Mzozo wa Mizozo
JF-Expert Member
- May 26, 2008
- 426
- 12
Nikiwa kama mteja wa Vodacom kwa kipindi kirefu, nilijiunga na utaratibu mzima wa tuzo point toka kipindi ulipoanzihwa na nikawa najikusanyia points nia na madhumuni ni kwamba nikusanye point nyingi zaidi ili nipate zawadi kubwa. Ni zaidi ya mwaka sasa natumaini umepita.
Kipindi chote natumia huo mtandao nipo katika moja Vodajaza na nimekuwa natumia 'almost' kiasi kile kile cha pesa kwa kila mwezi. Sasa tatizo limekuja kuanzia mwezi july mwaka huu ambapo points zimeanza shuka na pamoja na kujitahidi kuongeza matumizi bado zimeonekana kushuka kwa kasi ya ajabu. Nilijaribu kuongea na watu wa customer care wakaniambia kwamba kwa utaratibu wao, inapofika miezi kumi na nane zile point za mwezi wa kwanza zinatolewa katika point ulizokusanya, nilijaribu kuelewa hilo lakini kinachonitatiza ni kwamba pamoja na kuendelea kutumia kiwango kile kile cha pesa katika simu na wakati mwengine kuzidisha, toka mwezi wa saba points zimekuwa zinaenda chini tu kama situmii simu.
Malengo ya kupata zawadi kubwa zaidi yametokomea kabisa yaani na kila nikiangalia mwendo mzima wa hili suala la points naishia kusikitika tu. Kama ni kweli wanapunguza za ule mwezi wa kwanza tu baada ya mwezi wa kumi na nane nna hakika point zangu zingekuwa zinaongezeka kwa kiasi kidogo maana matumizi ya simu nimeyaongeza kwa asilimia 25 toka kipindi hicho, sasa badala yake zinapungua na inakuwa ni kama ssitumii simu siku hizi.
Mwenye ufaham zaidi juu ya hili tusaidiane.
Kipindi chote natumia huo mtandao nipo katika moja Vodajaza na nimekuwa natumia 'almost' kiasi kile kile cha pesa kwa kila mwezi. Sasa tatizo limekuja kuanzia mwezi july mwaka huu ambapo points zimeanza shuka na pamoja na kujitahidi kuongeza matumizi bado zimeonekana kushuka kwa kasi ya ajabu. Nilijaribu kuongea na watu wa customer care wakaniambia kwamba kwa utaratibu wao, inapofika miezi kumi na nane zile point za mwezi wa kwanza zinatolewa katika point ulizokusanya, nilijaribu kuelewa hilo lakini kinachonitatiza ni kwamba pamoja na kuendelea kutumia kiwango kile kile cha pesa katika simu na wakati mwengine kuzidisha, toka mwezi wa saba points zimekuwa zinaenda chini tu kama situmii simu.
Malengo ya kupata zawadi kubwa zaidi yametokomea kabisa yaani na kila nikiangalia mwendo mzima wa hili suala la points naishia kusikitika tu. Kama ni kweli wanapunguza za ule mwezi wa kwanza tu baada ya mwezi wa kumi na nane nna hakika point zangu zingekuwa zinaongezeka kwa kiasi kidogo maana matumizi ya simu nimeyaongeza kwa asilimia 25 toka kipindi hicho, sasa badala yake zinapungua na inakuwa ni kama ssitumii simu siku hizi.
Mwenye ufaham zaidi juu ya hili tusaidiane.