chungutamu
Member
- Apr 20, 2013
- 13
- 3
Habari wana Jf?
Wapendwa, nina rafiki yangu anahitaji ushauri la kufanya na maamuzi ya kuchukua.
Yeye ni binti na alikuwa na boyfriend wake ambae walidumu nae takriban miaka mitatu. Wakati wapo katika hayo mahusiano huyu mtu wake alikuwa na tabia ya kum cheat mwenzie na akim baini anombwa msamaha yanaisha. Hii tabia iliendelea ya huyo boyfriend wake kumsaliti hadi pale huyo dada alipoamua kuachana naye sababu ya kuto muamini tena. Hivyo akamwambia kuwa anaomba kila mtu ashike 50 zake.
Baada ya hapo rafiki yangu huyo alijiingiza katika mahusiano mengine yaliyodumu miezi 8 na wakapendana sana. Ikumbukwe kuwa Boyfriend wake wa mwanzo bado anampenda sana huyo dada. Pia kuna tatizo lililopo kwa huyu wa sasa kuwa ni tofauti ya kiimani. Mwanaume ni Muislam na hali mwanamke ni Mkristo na hataki kubadili dini, huyo boyfriend wake wa sasa amemwambia huyo dadad ole wake arudi kwa mpenzi wake wa mwanzo atahakikisha wanamkosa wote.
Je afanyeje?
Wapendwa, nina rafiki yangu anahitaji ushauri la kufanya na maamuzi ya kuchukua.
Yeye ni binti na alikuwa na boyfriend wake ambae walidumu nae takriban miaka mitatu. Wakati wapo katika hayo mahusiano huyu mtu wake alikuwa na tabia ya kum cheat mwenzie na akim baini anombwa msamaha yanaisha. Hii tabia iliendelea ya huyo boyfriend wake kumsaliti hadi pale huyo dada alipoamua kuachana naye sababu ya kuto muamini tena. Hivyo akamwambia kuwa anaomba kila mtu ashike 50 zake.
Baada ya hapo rafiki yangu huyo alijiingiza katika mahusiano mengine yaliyodumu miezi 8 na wakapendana sana. Ikumbukwe kuwa Boyfriend wake wa mwanzo bado anampenda sana huyo dada. Pia kuna tatizo lililopo kwa huyu wa sasa kuwa ni tofauti ya kiimani. Mwanaume ni Muislam na hali mwanamke ni Mkristo na hataki kubadili dini, huyo boyfriend wake wa sasa amemwambia huyo dadad ole wake arudi kwa mpenzi wake wa mwanzo atahakikisha wanamkosa wote.
Je afanyeje?