Ushahidi wa Udikiteta ndani ya CHADEMA.

Status
Not open for further replies.
Hili nalo kilaza kweli....Hapa ni kama kusoma biblia msikitini au Qran Kanisani wakati hayakuhusu.....Kalakabaho mchanga wewe
 
Kama umri wa Zitto utakuwa bado basi wa Dr Slaa utakuwa umepitiliza manake sasa hivi ameanza kupukutika mpaka nywele.


Hoja hii ni babu kubwa, itabidi kuifungulia Thread. Big up mkuu.

Ngoja nikusanye Takwimu.
 
kwa taarifa nilizo nazo ni kuwa zitto ana mchumba tayari na sikusikia jina la zawadi ngoda,ila kwa kuwa zitto ni mwislam endelea na jitihada unaweza kuja kuwa first lady wa kufikirika.
safari tuliyo nayo na aina ya gari tulilonalo dereva kwa wakati huu hatakiwi kuwa machachari,tunataka dereva mwenye kuijua njia ya kitonga kona zote mbaya na hila za wahalifu ccm katika hizo kona mbaya,tukifika njia tambarare ndio tutafikiria kumpa dereva machachari ili aonyeshe mbwembwe za kupiga gia na kupiga change down.

Hapo kwenye Tambarare mtafika lini? Yasiwe ni maneno tu na mkaamua kutofika hapo na matokeo yake mkaachiana uongozi wenyewe kwa wenyewe na wengine wakawa watazamaji na kuishia kwenye UBUNGE tu.

Kwa maelezo yako yanathibitisha kuwa Demokrasia ndani ya chama iko mbali sanaaa. Hata Rais Yoweri Museveni alikuwa na bado anayo matamshi yanayolingana na ya kwako, na mpaka leo yupo na wala hakai mkao wa kuaga ndio kwanza yupo katika mkao wa kula. Jihadharini na kuitwa majina kama DIKITETA na kadhalika.
 
Demokrasia ya kweli ni lazima ianzie katika vyama vya kisiasa. CHADEMA ni chama pekee katika vyama vikubwa TZ kilichoonyesha uchanga mkubwa wa Demokrasia hususan katika chaguzi za nafasi za juu ndani ya chama hicho.

Mtihani wa kwanza mkubwa ulikipata chama pale Mh Zitto Kabwe alipojitokeza kugombea nafasi ya Uenyekiti wa chama hicho. Wahasisi wa chama hicho walifahamu fika kwamba Mh Mbowe asingeweza kumshinda kijana matata na mashuhuri huyo. Ni wazi kuwa ukilinganisha elimu zao ni sawa na mlima Kilimanjaro (Zitto) na kichuguu (Mbowe) sikwambii mambo mengine. Hapo kura ya VETO ikatumika, wajiitao wahasisi au wazee wa chama wakamlazimisha Kabwe ajitoe,-Udikiteta ukatumika.. Wakafanikiwa.

Safari hii CHADEMA wameingia katika mtihani mkubwa zaidi, Kijana huyu ametangaza dhamira yake ya kugombea Urais. Safari hii anataka kumpangua Katibu wake- Mh Slaa ambaye naye anahitaji kugombea Uraisi kwa mara ya pili. Nilikuwa Arusha wiki mbili zilizopita na kuzungumza na wakuu wa ngazi za juu CDM (majina ninayo). Wamesema, huyu kijana ana ndoto za mwendawazimu, ni heri chama kife kuliko Kabwe kupewa nafasi hiyo ya kugombea urais. Hapa najiuliza, hivi watafanya nini? Lakini kama waliweza kumshinyikiza ajitoe kugombea Uenyekiti, nafikiri ni mbinu hizo hizo zitatumika Kumtupilia mbali. Huu ni UDIKITETA MKUBWA KABISA.

Kuna kila sababu ya kumuelewa Mh Sitta alipomwita Mh Slaa "Dikiteta", kwani kinachotakiwa ni uchaguzi wa vidole na sio nguvu za KI-Idd Amini Amini Dada. Na ni katika mazingira haya CHADEMA Ipo katika TEST kubwa sana. Mh Zitto Kabwe kadhamiria, na ametangaza mara nyingi tu Dhamira yake hiyo.

Safari hii ni lazima Vidole vitumike, ama sivyo Tendwa atalazimika kukifuta Chama hicho kwa kukiuka kanuni za vyama vya siasa. Kwa jinsi ninavyowafahamu akina Mtei, watatumia udikiteta na kumtupa nje kabla hajaingia hatua ya vidole. Je, huu sio udikiteta uliokithiri? Na watu kama hawa wakichukua nchi mnategemea nini?

