Ushauri (Bure) wa Biashara

Mtanganyika

JF-Expert Member
Jul 18, 2007
1,601
945
Wakuu,

1. Fahamu Biashara Yako Nje Ndani
Muda kama huu kama huifahamu biashara yako kindakidaki utakwenda na maji tuu. Unakutana na mtu anakwambia nina biashara yangu ya butcher, unamuliiza kwa siku unazua kilo ngapi anakwambia kuna siku nauza 60KG siku nyingine 45KG, unatamani umkate makofi sababu hajui anauza KG ngapi. Anajua inabidi akwambie kwa wastani nauza 55KG kwa siku, ndani ya mwezi huu mauzo ya juu ya siku yalikuwa 75KG na mauzo ya chini yalikuwa 45KG, faida yangu ni 40% ya bei ninayo nunulia ambayo ni xxx kwa siku napata faida ya shiling kadhaa kabla ya kutoa gharama za undeshaji kadhaa.

Umeona mtu anaejua anachofanya na anae subiri speed ya mwendokasi imtoe njiani. Lakini ukiachilia kufahamu financial zako, lakini lazima ufahamu wateja wako. Unatakiwa kujua jee unawateja wangapi ambao wanarudia rudia kufanya biashara na wewe na jee unawapa nafasi ya kwanza? Jee wateja wangapi wapya unapata kwa week? kwa kila mteja mmoja anatumia kiasi gani katika biashara yako? Jee una mpango wa kuwapa wateja motisha ili waongeze ununuzi kwako.

2. Weka Malengo Katika Biashara Yako
Biashara nyingi ndogo zinaendeshwa ovyo ovyo, mtu anamkaa asubuhi anafungua jioni anafunga, akiletewa kitu na supplier hata kama hajui kitauzika yeye ananunua tuu basi ili mradi yupo yupo, ndugu yangu na mwendo kasi huu utakwenda tuu. Muhimu kujiwekea malengo, lengo kuu namba moja biashara lazima iwe na BUDGET ndio bajeti, lazima undengeneze budget ya mwezi hadi mwezi ambayo mwisho ikupe budget ya mwaka. Katika budget yako ya mwezi lazima uweke makadirio ya mauzo kwa mwezi, makadirio ya gharama na makadirio ya faida. Makadirio ya mauzo lazima yawe yanaongezeka kwa kiasi fulani, na nilazima uweke mchakato wa kusukuma mauzo yako kufikia makadirio. Mwisho wa siku ni muhimu kulinganisha makadirio na mauzo, na kuelezea tofauti yoyote iwe ya juu au chini.

Mfano; una duka la hardware, umebudget mauzo kuwa 100 na mwisho wa mwezi yakuwa 90 lazima uwe na mchanganuo kwa nini budget yako imekuwa 10% below. Vilevile wanaokusaidia katika biashara lazima wote wafahamu malengo ya kila mwezi na mwaka ni mkakati wa kufikia malengo.

2. Boresha Huduma Kwa Wateja
Ushindaji wa biashara umeongezeka sana na hali ngumu ya maisha inapamba moto. Sasa kama utaamua kufumbia macho kuweka mkakati wa kuwajali wateja basi mwendo kasi lazima likutoe njiani. Mkakati wa kuwajali wateja lazima uandikwe chini, sio kusema tuu nina wajali wateja. Hapana tengeneza hata kurasa mbili za mkakati wa kuwajali wateja, fundisha wafanyakazi wako wote mkakati huo, haijalishi mfanyakazi wa uwani au offisini, wote lazima wafahamu mbinu za biashara yako ya kuwajali wateja. Ushasikia neno mteja mfalme, wengi tunadhani lile neno ni usemi tuu, hapana ukimuhundumia mteja kama mfalme ujue atarudi tuu.

Weka mkakati wa jinsi ya kuwajali wateja wako, wafundishe wafanyakazi wako. Hakikisha kila saa una sura ya kutabasamu, tumia maneno kama tafadhali, karibu. Kama kitu hicho huna mwambie kwa ukimya kwa nini huna, zungumza na mteja ukiwa umeacha kila kitu, sio unaongea na mteja huku upo kwenye Instagram. Weka kisanduku cha kuwauliza wateja wanaonaje huduma yenu, chukua takwimu, fanya improvement kwenye mapungukufu, toa motisha kwa wafanyakazi wenye kujali wateja kwa hali ya juu.

Wakuu hizo ni moja dondoo chache ambazo zinaweza kusaidia biashara yako ikakuwa kwa speed ya juu wakati huu mgumu.

Nilipotea kidogo, sasa nimerudi. Nakamilisha usajili wa kampuni yangu itakayo julikana kama Faru Venture Capital (FVC), lengo ni kuwekeza kwenye biashara zenye uhitaji wa mitaji midogo na ya kati, kwa kushirikiana. Muda ukifika nitalizungumzia zaidia.
 
Ushauri mzuri na mengine tulishawahi kuongea nayafanyia kazi mkuu,umesharudi tz?
 
Ushauri makini kabisa ndugu. Haya ndio mambo yanayohitajika JF. Kukosekana kwa elimu hii ukmesababisha watu wanafanya biashara miaka nenda rudi lakini haikuii wala haimsaidii kupiga hatua. Ubarikiwe
 
Nimeupenda ushauri wako mkuu kwani na mm ni mjasiriamali mdogo wa stationery

Unajipangaje kutoka ujasilimali mdogo kwenda wa kati? Tupo mchakato wako, nini unafanya kukutofautisha na vida umiza vyote vya stationary kila kona. Nikupe idea moja, anzisha customer list ( horodha ya wateja wako), kila mteja atakae kubali kuweka jina kwenye list yako unamuwekea lengo kwamba ukipiga copy 100 ndani ya mwezi huu basi kwa miezi 2 ijayo nakupa 10% punguzo, hii itakuongezea wateja na royalty ambayo ndio kitu muhimu zaidi
 
Ushauri makini kabisa ndugu. Haya ndio mambo yanayohitajika JF. Kukosekana kwa elimu hii ukmesababisha watu wanafanya biashara miaka nenda rudi lakini haikuii wala haimsaidii kupiga hatua. Ubarikiwe


Mkuu umesema ukweli, maza wangu anafuga kuku tangu mwaka 1987 mpaka leo anawapiga vibomu vya chakula cha kuku. Unaweza sema kwa nini hujampa huo ushauri, biashara na hobby ni vitu viwili kinzani, wengi wanadhani wanafanya biashara kumbe hobby. Mfano nawaambia wauza kuku, kwa nini kuku wako wanatofautiana na uzito? Kuku mmoja ana 1KG mwingine ana 1/2KG kwa nini? anakwambia aaah sasa utafanyaje. Unamuuliza kwanini kuku wa njee mfugaji anaweza kuwaweka wote waka na KG moja, sababu watu wana sort kuku kila baada ya muda ili kuwa malisho bora wale walio chini ya uzito.

Biashara yako kama haikuumizi kichwa ujue hiyo ni hobby tuu.
 
Mkuu hongera sana kwa venture capital yako, najiulizaga sana kwa nini bongo hakuna venture capital firms, na chache unazoziona unakuta zipo based nairobi sema zinaoperate hadi TZ.

If I read you correctly target market yenu ni small to medium enterprises, what is your smallest and highest amount does your firm offer?
Nitakuwepo mjini hapo ndani ya week mbili inshallah.
 
Mkuu hongera sana kwa venture capital yako, najiulizaga sana kwa nini bongo hakuna venture capital firms, na chache unazoziona unakuta zipo based nairobi sema zinaoperate hadi TZ.

If I read you correctly target market yenu ni small to medium enterprises, what is your smallest and highest amount does your firm offer?

