SautiYaMnyonge
JF-Expert Member
- May 13, 2018
- 439
- 742
Leo nilitembelea Ofisi za Nida Wilaya ya Ilemela ili kuona zoezi la upatikanaji wa namba za vitambulisho vya Nida linavyoendelea baada ya kupata taarifa kuna msongamano wa watu wengi.
Kwanza niwapongeze Ofisi zetu zote za Nida wakushirikiana na Ofisi ya Uhamiaji wanajitahidi Kwa kasi kubwa kuwahudumia wananchi ndio sababu Ofisi za Uhamiaji zimesogea hapo hapo Nida ili kurahisisha zoezi hilo, ila kuna changamoto moja kubwa ambayo nimeibaini watu wengi simu zao zitazimwa ifikapo tarehe 20/1/2020 kwa sababu tatizo liko Nida makao Makuu hawatoi namba za usajili Kwa wakati.
Leo nimeshuudia wananchi wengi waliosajili mapema tena mwanzoni kabisa lakini wakiangaliwa kwenye mfumo namba zao za usajili bado azijaandaliwa huko makao Makuu ya Nida ambako kuna mlundikano wa Majina ya Watu wengi ambao hawajapata namba zao.
Hii inaonesha mfumo uko taratibu sana kwa hiyo Kwa wale ambao awajapata namba zao na Nida wanakubali kwamba tatizo liko Makao Makuu kosa sio la Wananchi bali ni mfumo wa Nida wenyewe huko makao Makuu.
Hili jambo niiombe Serikali inayoongozwa na Rais wa Wanyonge Dkt.John Pombe Magufuli litazamwe upya kwani mpaka sasa watu zaidi ya Nusu ya watumiaji wa simu Nchi nzima hawana namba zao.
Ukweli ni kwamba haziko tayari wanaambiwa wasubiri kule Nida makao Makuu kuna Majina mengi yanaendelea kupewa namba. Kwa unyeti wa zoezi hili nashauri tuongeze muda kwani pia serikali itapoteza kodi kwa kiasi kikubwa sana kwani mpaka sasa kuna idadi inayokadiriwa zaidi ya watu milioni 17 hawajasajili kodi yao kwa siku au wiki kwa kutumia simu sio mchezo serikali itayakosa haya mapato. Utaratibu uwekwe upya mpaka Juni mwaka huu..
BY: DENNIS NYAMLEKELA KANKONO KATIBU WA SIASA NA UENEZI WA CCM WILAYA YA ILEMELA
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwanza niwapongeze Ofisi zetu zote za Nida wakushirikiana na Ofisi ya Uhamiaji wanajitahidi Kwa kasi kubwa kuwahudumia wananchi ndio sababu Ofisi za Uhamiaji zimesogea hapo hapo Nida ili kurahisisha zoezi hilo, ila kuna changamoto moja kubwa ambayo nimeibaini watu wengi simu zao zitazimwa ifikapo tarehe 20/1/2020 kwa sababu tatizo liko Nida makao Makuu hawatoi namba za usajili Kwa wakati.
Leo nimeshuudia wananchi wengi waliosajili mapema tena mwanzoni kabisa lakini wakiangaliwa kwenye mfumo namba zao za usajili bado azijaandaliwa huko makao Makuu ya Nida ambako kuna mlundikano wa Majina ya Watu wengi ambao hawajapata namba zao.
Hii inaonesha mfumo uko taratibu sana kwa hiyo Kwa wale ambao awajapata namba zao na Nida wanakubali kwamba tatizo liko Makao Makuu kosa sio la Wananchi bali ni mfumo wa Nida wenyewe huko makao Makuu.
Hili jambo niiombe Serikali inayoongozwa na Rais wa Wanyonge Dkt.John Pombe Magufuli litazamwe upya kwani mpaka sasa watu zaidi ya Nusu ya watumiaji wa simu Nchi nzima hawana namba zao.
Ukweli ni kwamba haziko tayari wanaambiwa wasubiri kule Nida makao Makuu kuna Majina mengi yanaendelea kupewa namba. Kwa unyeti wa zoezi hili nashauri tuongeze muda kwani pia serikali itapoteza kodi kwa kiasi kikubwa sana kwani mpaka sasa kuna idadi inayokadiriwa zaidi ya watu milioni 17 hawajasajili kodi yao kwa siku au wiki kwa kutumia simu sio mchezo serikali itayakosa haya mapato. Utaratibu uwekwe upya mpaka Juni mwaka huu..
BY: DENNIS NYAMLEKELA KANKONO KATIBU WA SIASA NA UENEZI WA CCM WILAYA YA ILEMELA
Sent using Jamii Forums mobile app