake, what will that ring change? Hisia zako, kuchelewa kwake kurudi na mengine ni mchanga tayari, ndoa haito badili those things.
Kama unaweza, fanya maamuzi magumu, endelea na maisha yako. akikupenda aje kwenu, akuoe, na muanze maisha mapya (but usiwekei sana focus huku, be independant kwanza)

thnx a lot...kweli JF ni home of great thinkers,sometimes kichwa kinakuwa overloaded kiasi kwamba nashindwa kutambua kama bado nakosea kuendelea kuishi dhambini.Asante sana kwa ushauri na ufunguzi wa akili.
 
Sasa kwa nini hujawahi kumuuliza kwa nini huwa anarudi asubuhi? unaogopa atakuacha! upendo wa kweli lazima ujue mmeo yuko wapi kwanini harudi nyumbani,vinginevyo ninatia shaka huu uhusiano.Mwambie sasa unaomba mfunge ndoa na umwambie aache tabia ya kutorudi nyumbani akikataa jua anataka kukutumia tu achana naye kwa maana anaku risk na magonjwa kama UKIMWI hasa huko anakolala.

Heshima ya ndoa ni pamoja na kuheshimu ndugu wa pande zote upande wa mke na upande wa mme au na ndugu zake huwa hapokei simu zao? maisha ya ndoa yanakuwa mateso sana hasa kama mmoja wapo hajampenda mwenziye.
 
Achana nae, na waambie ndugu zako wampotezee,kama wanapiga hapokei nidharau hana nia njema na hafai katika jamii. Maana hata angekuwa hataki kukuoa angesikia wanasema nini angewaheshimu hata kwa ajili ya mtoto. Achana nae kabisa,kama wako atakutafuta baadae akili ikimrudia.

Asante sana....i will do it!!
 
Sasa kwa nini hujawahi kumuuliza kwa nini huwa anarudi asubuhi? unaogopa atakuacha! upendo wa kweli lazima ujue mmeo yuko wapi kwanini harudi nyumbani,vinginevyo ninatia shaka huu uhusiano.Mwambie sasa unaomba mfunge ndoa na umwambie aache tabia ya kutorudi nyumbani akikataa jua anataka kukutumia tu achana naye kwa maana anaku risk na magonjwa kama UKIMWI hasa huko anakolala.

Heshima ya ndoa ni pamoja na kuheshimu ndugu wa pande zote upande wa mke na upande wa mme au na ndugu zake huwa hapokei simu zao? maisha ya ndoa yanakuwa mateso sana hasa kama mmoja wapo hajampenda mwenziye.

kuna kipindi nikiwa mjamzito nilimuuliza...alinifokea sana,hadi majirani walisikia..sitaisahau hiyo cku.huwa simuulizi kuepuka shari.
 
Kwanza kabisa, ukae na mwanaume sababu unampenda. Kama humpendi ondoka.
Pili, Unasema kosa lako lilikua kukaa nae bila ndoa. Kufanya kosa kunasameheka, ila kulidumisha, au kulirudia is avoidable. Umesha gundua lilikua kosa, kwanini usirekebishe?
Tatu unasema unaogopa mtoto atalelewa bila baba, this is nonsense. Watoto wangapi walilelewa bila baba zao na they did just fine? Obama kalelewa na baba wa kambo! Wengine tunao wajua na tusio wajua wanalelewa na mama zao tu and they do well. Ni wewe tu kuamua.
Nimalize kwa kusema it is not easy, maybe una-hope kua ukimtishia kuondoka atastuka na kukuoa, instead of kukupoteza but think about this: tayari mnaishi kama mtu na mume wake, what will that ring change? Hisia zako, kuchelewa kwake kurudi na mengine ni mchanga tayari, ndoa haito badili those things.
Kama unaweza, fanya maamuzi magumu, endelea na maisha yako. akikupenda aje kwenu, akuoe, na muanze maisha mapya (but usiwekei sana focus huku, be independant kwanza)


Maa Shaa Allah, what an advise on earth! Ila sijapenda hapo kwenye red yaani hiyo kitu isingekuwepo kabisa! Yaani sasa hivi anarudi asubuhi akioa si atakuwa anarudi jumatatu mpaka kumatatu akijua kuwa ndege yumo tunduni na ndoa za wenzetu zikifungwa ndio zimefungwa "pingu za maisha" hakuna kujikuna wala kunyoosha mikono!
 
Sasa umeshasema sometimes anarudi asubuhi hiyo ni dhahiri huyo mtu anamwanamke/wanawake wengine, hebu shtuka mapema kabla hajakuongezea tatizo lingine la UKIMWI!!
 
Hakuna Baba hapo kuna mwanaume mwenye uwezo wa kumpa mimba mwanamke lakini hastahili kabisa kupewa hadhi ya kuitwa Baba. Pole sana kwa yaliyokukuta anza taratibu za kujitafutia sehemu yako haraka iwezekenavyo na wala usibadili mawazo yako maana umeshampa nafasi chungu nzima za kujirekebisha lakini ameshindwa kuzitumia.
 
Sasa umeshasema sometimes anarudi asubuhi hiyo ni dhahiri huyo mtu anamwanamke/wanawake wengine, hebu shtuka mapema kabla hajakuongezea tatizo lingine la UKIMWI!!

wapo wengi tu,wengine nawajua kwa macho na wengine kwa majina....hivi vitu sidhani kama vinavumilika!!! pray for me nisonge mbele wala nisirudi nyuma.asante kwa ushauri.
 
Hakuna Baba hapo kuna mwanaume mwenye uwezo wa kumpa mimba mwanamke lakini hastahili kabisa kupewa hadhi ya kuitwa Baba. Pole sana kwa yaliyokukuta anza taratibu za kujitafutia sehemu yako haraka iwezekenavyo na wala usibadili mawazo yako maana umeshampa nafasi chungu nzima za kujirekebisha lakini ameshindwa kuzitumia.

sure!!
 
Nenda kwa wazazi wake na uwambie ukweli kuhusu tabia huyo mwenzako
 
Binafsi naona huna mume hapo,hilo ni gumegume.Yaani baba mzima analala nje wakati ana mke ndani!!! Analala kwa nani! .Dada yangu jipange sasa wake up time is not your again. Do what you are scared to do. Maamuzi magumu ndo yatanusuru maisha yako na mtoto wako.
 
Back
Top Bottom