Usaliti katika ndoa

Usaliti katika ndoa

mwakwetu

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2007
Posts
789
Reaction score
290
Habari wapendwa,
Njooni tulonge kuhusu hii mada hivi utafanyaje unapokugundua mkeo mpendwa anakusaliti? akaomba msamaha hatorejea?
 
ngoja nisikilize msaliti ya Christian Bella
 
Duuu jamani mambo ya uhusiano na mahusiano nimagumu saana. Yana siri kubwa kama kifo
 
Habari wapendwa,
Njooni tulonge kuhusu hii mada hivi utafanyaje unapokugundua mkeo mpendwa anakusaliti? akaomba msamaha hatorejea?

Wasuluhishi huwa tunatafuta factors zilizomfanya akasaliti!! Wakati mwingine anaweza kuwa alisaliti kwa sababu mwanaume ulikuwa harsh sana, umejisahau unapiga mzigo kama kuku, humpi pumziko, huna matunzo, huna heshima, mlevi kupindukia na familia kwako si lolote na mwisho unakuta na wewe ni malaya kupindukia.

Hapo unaweza kumsamehe but kama ulikuwa unajitahidi kwa yote lakini akasaliti hapo ni hakuna msamaha. Ni hayo tu
 
Habari wapendwa,
Njooni tulonge kuhusu hii mada hivi utafanyaje unapokugundua mkeo mpendwa anakusaliti? akaomba msamaha hatorejea?

Kwakuwa utakuwa umeshazaa naye watoto si vema kumurudisha makwao. Jitahidi kufanya kama alivyokufanyia. Kuanzia ulipogundua anza kutembea na kila mwanamke anayekuvutia hata kama ni dada yake, mamake, shangazi yake, wifi yake au rafiki yake na kama ana kaka shoga wee twanga tuuuu akikuuliza kulikoni mwambia ulianza wewe mimi namalizia.
 
namkumbuka mwana fa "ukiona mkeo kaliwa nawe tafuta mzembe ummegea aipunguzi maumivu ila inarudisha hadhi ya uwanaumeeee,
 
kujua ni kwa nini amesaliti hilo ni gumu, ni siri yake msaliti... ila unapokuwa umejitahidi kumridhisha kwa kila kitu na akakufanyia hivyo....
 
mleta mada amesema USALITI KTK NDOA...!
sasa naona mnaanza kuegemea kwa wanawake tu...!
usaliti ktk ndoa unavyanzo vingi...! lazma ziangaliwe sababu ktk pande zote...!

Mfano:-
kuna ndoa ya kaka mmoja imefika mahal ni shida, ME yuko bize kiasi aliwahi safir mtoto wake ametoka kuzaliwa baada ya wiki mbili tu akasafir ( tanzania hapahapa, yaan alikuwa anbadilisha mikoa tu) alirud mtoto anatembea (mwaka na miez mitatu) kakaa wiki mbili kasepa.

kwa hali hiyo ukisalitiwa utamlaumu nani?
 
Tamaa, na kukinai kwa ME hata KE.
Samehe but take care.
 
Na utakapogundua mmeo mpendwa anakusaliti na akaomba msamaha utafanyaje?:angry: Kila siku naona mke mke lloooooh
 
Back
Top Bottom