DVR- Ni kifaa cha kutunzia picha za video ambazo zimepigwa na Camera Kwa matumizi ya baadaye mara nyingi zinatumika kwenye ulinzi kwa kuunganisha na Closed Circuit TV - CCTV. DVR yenyewe haipigi picha...
Kwa kifupi... mfumo wenyewe uko hivi....
1. Unahitaji
Camera {moja au zaidi, nyingi na zilizowekwa kwenye pembe mbalimbali ndizo zina-guarantee fully coverage ya tukio}
2. Unahitaji kifaa cha kutunzia hizo picha zinazotoka kwenye camera nyingi... ambacho mara nyingi kinaitwa
DVR-- hii ni computer zenye Hard Disk yenye uwezo wa kuweka kumbukumbu nyingi. Na ina software malaaumu kwa ajili ya ku-play live tukio lolote ambalo unataka ku-rewind la Camera yoyote... Walinzi wa makampuni ya Ulinzi wanatumia sana. Au Wapiga Picha za Harusi wanatumia sana ku-rewind live kwenye tukio ambalo wamelipenda including kuweka slow motion. Mara nyingi kama unapenda ku-rewind matukio live lazima basi uweke Monitor/TV ya kuonyesha hayo matukio. Lakini kama huhitaji huna haja ya kuwa na monitor na kama unaamini mitambo yako kweli ina-record/tunza maana bila monitor huwezi kuverify kweli kama utunzaji unafanyika.
3.Kwa kuwa una Camera nyingi, unahitaji kuziunganisha kwenye hiyo DVR yako au kifaa cha kutunzia na ku-rewind picha kwa ajili ya ku-view... hapa unahitaji mfumo wa kuunganisha hizo camera zako zote kwenda kwenye DVR - Kwa maana nyingine unakuwa na Closed Circuit TV -
CCTV kwa ajili hiyo.
.
Mtu makini anaweza kukuambia ame-cover tukio kwa kusema idadi ya Camera alizotumia na Angle zilizowekwa. Kwa sababu hata bila DVR au CCTV ukiwa na Camera zako nyingi zenye DVD [Kifaa again cha kutunza] za kutosha na kama sio lazima kuona footage hapo kwenye tukio lenyewe huhitaji DVR au CCTV.
Kwa maana nyingi kitendo cha kwamba mnaongea kwa wiki sasa hamuongelei Camera za kuchukua matukio zilikuwa ngapi mnadanganyana tu.
Mfano mzuri. Kuwa na Latest DVR au na CCTV kwenye Harusi yako alafu usiwe na Camera... tuone kama utaambulia kitu...
Au uwe na Camera moja kwenye harusi yako... imeunganishwa kwenye latest worldclass DVR through CCTV alafu mpiga picha wako mwenye hiyo camera awe anapiga picha ndani ya hall/ukumbi alafu siku ya siku akuonyeshe picha za nje ya ukumbi wakati yeye muda wote alikuwa ndani ya ukumbi. Ati kwa sababu ya world class DVR au CCTV cabling.
Nilidhani niweke- Ukweli sawa.
"Mambo ya eti kutumia Satellite etc... Hauna maana yoyote..."
NB: Ukiwa na Latest DVR ku-review image footage za tukio ni suala la ku-click tu... muda gani? camera ipi? then you get everything huhitaji masaa, siku au ma-wiki.
Wapenzi wa Football au Wengine; Stadium zina CCTV system inayounganisha camera nyingi au zote zilizoko kwenye pembe mbalimbali za uwanja... kwenda kwenye DVR ku-record matukio yote... na mengine hata huyaoni kwenye TV yako, lakini ukitaka waweza onyeshwa almost kila kitu... Kwa sababu idadi ya picha zinazorikodiwa ziko sawa sawa na idadi ya Camera zilizoko uwanjani. Hivyo Stadiumu zina
Cameras, CCTV na DVR pamoja ndizo zinakuletea football live... Wengine Mlishawahi kusikia kwamba kuna mtangazaji akitamka kuna camera 200 au x... kwenye stadium Q, meaning accuracy ya matukio yote inasababishwa na Idadi ya kubwa ya Camera zilizosimikwa kila kona ya Uwanja mpaka nje ya Uwanja... sio DVR. DVR ni kwa jili ukubwa wa kutunza matukio tu.
Meaning of DVR from Wikipedia.
A
digital video recorder (
DVR), sometimes referred to by the merchandising term
personal video recorder (PVR), is a
consumer electronics device or
application software that records video in a digital format to a
disk drive,
USB flash drive, SD
memory card or other local or networked
mass storage device
Wateja wa DSTv wale wanaoweza ku-record program fulani na kucheki baadaye wanazo PVR.... recording events ambazo already zinaletwa na DSTv na kuangalia baadaye.
So DVR is something simple and not complicated like the way watu wanatoka mapovu navyo... na ukiwa na latest techonology DVR unaonyesha matukio instantly.
Mfano wa DVR ambazo wengine mnazo majumbani mwenu especially wateja wa DSTv wana PVR.
View attachment 99198
Note: Thread hii ni ya kuelimisha tu, haiko kupinga au ku-support chochote kinachoendelea kwenye Thread Zingine. Huenda kwa elimu hii ndogo mwaweza kujadili kwa hakika mambo yenu yanayoendelea.
Nawatakia siku njema na Mukamwombe Mungu.