Mkuu Tatizo kubwa sana la Tanzania ni sheria zinazolinda mitaji, sheria ni mbovu hakuna mfano. Pili, ugumu mkubwa wa Tanzania ni innovative mind zipo chache sana. VC business ni very risk, hivyo sehemu ambayo naweka pesa lazima iwe na potential ya kushika soko sababu ya innovation yake, na kingine watu wengi wenye biashara Tanzania unakuta hana registration, anaendesha biashara kama genge, hana documentation ya process, hana bank account ambayo biashara iko link, ana changanyachanganya tuu cash, zakwakwe za biashara twende. Hapo inakuwa ngumu sana kuweka mtaji, sababu pesa za VC most of the time ni za watu sisi tunafanya management of cash kwa kutafuta good investments.

Capital infusion inaanzia 5M-100M, lakini kuna vigezo vingi ambavyo vinatumika depends on many things. Mfano kuna biashara nyingine haina hata leseni ya biashara lakini product zake naziona zina potential kama zitafanyiwa packaging and registrations na local office. Business kama hii japo ina potential kubwa, lakini offer yangu might end to be own over half of the business sababu their is so much work that will do kabla ya kuipeleka biashara kwenye soko.
 
Mkuu umenifurahisha huko mwishoni kwamba you take half ownership, sasa wewe ukichukua equity nyingi namna hiyo kwenye early stages, later on mkitaka kuraise fund tena huyo mjasiriamali si atajikuta anakuwa mfanyakazi kwenye kampuni yake mwenyewe.

Do you guys have specific industries ambazo mnazitarget kwenye kuinvest?
Mkuu Tatizo kubwa sana la Tanzania ni sheria zinazolinda mitaji, sheria ni mbovu hakuna mfano. Pili, ugumu mkubwa wa Tanzania ni innovative mind zipo chache sana. VC business ni very risk, hivyo sehemu ambayo naweka pesa lazima iwe na potential ya kushika soko sababu ya innovation yake, na kingine watu wengi wenye biashara Tanzania unakuta hana registration, anaendesha biashara kama genge, hana documentation ya process, hana bank account ambayo biashara iko link, ana changanyachanganya tuu cash, zakwakwe za biashara twende. Hapo inakuwa ngumu sana kuweka mtaji, sababu pesa za VC most of the time ni za watu sisi tunafanya management of cash kwa kutafuta good investments.

Capital infusion inaanzia 5M-100M, lakini kuna vigezo vingi ambavyo vinatumika depends on many things. Mfano kuna biashara nyingine haina hata leseni ya biashara lakini product zake naziona zina potential kama zitafanyiwa packaging and registrations na local office. Business kama hii japo ina potential kubwa, lakini offer yangu might end to be own over half of the business sababu their is so much work that will do kabla ya kuipeleka biashara kwenye soko.
 
Asamte mkuu kwa uzi huu, pia ninapenda udadavue juu ya njia za kutumia ili kupata siri za biashara ambayo nahitaji kuifanya ila sina ujuzi nayo, mfano:- nataka kuzalisha mafuta ya nywele ila sina utaalamu na nikiuliza wazalishaji hawanipi ufafanuzi kwa kuogopa ushindani sokoni. Je nitafanyaje kujua njia za kufanikisha hili?
 
Bado nafuatilia hasa huu mjadala uloibuka wa capital......Go on wakuu

Mkuu umenifurahisha huko mwishoni kwamba you take half ownership, sasa wewe ukichukua equity nyingi namna hiyo kwenye early stages, later on mkitaka kuraise fund tena huyo mjasiriamali si atajikuta anakuwa mfanyakazi kwenye kampuni yake mwenyewe.

Do you guys have specific industries ambazo mnazitarget kwenye kuinvest?

Mkuu unafanya valuation ya biashara kisha unaangalia jee thamani ya pesa ninayo weka na thamani ya biashara kwa leo zina shabiiana. Mfano, product ni manukato na sabuni za mjasilimali lakini hana registration ya biashara, hajafanya lab test ya chemicals za kwenye products, hajui atafanyaje packaging, hana roadmap ya marketing na strategy yake. Kaka inabidi nikae chini kufanya kazi zote plus capital, dawa ni moja tuu lazima niwe na umiliki wa 50%.

