Mkuu BAK, usilalamike hilo tu, kuna watu kibao wana kesi na wako rumande kwa sababu kama hiyo. Mtuhumiwa ni haki yake kesi kusikilizwa mapema ili kama ana makosa afungwe na kama hana awe huru. Utasikia upelelezi haujakamilika miaka 3, kweli hii ni haki. Tena hiyo miaka yote mtu yuko rumande, kashindwa masharti ya dhamana. Suala lina baki pale pale wale waliopewa (TANU-CCM) nchi toka uhuru imewashinda. Na hii inatokana na kuwa na mazoea lolote watakalofanya watarudishwa madarakani, kwa kupenda ama kwa lazima (wizi wa kura).