Sehemu zilizo na red, zizingatie.
  1. Alishauriwa/alishinikizwa ajitoe akakubali... Alikubali mwenyewe. Kama alikuwa hajaridhika, kwanini alitoa jina? Alikutuma ulete thread hapa kulaumu? yeye hana mdomo? maana yeye ni mjumbe wa kamati kuu... kumbe ana fursa ya kuwasilisha hoja zake katika vikao husika.
  2. Kwani muda wa kuchukua fomu za uchaguzi wa 2015 umepita? Kwanini tusisubili ikifika 2015 aende kuchukua fomu anyimwe ili tujue kuwa hakuna demokrasia? wewe umeona ushahidi wapi kuamekataliwa kuchukua fomu? Maana kuonesha nia, si kugombea. Pia kuchukua fomu, siyo kupitishwa na chama kupeperusha bendera ya chama katika nafasi unayoomba.
Tupunguze "assumptions hasa negative assumptions" naweza kuona wewe mwenye kuleta mada katika picha mbili

  1. Ni mwana CCM mzuri kwa hiyo unataka kutuaminisha kuwa CDM haina demokrasia kwa malengo yko na CCM
  2. Una maslahi binafsi na Zitto ambaye hajakutuma umtetee

Quality... Ubora hauzeeki
 
Ni haki yako kuandika hivyo ila ungetuonesha namna ulivyo critical analyst kama ungeanzia kuonesha democrasia ya chama tawala CCM. ungeanza kueleza namna walivyomfanya Samweli Sita alipochukua form kugombea tena uspika na baadae kuja na hoja isiyokuwepo ya kutaka spika awe mwanamke. Tuone uchaguzi mkuu ujao kama watakuja na hoja hiyo. Umeyanyamazia pia pale Kikwete alipopinduliwa na kuwekwa Mkapa kwa hoja nyepesi kwamba umri mdogo ilhali wakati anagombea na kupigiwa kura Halmashauri kuu wakijua umri wake. Unazungumzia udikteta lakini unasahau namna alivyoletewa zengwe Salim Ahmedi Salim na kuambiwa siraia wakati amekuwa balozi kwa miaka mingi tu. hayo ni machache tu ambazo ni rafu na udikteta uliokithiri ambao huuoni. inawezekana nawewe unagamba INABIDI UBANDULIWE.

Naam, hapa umenena na nimekusikia. Napenda hoja kama hizi.

CCM imekua kidemokrasia ndani ya chama. Kwa kuelewa kuwa safu ya CCM ni pana wamekuwa na utaratibu kupitia Demokrasia kuwapa makada nafasi za juu za uongozi mbali mbali. Makada vijana, wazee, wanaume na wanawake hupata nafasi za kushika nafasi hizo.

Tukianza na Samwel Sitta: Ni kada wa kueleweka anayeweza kushika nafasi yeyote ile ya juu Tokea Ubunge, w/kiti wa chama, waziri mkuu mpaka Uraisi. Ni kweli Kada huyu angeweza kuwa Spika mpaka kufa. Kada Makinda naye hali kadhalika, uzoefu wake katika uongozi na siasa hakuna atayejiuliza mara mbili. Kilichofanyika ni uamuzi wa pamoja wa chama kuwapa nafasi wanawake kwa kuelewa mchango wao mkubwa ndani ya CCM. La msingi hata hao wanawake walipambana na Kada Makinda alishinda kwa vidole na sio kwa kuachiwa, kuteuliwa kama mfalme. Hili ndilo la muhimu kabisa na linalothibitisha Kukua kwa Demokrasia ndani ya Chama.

Mkapa vs Kikwete: Kama nilivyosema awali kuwa safu ya CCM katika uongozi imenona. Wote hawa wamefanya kazi na mwalimu kwa miaka kadhaa katika nafasi mbali mbali za juu, hapa sina haja ya kueleza kwa wingi. Suala lilikuwa ni nani aanze na nani afuetie baadae. Unajua haiwezekani kuwa na maraisi wawili kwa wakati mmoja. Hivyo kwa kigezo cha umri (tena hakutofautiana sana) Kikwete akaombwa asubiri. Hata wakati wake Kikwete ulipofika, japo ya kuahidiwa ilibidi apitie test la kidemokrasia. Wengi waliruhusiwa kuchukua fomu, naye akapita kwa njia ya vidole.

Ingekuwa CHADEMA, kwa vile Kikwete aliahidiwa basi isingeruhusiwa kuwa na mpinzani, hakuna mwingine ambaye angeruhusiwa kuchukua fomu. Huku ni kukua kwa Demokrasia kukubwa sana. Mfano unaohitajiwa uigwe na vyama vyote vya upinzani, hususan CHADEMA ambao wako nyuma sana katika Demokrasia ndani ya chama.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom