Ushauri: Amemuambia akichepuka atamuua

Ushauri: Amemuambia akichepuka atamuua

The Hidden

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2017
Posts
246
Reaction score
102
Habari zenu wana JF? Kwa sasa mimi naweza sema nina ufahamu mpana sana juu ya ishu ya mahusiano kwani nilikaa katika uchumba kwa miaka kadhaa na tangu nioe sasa ni karibu miaka miwili lakini kwa hili la huyu ndugu yangu nimeshindwa kulielewa japokuwa ananitegemea mara nyingi sana katika ushauri so imebidi nikwepe kuzungumza naye juu ya hili nipate mawazo yenu kwanza:

Rafiki yangu huyu ambaye sasa ni kama ndugu, amekuwa na mahusiano na binti mmoja ambaye mpaka sasa ni miaka 2 na nusu(kwa maelezo yake) wakiwa kama wachumba binti huyu ni mvumilivu katika dhiki ya kukosa pesa na japokuwa kuna wakati wanatofautiana mara nyingi alikuwa akinishirikisha nikamshauri na wakarejeana.

Leo hii ameniijia anasema ni mara ya pili sasa amekuwa akimsikia mpenzi wake huyo(mke) ambaye anaoneshaga kuwa ni mtu mwenye wivu sana, akimwambia huyu ndugu kuwa kama atamuoa na ikatokea amemsaliti yaani kuchepuka basi atamuua abaki tu na nyumba, jamaa anasema kwa mara ya kwanza haikumuingia akilini sababu alidhani ni utani tu ila leo hii wakiwa wanaangalia movie iliyoonesha mshikaji mchepukaji alirudia tena kumwambia hivyo, hii kauli sasa imemchanganya na anajihoji amuoe au amuache huyu mwanadada.

Nimejifikiria sana kwa upande wangu nimeshindwa kumwambia jamaa nini aamue ikiwa jamaa anaonesha kumhitaji huyu mwanamke ila anahofu kauli hizo na mwanadada pia huwa anaonesha anampenda sana jamaa!

Nimejiuliza kwa upande wangu hivi inawezekana mwenye dhamira ya kufanya hivyo akajinadi kabisa? Au alitumia kauli hizo kumtishia tu jamaa asijechepuka? Na pia hayo mawazo anayatoa wapi kama si kwamba labda alimaanisha?

Karibuni wadau mnipe pa kuanzia kwasababu nimemuahidi jamaa kuongea naye juu ya hili hapo kesho
 
Wanawake wengi wa kujilinda mkuu ,nahapo siku akichepuka .

Maajabu nikwamba ,mwanamke ataishia kumpiga vimakofi kifuani ,baadae atajikimbiza chumbani anaanza kulia huku amekumbatia mto akingoja uje umguse mabegani umwambie " Am sorry baby , yaani hata sikufanya kitu maana mashine haikusimama kabisa"

Hapo atakuangalia moyoni anacheka ,mdomoni anakuambia "kwendraaaaa zako weeeeewe kweli usisimamishe?" ukikazia hapo hapo ,anakuambia yameisha .
 
Kimtokacho MTU ndicho kilichopo rohoni, sasa Jamaa anasubiri nini kumkimbiza akatafute killers wenzie
 
Huyo binti ni gas kabisa yaani anaongea upupu kama huo akidhani atamtisha,ilitosha kumwambia sipendi ucheat sio mpaka anaahidi kukuua kabisa.

Yaani hawa wadudu sijui vipi hapo kama ndo mtihani kashafeli,mwanamke hana hats chembe ya moyo wa huruma. Unajua kuna maneno hutegemei yatoke kwa mtu unayetarajia uishi nae milele hata kama utani hapana aisee
 
Huyo binti ni gas kabisa yaani anaongea upupu kama huo akidhani atamtisha,ilitosha kumwambia sipendi ucheat sio mpaka anaahidi kukuua kabisa. Yaani hawa wadudu sijui VP hapo kama ndo mtihani kashafeli,mwanamke hana hats chembe ya moyo wa huruma. Unajua kuna maneno hutegemei yatoke kwa MTU unayetarajia uishi nae milele. Hata kama utani hapana aisee
Kwahiyo kama wewe ungemshauri nini Mkuu?
 
Wanawake wengi wa kujilinda mkuu ,nahapo siku akichepuka .

Maajabu nikwamba ,mwanamke ataishia kumpiga vimakofi kifuani ,baadae atajikimbiza chumban anaanza kulia huku amekumbatia mto akingoja uje umguse mabegan umwambie " Am sorry baby , yaan hata sikufanya kitu maana mashine haikusimama kabisa"

Hapo atakuangalia moyon anacheka ,mdomon anakuambia "kwendraaaaa zako weeeeewe kweli usisimamishe?" ...ukikazia hapo hapo ,anakuambia yameisha .
Wewe uliwahi kuambiwa hivyo Mkuu?
 
Sasa umesema Jamaa anamuhitaji.

Sasa kwanini awe na Mawazo ya wasi wasi kwa yule ampendae!

Kwahiyo jamaa anaonesha dhahiri ni Kiwembe, na ni mchepukaji.

Tukirudi hapo kwenye Suala husika ni kwamba, huyo DEMU anatishia tu.

Jamaa yako asiogope wala nini.

Kama kweli anamuhitaji huyo DEMU kama anavyodai, basi aendelee nae tu
 
Huyo kaongea hayo maneno ili kumtisha tu jamaa na pia inaonekana anampenda kupitiliza hapo ingekuwa ni sisi wanaume tumetoa vitisho kama hivyo wala hakuna mtu angejali, ila kwakuwa ni mwanamke kasema hivyo basi imeshakuwa nongwa.
 
Huyo mwanaume ni venye anampango wa kuchepuka/anachepuka ndio maana anaogopa
 
Hamna ni kama wanawake haturidhiki na mume mmoja maisha
Hakuna kiumbe chochote cha kike chini ya jua kilicho umbwa na tamaa ya viumbe vya kiume zaidi ya kimoja at a time, lakini hakuna kiumbe chochote cha kiume kinacho ridhika ama kilicho umbwa kwaajili ya kiumbe cha kike kimoja,


Iwe ng'ombe, kuku, mbuzi, swala, sungura, simba, tembo, yaan chochote kile mwanaume sio kwaajil ya mwanamke mmoja, ila mwanamke ni kwaajili ya mwanaume mmoja
 
Sema wewe hapo mkeo kakupiga biti siyo rafiki yako.....

Mkeo anachepuka ndiyo maana anakuonya usimgundue haraka....
 
Hayo ni maneno tu, ni mipango ya kazi, ukimfuatilia yeye ndiyo atakua anachepuka, anakutengenezea mazingira fulani hivi uwe boya.
 
Back
Top Bottom