In the future kama tunataka kuongeza mtaji na route zipo mbili either tuna fanya kupitia mkopo ( leverage) au equity, sasa kama lengo ni kuongeza kupitia equity inabidi wote tukubaliane kupunguza % ya umiliki.
 
Asamte mkuu kwa uzi huu, pia ninapenda udadavue juu ya njia za kutumia ili kupata siri za biashara ambayo nahitaji kuifanya ila sina ujuzi nayo, mfano:- nataka kuzalisha mafuta ya nywele ila sina utaalamu na nikiuliza wazalishaji hawanipi ufafanuzi kwa kuogopa ushindani sokoni. Je nitafanyaje kujua njia za kufanikisha hili?

Mkuu hapa njia moja kubwa ni wewe kuumiza kichwa kumkamata mmoja wa wazalishaji akubali kukupa mpango mzima. Na dawa ni moja tuu mlungula au cash, lakini usiende kienyeji enyeji utapoteza pesa na hupati recipe. Cha kufanya kwanza poteza muda kuisoma business yenyewe kwa nje nje macro analysis, angalia washindani wako, angalia weakness (udhaifu) wa product zote kwenye soko, angalia kama ukipata hiyo secret source utajiposition vipi kukamata % ya soko. Wakati ushapoteza muda huo na kwamba umehakiki unafahamu soko lote na umejua udhaifu wa product zilizo sokoni, sasa weka mkakati (strategy) wa kutafuta dhaifu mzalishaji (weaker) ambae atakubaliana na wewe either wa kupartner na wewe sababu unakuja na cash and technical know-how ya kuingia sokoni, au umnunue mtu kabisa wewe utengeneze mchakato mzima.

Mafuta ya nywele mimi pia natolea macho, hasa ambayo ni natural ingredients yasiyo na artificial chemicals. Kingine sababuni za kuogea na shampoo vyote liquid hii nayo naitolea macho.
 
Wakuu ambao mpo interest tunaweza kukutana baada ya mfungo mahali tukanywa kahawa kidogo huku tukibadilishana mawazo.
 
Naona mtanganyika amekujibu vizuri sana lakini sio mbaya na mimi nikiongeza machache. Mkuu hizo formula ambazo washindani wako wanatumia kutengeneza bidhaa zao kwenye lugha ya kisheria ndio hati miliki(Intellectual property) ambayo kiundani zaidi ni trade secrets, ambapo kiukweli lazima walinde siri hizo la sivyo kila mtu anaweza kuchukua ujuzi wao na kuzalisha bidhaa kama zao.

Binafsi ningekushauri kuanzia kufanya research yako google ili uone watu wengine huko duniani wanafanyaje, kama ikishindikana kupata hiyo taarifa unayoitaka huko google basi jaribu kununua izo taarifa kutoka kwa washindani wako.
Asamte mkuu kwa uzi huu, pia ninapenda udadavue juu ya njia za kutumia ili kupata siri za biashara ambayo nahitaji kuifanya ila sina ujuzi nayo, mfano:- nataka kuzalisha mafuta ya nywele ila sina utaalamu na nikiuliza wazalishaji hawanipi ufafanuzi kwa kuogopa ushindani sokoni. Je nitafanyaje kujua njia za kufanikisha hili?
 
Binafsi ninashauri kama tutaweza kuanzisha mijadara/threads kadhaa zinazozungumzia biashara i.e raisings funds, business growth, marketing, branding, employee management etc ili tu kuattract attention ya members wengine itasaidia hata hapo tutakopokutana kutakuwa na watu wengi zaidi ukilinganisha na sasa.
Wakuu ambao mpo interest tunaweza kukutana baada ya mfungo mahali tukanywa kahawa kidogo huku tukibadilishana mawazo.
 
Back
Top Bottom